BOBBI KRISTINA ANUSURIKA KATIKA AJALI MBAYA YA GARI...

Binti wa Whitney Houston, Bobbi Kristina amenusurika kimiujiza baada ya kuliharibu gari lake aina ya Chevy Camaro kwenye ajali mbaya muda mfupi uliopita.
Ajali hiyo ambayo imetokea Alpharetta, mjini Georgia, vyanzo vya habari vimeeleza mtembea kwa miguu aligundua gari la Bobbi likiwa limepondeka na hivyo akapiga simu polisi.
Wakati wafanyakazi wa huduma ya dharura walipowasili eneo la tukio, Bobbi Kristina alikuwa kasimama kando la gari lake na alionekana hakujeruhiwa popote.
Polisi walifanya uchunguzi rasmi kujua chanzo cha ajali -- na kuamini kwamba Bobbi Kristina alishindwa kulimudu gari lake wakati akipinda kona kuelekea nyumbani kwake ... na kugonga kizuizi kisha kugonga miti kadhaa hadi bondeni.
Baada ya uchunguzi, polisi walimpa Bobbi Kristina dondoo la usalama kwa "kushindwa kumudu njia."
Polisi wamesema ... haionekani kama matumizi ya dawa za kulevya ama pombe kuwa chanzo cha ajali hii.
Alipofuatwa Bobbi Kristina hakutaka kusema chochote kuhusiana na ajali hiyo.

No comments: