SENSA 2012 YAFICHUA IDADI KUBWA YA WATANZANIA NI WATOTO...

Baadhi ya watoto wa Kitanzania wakiwa darasani.
Sensa ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 inaonesha kuwa sehemu kubwa ya idadi ya watu  nchini ni watoto wenye umri wa chini ya miaka 15 na vijana.

Sensa hiyo inaonesha kuwa idadi ya Watanzania ni milioni 45, kati yao wanawake ni milioni 23 na wanaume milioni 21.9.  Tanzania Bara ina wanaume milioni 21.2 na wanawake milioni 22.4 na Zanzibar ina wanaume 630,677, wanawake 672,892.
Takwimu zilizotangazwa jana za Mgawanyo wa Watu kwa Umri na Jinsi zinaonesha asilimia 44  ni   wenye umri wa chini ya miaka 15. Kiasi hicho kinaelezwa kuwa juu kidogo ya wastani wa nchi za Afrika ambao ni asilimia 41. Uzinduzi huo ulifanywa na Makamu wa Pili wa Rais Zanzibar, Balozi Seif Ali Idd.
Mkurugenzi wa Idara ya Takwimu ya Taifa, Albina Chuwa alisema kwa mujibu wa utafiti wa Mama na Mtoto wa mwaka 2010 kiwango cha uzazi nchini ni wastani wa watoto 5.4 kwa kila mama mwenye umri wa kuzaa. Alisema asilimia 27 ya wanawake ambao wameolewa ndio wanaotumia uzazi wa mpango wa njia za kisasa.
Takwimu hizo pia zinaeleza kuwa kwa kila watu 10 wa Tanzania, wanne ni vijana  ambao umri wao ni kati ya miaka 15 na 35. Idadi ya kundi hilo ni asilimia 35 ambao idadi yao ni milioni 16. Mkoa wa Dar es Salaam una asilimia kubwa zaidi ya vijana huku Singida ikiwa na asilimia ndogo zaidi ya watu walio katika kundi hilo.
Sensa hiyo imebaini kuwa asilimia 52.2 ya watu nchini wana umri wa kufanya kazi ambao ni kati ya miaka 15 na 64 .  "Takwimu hizi zinaonesha kuwa rasilimali watu kwa ajili ya kuzalisha na kuongeza uchumi na kupunguza umasikini si tatizo nchini.”
Chuwa alisema kinachotakiwa ni watu kutumia fursa zilizopo kufanya kazi kwa bidii ili kuinua uchumi wa nchi. Alitaja mkoa unaoongoza kwa kuwa na watu wengi wa kufanya kazi kuwa ni  Dar es Salaam ambako kwa kila watu watatu, wawili wana umri wa kufanya kazi huku Simiyu  ikiwa na idadi ndogo ambayo ni asilimia 45.5.
Takwimu hizo zimebainisha kuwa idadi ya watu wenye umri wa miaka 60 na zaidi ambao ni wazee ni  milioni 2.5 sawa na asilimia 5.6. Mkoa unaoongoza kwa kuwa na wazee wengi ni Kilimanjaro ambao una asilimia 9.7 , Dar es Salaam ikiwa na wazee wachache sawa na asilimia 3.5.
Kundi la watu wanaoishi mijini limeongezeka hadi watu milioni 13.3 sawa na asilimia 30 na kuacha   wanaoishi vijijini wakiwa asilimia 70. Hii inaonesha kuwa idadi ya watu vijijini imepungua huku  mijini wakiongezeka kutoka asilimia 20 hadi 30.
Kutokana na takwimu hizo, uwiano wa watu wenye umri tegemezi unaendelea kuwa juu na kulingana na matokeo ya sensa hiyo karibu watu 92 hutegemea watu 100 wenye umri wa kufanya kazi.
Mkoa wa Simiyu una uwiano wa juu ambao ni  119.7, Mara ina 113.2, Geita na Rukwa 112.9 huku uwiano wa chini kabisa ukiwa Dar es Salaam yenye 50.8.
Balozi Idd  alisema kwa matokeo hayo ameziagiza wizara, idara na taasisi za Serikali kuboresha sera zilizopo kwa kutumia takwimu hizo kupanga mipango ya maendeleo.
"Takwimu hizi zimetufungua macho na masikio kwa kuonesha hali halisi ya idadi ya watu nchini, hivyo ziwe kichocheo cha kupanga maendeleo sahihi kwa wananchi wa Tanzania," alisema Balozi Idd.
Alisema takwimu hizo hazitakuwa na manufaa endapo hazitafikia walengwa. "Natoa mwito kwa viongozi wa Serikali zote mbili kutumia na kusambaza matokeo haya katika ngazi zote za utawala kwa kutumia lugha nyepesi ambayo inaeleweka kwa wengi ili kuwezesha wadau kupanga mipango sahihi ya maendeleo."

12 comments:

Anonymous said...

WOW just what I was searching for. Came here by searching for
デザイン

Anonymous said...

Post writing is also a fun, if you know then you can write if not it is complicated to write.

Anonymous said...

Fine way of telling, and good article to take facts about my presentation subject, which
i am going to present in institution of higher education.

Anonymous said...

You are so cool! I do not think I've read anything like
this before. So nice to discover another person with a few original thoughts on this issue.
Seriously.. many thanks for starting this up. This web site is something that is required on the web, someone with
some originality!

Anonymous said...

excellent points altogether, you just won a emblem new reader.

What may you recommend about your submit that you just made some days
ago? Any sure?

Anonymous said...

I visited many sites however the audio quality for audio songs present at this website is truly
excellent.

Anonymous said...

Neat blog! Is your theme custom made or did you download it from somewhere?

A theme like yours with a few simple adjustements would
really make my blog jump out. Please let me know where you got your design.
Kudos

Anonymous said...

I loved as much as you will receive carried out right here.
The sketch is attractive, your authored subject matter stylish.
nonetheless, you command get bought an edginess over that you wish
be delivering the following. unwell unquestionably come more formerly again since exactly the same nearly very often inside case you shield this increase.

Anonymous said...

Greetings, I believe your site could be having browser compatibility problems.

When I look at your site in Safari, it looks fine however, if opening in Internet Explorer, it's
got some overlapping issues. I just wanted to give you a quick heads up!

Apart from that, fantastic blog!

Anonymous said...

Great information. Lucky me I discovered your blog
by chance (stumbleupon). I have bookmarked it for
later!

Anonymous said...

Hello, I log on to your blog like every week. Your humoristic style
is witty, keep it up!

Anonymous said...

First off I want to say great blog! I had a quick question which
I'd like to ask if you don't mind. I was interested to find out how
you center yourself and clear your mind before writing.

I have had a tough time clearing my thoughts in getting
my thoughts out. I do take pleasure in writing however
it just seems like the first 10 to 15 minutes are generally
wasted just trying to figure out how to begin. Any recommendations or tips?
Cheers!