Askari wawili wa Mamlaka ya Bandari
Tanzania(TPA), Jonas Bakari (25) na Hashim Salum (43) wamefikishwa mahakamani
kwa tuhuma za kumkata mtu mkono.
Akisomewa mashitaka, Mwendesha
Mashitaka, Vitalia Kidabulo mbele ya Hakimu Catherine Kioja alidai washitakiwa
hao walitenda kosa hilo Mei 30 mwaka huu katika geti la Mfuko wa
Maendeleo ya Jamii (TASAF).
Alidai washitakiwa hao walimkata
mkono wa kushoto Omary Hamza na kumsababishia maumivu huku wakijua kufanya
hivyo ni kosa kisheria.
Washitakiwa wote wako nje kwa
dhamana iliyowataka kuwa na wadhamini wawili kila mmoja na kiasi cha Sh milioni
moja kila mmoja na kesi itatajwa tena Juni 30 mwaka huu.
Katika tukio jingine, mkazi wa
Chanika, Shukuru Bakari (25) amefikishwa katika Mahakama ya Wilaya Ilala kwa
tuhuma za kulawiti mtoto wa miaka 11.
Akisomewa mashitaka yake na
Mwendesha Mashitaka Anunciath Leopold mbele ya Hakimu Mkazi
Mwandamizi, Hassan Juma, alidai mshitakiwa huyo alitenda kosa hilo
Septemba mwaka 2013 huko Chanika Wilaya ya Ilala.
Alidai mshitakiwa huyo alimlawiti
mtoto wa miaka 11 huku akijua kufanya hivyo ni kosa kisheria.
Mshitakiwa alikana mashitaka yake na
amerudishwa rumande mpaka Juni 26 mwaka huu kesi itakapotajwa tena.
No comments:
Post a Comment