Mtu
mmoja amefikishwa katika mahakama ya wilaya ya Ukerewe, Mwanza kwa tuhuma za
kukutwa akifanya mapenzi na mbuzi.
Mtuhumiwa
huyo, William Sebastian (21), mkazi wa Kijiji cha Mlezi alisomewa mashtaka hayo
mbele ya Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya wilaya hiyo, Faustine
Kishenyi.
Mwendesha Mashitaka wa
Polisi, Inspekta Samwel
Onyango aliieleza mahakama hiyo
kuwa mshitakiwa huyo alitenda kosa
hilo Juni 4 mwaka huu saa 9
alasiri huko Mlezi, Ukerewe.
Katika
hati ya mashitaka imeelezwa kuwa
mshitakiwa huyo alikutwa akitenda kosa hilo katika banda la mbuzi
nyumbani kwao na mmoja
wa wanafamilia.
Katika
maelezo hayo, Onyango alisema mwanafamilia huyo ambaye ni
mwanafunzi wa darasa la tatu katika
Shule ya Msingi Mlezi, baada ya
kushuhudia tukio hilo alikwenda kutoa taarifa kwa baba yao, Maxmilian Stephan aliyefika na kumkuta mtuhumiwa akiendelea
`kuhangaika' na mbuzi huyo.
Akifafanua, alisema
kosa hilo ni kinyume cha sheria
ya makosa la kujamiiana kifungu namba
K/F 154 (1) na (2) C sura ya 16
ya marekebisho ya sheria ya mwaka
2002.
Mtuhumiwa
amekana kutenda kosa hilo na amerudishwa rumande kwa kukosa wadhamini.
No comments:
Post a Comment