Kampuni
ya simu za mkononi ya Vodacom, Tanzania, imezindua ofa ya simu ya mkononi aina
ya Vodafone 875 yenye mfumo Adroid kuwezesha matumizi zaidi ya intaneti katika
jamii. Imesema simu hiyo itauzwa kwa Sh 100, 000.
Mkuu
wa Idara ya Masoko na Mawasiliano wa Vodacom Tanzania, Kelvin Twissa, alisema
hayo hivi karibuni, alipozungumzia utafiti uliofanywa kuhusu idadi ya watumiaji
wa simu za mkononi na intaneti kwa Afrika ya Mashariki.
“Simu
hii aina ya Vodafone 875 yenye mfumo Adroid inapatikana kwa Sh 100, 000 taslimu
katika maduka yote ya Vodacom. Ni ya kisasa imeunganishwa na 3G na inampatia
mteja uwezo wa kuperuzi mitandao ya Facebook, Whatsap, Twitter, Viber,
Instagram na mingineyo,” alisema Twissa.
Aliongeza;
“Mbali na uwezo wa simu hiyo inayopatikana kwa bei nafuu, mteja anunuapo simu
hiyo atapatiwa MB 500 na SMS 200 bure kwa kila mwezi ndani ya miezi sita
mfululizo. Ili kupata ofa hiyo, mteja atatakiwa kutuma neno CIMEI kisha kuacha
nafasi ikifuatiwa na namba ya CIMEI ya simu kwenda namba 15300”.
Akizungumzia
utafiti huo, alisema takwimu zinaonesha kwamba, Kenya inaongoza kwa maendeleo
ya mawasiliano ya simu na intaneti kwa nchi za Kusini mwa Jangwa la Sahara
ikifuatiwa na Tanzania, Uganda, Rwanda na Burundi.
Kwa
mujibu wa Twissa, takwimu za Julai mwaka jana, zinaonesha Kenya yenye
wakazi milioni 44, ina watumiaji wa simu za mkononi milioni 30.4 huku wa
intaneti wakiwa milioni 16.2 sawa na asilimia 41.
Tanzania
inafuata kwa kuwa na wakazi milioni 48.3 na watumiaji wa simu za mkononi
ni milioni 27.4 na wanaotumia intaneti ni milioni 5.31 sawa na asilimia 11
tu.
No comments:
Post a Comment