MWIMBAJI WA KIBAO CHA "RESCUE ME" AFARIKI DUNIA...

  
Mwimbaji Fontella Bass, aliyejizolea umaarufu mkubwa kutokana na kibao chake kilichotikisa mno mwaka 1965 cha "Rescue Me" amefariki dunia juzi Jumatano mjini Missouri. Amefariki akiwa na umri wa miaka 72.
Kwa mujibu wa familia ya Fontella, mwimbaji huyo alifariki katika Hospitali ya St. Louis kutokana na matatizo aliyokuwa akisumbuliwa nayo kufuatia ugonjwa wa moyo aliopata wiki tatu zilizopita. Bass pia amekuwa akikumbwa na maradhi ya kupooza mara kwa mara tangu mwaka 2005.
Nyota huyo wa miondoko ya R&B ametamba na vibao vyake kadhaa katika maisha yake ya muziki ikiwa ni pamoja na "You'll Miss Me (When I'm Gone)" na "Don't Mess Up a Good Thing" -- lakini hakuna kilichofikia mafanikio ya juu kama "Rescue Me."

No comments: