"SHARO MILIONEA" AFARIKI DUNIA KWA AJALI YA GARI...

  
Habari zilizotufikia hivi punde zinasema kuwa msanii wa muziki wa kizazi kipya na mwigizaji maarufu wa filamu nchini, Hussein Mkiety maarufu kama Sharo Milionea amefariki dunia usiku wa kuamkia leo kwa ajali ya gari iliyotokea maeneo ya Muheza, mkoani Tanga.
Kwa mujibu wa chanzo chetu cha habari, Sharo alikuwa akitoka Dar es Salaam kuelekea kijijini kwao Lusanga, Muheza kwa usafiri wa gari binafsi aina ya Toyota Harrier ndipo alipopatwa na ajali hiyo iliyokatisha maisha na ndoto zake majira ya Saa mbili usiku.
Sharo alitamba sana katika tasnia ya filamu nchini ambapo alifanikiwa kuwateka mashabiki kwa 'swagga' zake za 'Kamata mwizi meeeeen!" na pia alipogeukia fani ya muziki ameweza kutamba na vibao vyake kadhaa kikiwamo cha 'Chuki' alichomshirikisha Brazamen Dully Sykes.
Hivi karibuni amekuwa kivutio kikubwa kiasi cha kushirikishwa katika video mbalimbali za wasanii wa Bongo Flava huku akishiriki pia katika kucheza filamu kadhaa zinazotikisa kwa sasa.
Tunaungana na familia ya marehemu katika kipindi hiki kigumu na tunaahidi kuwaletea taarifa zaidi kuhusu mkasa mzima ulivyotokea. Endelea kuperuzi "ziro99blog".

No comments: