Kampuni
ya Kichina ya kuhuisha plastiki,
inayofanya shughuli zake jijini Dar es Salaam ya Fusun Investment United
Limited ina mpango wa kutanua shughuli
zake kwa kuwekeza zaidi nchini na kuongeza ajira zaidi kwa Watanzania.
Ilisema
hayo jana wakati wa ziara ya waandishi wa habari katika kiwanda cha kampuni
hiyo kilichopo Kurasini, ambacho tayari
kimetoa ajira zaidi ya 300 hadi sasa.
"Wakati
biashara yetu ikiendelea kutanuka, kuna uwezekano mkubwa wa sisi kuweza kuajiri
watu wengi zaidi," alisema Mkurugenzi wa kampuni hiyo, Jiang Jiaxing.
Alisema
kuwa kampuni hiyo, iliyoanzishwa tangu Desemba mwaka 2010 inakusanya tani 700
za chupa za plastiki kutoka mtaani kwa wananchi kila mwezi na kuzisaga kuwa
chakavu na kuzisafirisha kwenda China,
kutengeneza vifaa vya plastiki vipya.
Pia,
alisema kampuni yake imefungua viwanda viwili katika maeneo ya Mabibo na
Mikocheni jijini Dar es Salaam na mipango inafanyika ya kupanua shughuli zake
katika mikoa mingine vijijini.
"Tumechangia
katika uchumi wa Tanzania kwa njia nyingi, kama vile kuingizia nchini fedha za
kigeni, mapato kwa njia ya malipo ya kodi na ushuru na kuunga mkono jitihada za
serikali za utunzaji wa mazingira kwa kukusanya plastiki zinazozagaa ovyo kisha
kuhuisha," alisema na kuongeza: "Hebu tafakari, nini kingeweza
kutokea endapo tani 700 za chupa chakavu za plastiki, zingeachwa zikizagaa
mitaani? Ingelikuwa ni tatizo kubwa".
No comments:
Post a Comment