BINTI WA WHITNEY SASA NI SIGARA MTINDO MMOJA...

Binti wa Whitney Houston, Bobbi Kristina na rafiki yake wa kiume, Nick Gordon walikuwa wakivuta kwa fujo huku wakipokezana sigara mfululizo mikononi mwao mjini Atlanta juzi ... takribani mwaka mmoja tangu kifo cha mwimbaji huyo kutokana na kujizidishia dozi ya dawa za kulevya.
Haikufahamika kilichokuwamo ndani ya karatasi hizo zilizoviringwa.
Inavutia, kukumbukia mama wa Whitney, Cissy Houston jinsi ambavyo amekuwa akipigia kelele kusisitiza kwamba Bobby Kristina anaweza kufuata njia ya Whitney kwenye matumizi ya dawa za kulevya isipokuwa tu akibadilisha haraka mwenendo huo wa  maisha yake.
Bobbi amekuwa kwenye vita kali na bibi yake huyo kwa miezi kadhaa sasa ... na hivi karibuni alimshutumu Cissy kwa kuandika kitabu kinachoelezea kila kitu kuhusu Whitney.
Whitney alifariki dunia Februari 11, 2012 baada ya kutumia mchanganyiko wa dawa za kulevya uliohusisha cocaine, vidonge na bangi.

No comments: