MWALIMU ALIYEMDHALILISHA MTOTO AKABILIWA NA KIFUNGO JELA...

Aaron Ledean.
Mwalimu wa zamani anakabiliwa na kifungo jela baada ya kufanya vitendo vya kujirudia vya udhalilishaji dhidi ya mvulana mwenye umri mdogo.
Baraza la wazee kwa kauli moja lilimtia hatiani Aaron Ledean kwa matukio matatu ya udhalilishaji dhidi ya mvulana chini ya miaka 20 katika miaka ya 1990.
Mwalimu huyo wa zamani wa sayansi tayari alishatiwa hatiani kwa makosa ya kunakili picha takribani 4,000 zinazodhalilisha mtoto.
Wazee wa baraza wameelezwa jinsi mwathirika huyo wa udhalilishaji - ambaye hawezi kutajwa kwa sababu za kisheria, sasa mtu mzima - alivyohisi 'vitendo vya furaha' wakati akiendelea kupondeka kwa nguvu katika bashasha, kwa shoga asiyejificha Ledean.
Alisema ilikuwa ni wakati mgumu katika maisha yake walipokuwa wakioneshana mapenzi kila mmoja.
Walikwenda kwenye mabaa katika 'siku yao ya kwanza' mjini Middlesbrough na kujihusisha na vitendo vya kimahaba walipokwenda kwenye sinema na wawili hao waliandaa ziara nyumbani kwa Ledean.
Kijana 'aliharibikiwa' pale Ledean baadaye alipovunja mahusiano hayo.
Miaka baadaye, kijana huyo alimkabili Ledean na kusema haikuwa muafaka kwa yeye kuwa katika nafasi ya kuwajibika moja kwa moja kwa watoto.
Ledean alikuwa mwalimu katika shule ya Teesside kwa miaka kadhaa. Mdai alisema matukio hayo yamekuwa akilini mwake kwa zaidi ya miaka na amekuwa huku akiamini kilichokuwa kimetokea hakikuwa sahihi.
Alifanyiwa ushauri nasaha na kuripoti suala hilo kwa polisi mwaka 2010. Ledean hakusemema chochote kuhusiana na madai hayo ya vitendo vya ngono au hatari iliyopo.  
Alisema alifikiria madhara lakini sio mvuto wa kimapenzi kwa kijana huyo na kusisitiza walikuwa ni marafiki tu.
Alisema anajutia sana kumkana kijana huyo, baada ya kijana huyo bila kutarajiwa kwenda nyumbani kwake akiwa na bunda la maua waridi.
Ledean mwenye miaka 40, amekana mashitaka matatu ya udhalilishaji katika kesi kwenye mahakama ya Teesside.
Lakini mwendesha mashitaka Shaun Dodds alidai kwamba Ledean alionesha hakuonesha kuvutiwa kimapenzi na wavulana wadogo.
Jaji Walford alimweleza Ledean, mkazi wa Crook, County Dyrham, kwamba jela haiepukiki, na kumsweka rumande hadi Machi 18.

No comments: