JAJI AAHIRISHA KWA SIKU 60 ADHABU YA KIFO YA MFUNGWA WA KIKE...

KUSHOTO: Kimberly McCarthy. KULIA: Kitanda atakacholazwa Kimberly wakati wa kuchomwa sindano ya sumu.
Mauaji yaliyopangwa ya mfungwa wa kike mjini Texas yameahirishwa kwa siku 60 na Jaji kwenye jimbo la Lone Star.
Mauaji hayo, ambayo yalipangwa yafanyike baada ya Saa 12 juzi jioni (kwa saa za Marekani) inaweza kuwa ni mara ya kwanza kwa zaidi ya miaka miwili mfungwa wa kike kukabiliwa na adhabu ya kifo.
Kimberly McCarthy, mwenye miaka 51, alihukumiwa kifo kwa ujambazi wa mwaka 1997, kumpiga na kumchoma choma kwa kisu jirani yake mwenye miaka 71, Dorothy Booth - alikuwa akisubiria kuchomwa sindano maalumu ya sumu.
Profesa mstaafu wa saikolojia, wachunguzi wanasema Dorothy alikuwa amekubali kumpatia Kimberly kikombe cha sukari kabla ya kushambuliwa kwa kutumia kisu cha kukatia nyama nyumbani kwake mjini Lancaster, takribani maili 15 (kilometa 24) kusini mwa Dallas.
Ilikuwa ni kati ya mikato mitatu ilihusishwa kwa Dorothy, mkunga wa jadi ambaye amekuwa akihusishwa na upenyezaji cocaine.
Sindano yake ya sumu ilikuwa imepangwa achomwe jana usiku.
Kimberly atakuwa mwanamke wa 13 kuhukumiwa kifo katika Marekani na wa nne mjini Texas, jimbo lenye hukumu nyingi zaidi za kifo nchini humo, tangu Mahakama Kuu kuruhusu adhabu za kifo kuendelea mwaka 1976.
Katika kipindi hicho, zaidi ya wafungwa wa kiume 1,300 wamehukumiwa kifo katika nchi nzima.
Takwimu zilizokusanywa kutoka mwaka 1980 hadi 2008 zinaonesha wanawake ni asilimia 10 tu ya washitakiwa wote wa mauaji ya biandamu kote nchini humo.
Kimberly ni mke wa zamani wa Aaron Michaels, muasisi wa New Black Panther Party, na alichunguzwa kwa niaba yake. Waliachana kabla ya mkasa huu wa Dorothy.
the New Black Panther Party ni miongoni mwa wanawake 10 walioko kwenye foleni ya kusubiria kutekelezwa kwa hukumu zao za vifo mjini Texas, lakini ni yeye pekee ambaye ametajiwa tarehe ya kifo chake.
Mwaka 1998, Karla Faye Tucker, mwenye mwenye miaka 38, alikuwa mwanamke wa kwanza kuuawa mjini Texas tangu vita vya wenyewe kwa wenyewe kwa ajili ya ujambazi mjini Houston ambako watu wawili waliuawa.
Miaka miwili baadaye, bibi mwenye maiak 62, Betty Lou Beets, alidungwa sindano ya sumu kwa kumcharanga mapanga mumewe wa tano huko kaskazini-mashariki mwa Texas ili asombe fedha za bima na mafao yake ya pensheni.
Na mwaka 2004, Frances Newton mwenye miaka 40, aliuawa kufuatia mauaji ya kuwakata visu mumewe na watoto wawili mjini Houston mwaka 1987.
Takribani wafungwa wanaume wanane Texas wanasubiria kutekelezwa kwa hukumu zao za kifo katika miezi michache ijayo.

No comments: