Naibu
Waziri anayemaliza muda wake wa Serikali za Mitaa nchini Malawi, Godfrey
Kamanya, amejiua kwa kujipiga risasi, baada ya matokeo ya awali ya kura za
ubunge, kuonesha ameshindwa kukomboa jimbo alilokuwa akishikilia la Lilongwe,
Msozi Kaskazini.
Waziri
huyo alijitoa uhai wake, jana saa 9.30 alfajiri akiwa nyumbani kwake Lilongwe.
Katika
ujumbe wake aliouacha baada ya kujiua unaoshikiliwa Polisi, Kamanya alisema
amechukua uamuzi huo kutokana na mkanganyiko wa kisiasa.
Mbali
na sababu za kuchukua uamuzi huo, Kamanya alibainisha namna anavyotaka mali
zake alizoacha zigawanywe, ambapo pia alimuomba Rais wa Malawi wa sasa, Joyce
Banda asaidie kumsomesha mtoto wake.
Hata
hivyo, baadhi ya ripoti zimeonesha kuwa Kamanya alikuwa akiishi kwa hofu,
kutokana na vitisho alivyokuwa akipata kutoka kwa watu wasiojulikana.
Kamanya
alikuwa mbunge wa jimbo hilo la Lilongwe, Msozi Kaskazini tangu alipojiunga na
chama cha PP.
Katika
matokeo yasiyo rasmi yaliyotolewa juzi, yalionesha kuwa Kamanya anashika nafasi
ya tano kati ya wagombea saba waliokuwa wakiwania jimbo hilo.
Matokeo
hayo yalionesha kuwa Kamanya alipata kura 1,738, wakati mmoja wa wapinzani
wake, kutoka chama cha Malawi Congress, Hilton Jiya, alikuwa amepata kura
4,625. Katika baadhi ya kata na vitongoji, Waziri huyo alikuwa akiambulia
kura zisizozidi 35.
Kwa
mujibu wa rafiki yake Kamanya, ambaye pia ni Waziri wa zamani wa Uchukuzi
nchini humo, Ulemu Chilapondwa, mke wake alipokea simu kutoka kwa mke wa
Kamanya, ikimtaarifu kuwa amesikia mlio wa risasi ukitokea katika chumba
ambacho mumewe alikuwa amejifungia.
Alisema
alipowasili nyumbani kwa marehemu akisaidiana na watu wengine wawili,
walifanikiwa kuvunja mlango wa chumba hicho, na walipoingia ndani walikuta
tayari Kamanya ameshakufa kwa kujipiga risasi kifuani.
Hata
hivyo, Polisi nchini humo, imesema kuwa inachunguza zaidi tukio hilo.
No comments:
Post a Comment