Mfanyabiashara Salim Abri (kulia) katika picha ya pamoja na viongozi mara baada ya kukabidhi mifuko hiyo ya saruji. |
Salim Abri (wa pili kulia) akikabidhi mifuko 200 ya saruji kusaidia ujenzi wa mabweni wilayani Kilolo. |
Akikabidhi msaada huo ofisini kwake, Asas ambaye pia ni Kamanda wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) mkoa wa Iringa, alisema kuwa amelazimika kuchangia ujenzi huo wa mabweni ikiwa ni sehemu ya kuiunga mkono serikali iliyopo madarakani chini ya Rais Jakaya Kikwete katika kuinua kiwango cha elimu ambapo elimu imekuwa ikipewa kipaumbele zaidi.
Alisema kuwa mbali ya kuchangia ujenzi huo katika wilaya ya Kilolo pia ameshafanya hivyo katika Halmashauri ya Manispaa ya Iringa na maeneo mengine ya mkoa wa Iringa.
Alisema kuwa wilaya ya Kilolo kupitia kwa Mkuu wa Wilaya waliandika barua kwake kuomba kusaidiwa ujenzi wa Shule za Sekondari na mabweni katika wilaya hiyo ya Kilolo.
Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Kilolo, Gerald Guninita mbali ya kumpongeza Asas ambaye pia ni mmoja kati ya wafanyabiashara wakubwa mkoani Iringa, aliwaomba wadau zaidi wa elimu katika mkoa wa Iringa wakiwemo wafanyabiashara kujitokeza kuchangia maendeleo ya elimu katika wilaya hiyo ya Kilolo.
Hata hivyo mkuu huyo wa wilaya alisema kuwa saruji hiyo itagawanywa mifuko 50 kwa shule nne za sekondari ambazo zinaendelea na ujenzi wa mabweni ya wanafunzi wa kike.
Alizitaja shule za sekondari ambazo zitanufaika na msaada huo kuwa ni Uhambingeto, Gangwa, Ukwega na Masisiwe.
No comments:
Post a Comment