BAJETI YA WIZARA YA UCHUKUZI KWA MWAKA 2012 - 2013...


HOTUBA YA WAZIRI WA UCHUKUZI, MHESHIMIWA DKT. HARRISON G. MWAKYEMBE (MB), AKIWASILISHA BUNGENI MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI YA FEDHA KWA MWAKA 2012/2013

A.UTANGULIZI
Mheshimiwa Spika, baada ya Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu kuweka mezani taarifa ya Kamati mbele ya Bunge lako Tukufu, naomba kutoa hoja kwamba Bunge lako sasa likubali kupokea, kujadili na kupitisha Mpango na Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha ya Wizara ya Uchukuzi kwa mwaka wa fedha 2012/2013.  
Mheshimiwa Spika, awali ya yote naomba nichukue fursa hii adhimu kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kutujalia uhai na kutuwezesha leo hii kutafakari kwa pamoja kuhusu Sekta ya Uchukuzi na maendeleo ya Taifa letu kwa ujumla. 
Mheshimiwa Spika, napenda kumpongeza Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuendelea kuiongoza nchi yetu na kusimamia utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2010 kwa umakini na umahiri mkubwa. Nawapongeza vilevile Mhe. Dkt. Mohamed Gharib Bilal, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mhe. Mizengo Kayanza Peter Pinda, Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kwa uchapakazi na uongozi wao thabiti. 
 Mheshimiwa Spika, niruhusu sasa nitoe shukrani zangu za dhati kwa Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kwa kuniamini na kuniteua kuwa Waziri wa Uchukuzi. Aidha, napenda kuwashukuru Watanzania wa dini zote kwa kuendelea kuniombea na matokeo yake yanaonekana; afya yangu inaendelea kuimarika siku hadi siku kwa neema ya Mwenyezi Mungu. Sijawasahau wapiga kura wangu wa jimbo langu la uchaguzi la Kyela kwa kuniombea na kunivumilia kipindi chote nilichokuwa sijiwezi na kuendelea kunipa ushirikiano katika kutekeleza shughuli mbalimbali za maendeleo ya Taifa na Jimbo la Kyela.  
Mheshimiwa Spika, naomba vilevile kumpongeza Mhe. Dkt. Charles John Tizeba, Mbunge wa Buchosa kwa kuteuliwa kuwa Naibu Waziri wa Uchukuzi. Mhe. Dkt Tizeba amekuwa msaada mkubwa kwangu katika kusimamia sekta ya uchukuzi na kuhakikisha kuwa sekta hii inachukua nafasi yake muhimu katika kuchochea ukuaji wa uchumi wa nchi. Nitumie nafasi hii kuwapongeza Waheshimiwa mawaziri na naibu mawaziri wote walioteuliwa kuongoza Wizara mbalimbali. Aidha, napenda kuwapongeza Waheshimiwa Wabunge wote waliojiunga na Bunge hili kwa njia ya kuchaguliwa au kuteuliwa katika mkutano huu wa nane (8) na kuwatakia kila la kheri wabunge tisa (9) tuliowachagua ndani ya Bunge hili kutuwakilisha katika Bunge la Afrika ya Mashariki.
Mheshimiwa Spika, naungana na wabunge wenzangu kwa majonzi makubwa katika kutoa pole kwa viongozi wa Taifa letu na wananchi wote  kwa ujumla kwa msiba mkubwa uliolisibu Taifa kutokana na ajali ya Meli ya MV Skagit iliyotokea karibu na kisiwa cha Chumbe tarehe 18 Julai 2012 na kusababisha vifo na majeraha ya kimwili na kisaikolojia kwa abiria waliokuwa katika meli hiyo. Mungu azilaze roho za marehemu mahali pema peponi na awape ahueni ya haraka wale wote waliojeruhiwa- Amina.
Mheshimiwa Spika, naomba nihitimishe salaam zangu kwa kuungana tena na Waheshimiwa Wabunge wenzangu kumpongeza Mhe. Mizengo Kayanza Peter Pinda, Waziri Mkuu na Mbunge wa Katavi, Mhe. Dkt. William Mgimwa, Waziri wa Fedha na Mbunge wa Kalenga na Mhe. Stephen Masatu Wasira, Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (Mahusiano na Uratibu) na Mbunge wa Bunda kwa hotuba zao zilizotoa mwelekeo wa jumla wa mipango na bajeti ya Serikali kwa kipindi cha mwaka wa fedha 2012/2013. Hotuba ya Mhe. Waziri Mkuu imeeleza kwa ujumla utekelezaji wa shughuli za Serikali, mipango na mikakati inayolenga kuimarisha na kuboresha huduma za jamii. Baada ya maelezo ya jumla ya Mhe. Waziri Mkuu, ni jukumu langu sasa kutoa ufafanuzi wa kina kuhusu utekelezaji wa mipango ya maendeleo kwa mwaka wa fedha 2011/2012, mikakati na mwelekeo wa Sekta ya Uchukuzi katika mwaka 2012/2013. 
Mheshimiwa Spika, sina budi kuishukuru Kamati ya Bunge ya Miundombinu chini ya Mwenyekiti wake Mhe. Peter Joseph Serukamba, Mbunge wa Kigoma Mjini na Makamu Mwenyekiti wa Kamati Mhe. Anne Kilango Malecela, Mbunge wa Same Mashariki kwa kuendelea kunipa ushirikiano katika kuiongoza Sekta  hii. Ushauri na maelekezo yao mazuri yameisaidia Wizara yangu kuboresha mipango na utendaji wake. Binafsi nina imani kubwa na Kamati hii na naomba kuihakikishia kuwa Wizara itaendelea kutoa ushirikiano wa karibu katika utekelezaji wa majukumu yake.  
Mheshimiwa Spika, baada ya maelezo hayo ya utangulizi, napenda sasa kuchukua nafasi hii kufanya mapitio ya utekelezaji wa mipango ya Wizara ya Uchukuzi kwa mwaka wa fedha 2011/2012 na kutoa maelezo kuhusu malengo na makadirio ya bajeti ya Wizara kwa mwaka 2012/2013. 

B. MAPITIO YA UTEKELEZAJI WA MIPANGO YA WIZARA KWA MWAKA 2011/2012 NA MALENGO YA MWAKA 2012/2013. 
Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2011/2012, Wizara iliendelea na jukumu la kuandaa na kusimamia utekelezaji wa Sera za sekta na kufanya tathmini ya utendaji wake ili kuhakikisha kuwa majukumu yaliyopangwa yanatekelezwa kwa ufanisi. Aidha, katika kipindi hicho Wizara iliendelea na utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2010 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa wa Miaka mitano. 

Ubunifu na utekelezaji wa Sera za Sekta
Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2011/2012 Wizara ilifanya mapitio ya Sera ya Taifa ya Uchukuzi ya mwaka 2003 na kuandaa mkakati wa utekelezaji wake. Aidha, Rasimu ya Sera ya Hali ya Hewa iliwasilishwa Serikalini na kutolewa maelekezo ambayo yamefanyiwa kazi. Rasimu za Sera hizi zinatarajiwa kupitishwa katika mwaka wa fedha 2012/2013. 

Urekebishaji wa Taasisi za Wizara 
Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2011/2012, Wizara kwa kushirikiana na Shirika Hodhi la Mali za Serikali (Consolidated Holding Corporation–CHC) na wadau wengine iliendelea na zoezi la kurekebisha taasisi zilizo chini yake. Kwa upande wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari, ushirikishaji wa sekta binafsi umesaidia katika kuhudumia meli zinazobeba makasha katika Bandari ya Dar es Salaam, ujenzi na uendeshaji wa yadi za kuhifadhi makasha na magari ambao umepunguza tatizo la mlundikano na msongamano wa makasha na meli katika Bandari ya Dar es Salaam. Hadi sasa kuna yadi za kuhifadhi makasha 10 zenye uwezo wa kuhifadhi makasha 9,000 na vituo 4 vyenye uwezo wa kuhifadhi magari 5,000 kwa wakati mmoja.
Mheshimiwa Spika, Kampuni ya Reli Tanzania (TRL) sasa inamilikiwa na Serikali kwa asilimia 100 baada ya kuvunjika kwa mkataba wa ubia  kati ya  Serikali na RITES kutoka India tarehe 22 Julai, 2011. Pamoja na zoezi hili kukamilika Serikali imeipokea TRL ikiwa katika hali duni ya utendaji, vitendea kazi (ikiwa ni pamoja na injini za treni, mabehewa ya mizigo na ya abiria, mitambo na mashine mbalimbali) vingi vikiwa vimechakaa, vikihitaji matengenezo makubwa na ya haraka. Ili kukabiliana na hali hiyo, Serikali imeazimia kuwekeza katika kampuni ya TRL kupitia bajeti yake, mikopo pamoja na kushirikisha sekta binafsi.
Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2011/2012, Wizara imeendelea kuisaidia Kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL) ili iendelee kutoa huduma za usafiri wa anga na iweze kujiendesha kibiashara. Mbali na kuitengea ATCL fedha kwenye bajeti yake, Wizara imebadili uongozi wa juu wa Kampuni hiyo na kuteua bodi mpya ya Wakurugenzi kwa lengo la kuimarisha utendaji na kurejesha nidhamu na uadilifu katika usimamizi na matumizi ya rasilimali. 
Mheshimiwa Spika, Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Kilimanjaro (KIA) nacho kimerejeshwa kwenye umiliki na uendeshaji wa Serikali kwa asilimia 100 baada ya kuvunjika kwa Mkataba wa ubia kati ya Serikali na wanahisa wengine mwezi Septemba, 2009. Kampuni ya Kilimanjaro Airports Development Company (KADCO) iliyopewa uendeshaji wa kiwanja hicho kwa miaka 25 ilikuwa na wanahisa wanne ikiwemo Serikali yenyewe iliyokuwa na asilimia 24 ya hisa, Kampuni ya Mott MacDonald International ya Uingereza iliyokuwa na asilimia 41.4 ya hisa, Kampuni ya South Africa Infrastructure Fund (SAIF) iliyokuwa na asilimia 30 ya hisa na Kampuni ya Inter Consult ya Tanzania iliyokuwa na asilimia 4.6 ya hisa. Mwaka 2009 Serikali iliamua kununua hisa zote zilizokuwa zinamilikiwa na  wanahisa wengine wa Kampuni baada ya kutoridhika na utekelezaji wa Mkataba uliosainiwa. Hivyo, kama nilivyodokeza awali, KADCO kwa sasa inamilikiwa na Serikali kwa asilimia 100 na inaendelea na jukumu la kukiendesha Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Kilimanjaro (KIA).
Mheshimiwa Spika, Serikali imefanikiwa kupata mkopo wenye masharti nafuu wa shilingi bilioni 51 kutoka Taasisi ya misaada iitwayo “ORIO Grant Facility” ya Uholanzi. Fedha hizi zitatumika kukarabati njia ya kurukia na kutua ndege (runway), maegesho ya ndege (apron), barabara za viungio (taxiways) na uboreshaji wa jengo la abiria. Kazi inayofanyika kwa sasa ni usanifu na uandaaji wa michoro ya miundombinu na jengo. Mradi huu unatarajia kuanza mwaka 2013 na utakamilika katika kipindi cha miaka mitatu (3). Kukamilika kwa ujenzi huo kutaiwezesha KADCO kukabiliana na ongezeko la abiria na ushindani wa soko.

HUDUMA ZA UCHUKUZI KWA NJIA YA NCHI KAVU
Usafiri na Uchukuzi wa Reli  
Mheshimiwa Spika, pamoja na maelezo yangu mafupi ya awali kuhusu umiliki wa TRL, nalazimika kurudi nyuma kidogo ili changamoto zinazokabili usafiri na uchukuzi wa reli leo hii zieleweke vema na hivyo kutoa fursa pana ya ushauri wa namna ya kuzikabili changamoto hizo kikamilifu. Kwa miaka takriban 15, usafiri na uchukuzi wa reli nchini umepitia misukosuko mikubwa ya kisera na kiuendeshaji ambayo athari zake tunaziona hadi leo. Kwanza, mwaka 1997 Shirika la Reli Tanzania (TRC) wakati huo, liliorodheshwa miongoni mwa mashirika ya kubinafsishwa. Hatua hiyo ilipelekea TRC kutotengewa fedha yoyote ya maendeleo kwenye Bajeti ya nchi kwa matarajio ya kumpata mwekezaji mzuri wa kulifufua na kuliendeleza shirika hilo. Ikatuchukua miaka 10 kumpata mwekezaji, kampuni ya RITES kutoka India, ambayo ilinunua asilimia 51 ya hisa ndani ya TRL
Pili, Mheshimiwa Spika, miaka mitatu (3) ya uwepo wa RITES ndani ya TRL haikuzaa matunda yaliyotarajiwa. Badala yake huduma zikazorota zaidi, uwekezaji katika miundombinu pamoja na vichwa na mabehewa ya treni haukufanyika ipasavyo na hata uwezo wa ndani wa TRL wa kukarabati injini na mabehewa ya treni ukadorora kutokana na mikakati ya makusudi ya RITES kutumia fedha zilizotafutwa na wanahisa kukarabati na kukodi injini na mabehewa nchini India badala ya kutumia karakana za TRL kutengeneza injini na mabehewa yaliyokuwepo. Aidha, kinyume na makubaliano ya mkataba ya ukodishaji, njia ya reli haikufanyiwa matengenezo stahiki kutokana na RITES kukosa utayari wa kuwekeza.
Tatu, Mheshimiwa Spika, mvua kubwa zilizonyesha nchini mwezi Desemba 2009 na mwanzoni mwa mwaka 2010 zilisababisha uharibifu mkubwa katika maeneo 32 ya njia ya reli kati ya Kilosa na Gulwe, umbali wa kilometa 83 na kulazimu huduma za usafirishaji abiria na uchukuzi wa mizigo kusitishwa kwa muda wa miezi sita(6).  Matengenezo makubwa na ya dharura yakafanyika (restoration works) na kuwezesha njia ya reli kufunguliwa mwezi Juni 2010.
Nne, Mheshimiwa Spika, mvua zingine kubwa zikanyesha katikati ya mwezi Desemba 2011 katika maeneo ya Kibakwe na Wota wilaya ya Mpwapwa, na kusababisha mafuriko makubwa yaliyoathiri tena miundombinu ya reli kati ya stesheni za Godegode na Gulwe. Mvua hizo zilisababisha mafuriko kwenye mito ya Mzase, Kidibo, Ikuyu, Luhundwa, Kidenge, Mingui, Onjereza na Wota. Mito hii hukatiza reli karibu na stesheni ya Godegode, eneo la Kidibo na eneo la karibu na stesheni ya Gulwe. Eneo hili la Kilosa hadi Gulwe liko katika bonde lililo sambamba na mto Mkondoa kwa zaidi ya kilomita 80. 
Mheshimiwa Spika, matukio yote haya ndani  ya miaka 15 ya usafiri na uchukuzi wa reli, yamekuwa na athari kubwa katika maendeleo ya sekta hii muhimu katika uchumi wa nchi. Pamoja na changamoto zote hizo zilizolazimu, pamoja na mambo mengine, kusitishwa kwa treni za abiria kwenda Mwanza, Dodoma kwenda Singida mwaka 2009 kutokana na uhaba wa mabehewa na injini na kusitishwa kwa muda kwa treni za abiria na mizigo kutoka Dar es Salaam kwenda Kigoma, katika vipindi nilivyovielezea vya mafuriko kwenye reli ya kati, kupungua kwa kiasi kikubwa kwa mzigo unaosafirishwa kwa treni kutoka tani milioni 1.445 mwaka 2002 mpaka tani 267,008 mwaka 2011, TRL na Kampuni Miliki ya Rasilimali za Reli nchini (RAHCO) zimefanya kazi kubwa katika kipindi kifupi cha miezi 12 tu kurejesha uhai katika usafiri na uchukuzi wa reli. Nguvu kubwa tuliyonayo ni rasilimali watu. Tuna wafanyakazi wazalendo TRL na RAHCO wenye ari ya kufanyakazi na ujuzi mkubwa unaorutubishwa na uzoefu wa muda mrefu wa kufufua chochote kile kinachotambaa kwenye reli.
Mheshimiwa Spika, kwa sasa TRL ina injini za treni 20 tu zinazofanya kazi kwenye njia kuu na injini 24 zimesimama kutokana na uchakavu pamoja na kukosa matengenezo muhimu katika miaka hiyo ya nyuma. Injini 20 zinazofanya kazi zimekuwa zikiharibika mara kwa mara ziwapo safarini kutokana na uchakavu na kukosekana kwa vipuri asilia kwani viwanda karibu vyote vilivyotengeneza treni zetu havipo tena au vimeingia kwenye teknolojia mpya na tofauti kabisa ya teknolojia ya magari moshi tuliyonayo. Kwa upande wa mabehewa ya mizigo Kampuni ina mabehewa 638 yanayofanya kazi na mabehewa 719 ni mabovu. Kati ya mabehewa mabovu, mabehewa 330 yanaweza kukarabatiwa na kufanya kazi. Aidha, kampuni ina mabehewa ya abiria 45 yanayofanya kazi na mabehewa 52 ni mabovu ambayo kati yake mabehewa 31 yanaweza kukarabatiwa na kufanya kazi. Kazi ya ukarabati imeshaanza, itaongeza kasi mara baada ya Bunge hili tukufu kupitisha Bajeti yetu.
Mheshimiwa Spika, ili kuimarisha na kuboresha utendaji wa TRL, Wizara imetenga shilingi bilioni 104 katika bajeti ya mwaka 2012/2013. Fedha hizi zitatumika kutekeleza miradi mbalimbali ikiwa ni pamoja na kuzijenga upya (re-manufacture) injini za treni nane (8) aina ya 88xx, kufanya malipo ya awali ya ununuzi wa injini za treni mpya 13, kufanya malipo ya awali ya ununuzi wa mabehewa mapya ya abiria 22, kukarabati mabehewa mabovu ya mizigo 125, kufanya malipo ya awali ya ununuzi wa mabehewa mapya ya mizigo 274, kufanya malipo ya awali ya ununuzi wa mabehewa mapya ya breki 34 na ukarabati wa karakana za Tabora na Dar es Salaam. Katika fedha hizo shilingi bilioni 18.9 zimetengwa kwa ajili ya kulipa madeni ya kimikataba na IFC, RITES, RVR (Uganda) na wadai wa hapa nchini. Fedha hizo zikitolewa kwa wakati zitaiwezesha TRL kutekeleza mipango yake kwa wakati uliopangwa ili kuiwezesha kutoa huduma inayotarajiwa. Ni matumaini ya Wizara kuwa uwezweshwaji huu kifedha utaongeza idadi ya treni za abiria kutoka Dar es Salaam kwenda Kigoma kufikia treni tatu (3) kwa wiki ifikapo mwishoni mwa mwaka huu na kurejesha huduma ya treni za abiria kwenda Mwanza mara tatu kwa wiki kabla ya mwisho wa mwaka huu.
Mheshimiwa Spika, kwa upande wa RAHCO kazi kubwa ya kukinga tuta la reli dhidi ya mmomonyoko inaponyesha mvua kubwa (protection works) katika maeneo 32 kati ya stesheni za Kilosa na Gulwe yaliyoathirika kwa mvua za Desemba 2009 na mwanzoni mwa 2010 na mvua za Desemba 2011, na vilevile kazi ya kurudisha mto Mkondoa kwenye njia yake (river training) inaendelea vizuri na inategemewa kukamilika mwezi Septemba mwaka huu. Aidha, RAHCO imesaini mkataba na mkandarasi China Civil Engineering Construction Company (CCECC) kwa ajili ya ujenzi wa madaraja mawili yaliyoharibiwa au kuchukuliwa na mafuriko ya 2009/2010 yaliyopo km 293 na km 303 kati ya Kilosa na Gulwe. Kazi ya ujenzi wa madaraja haya mawili itakayogharimu shilingi bilioni 10.85 ilianza tarehe 25 Juni 2012  na inatarajiwa kumalizika  mwezi Oktoba 2013.
Mheshimiwa Spika, maeneo mengine ya miundombinu ya reli ya Kati yaliyoharibiwa na mvua za mwaka 2010/2011 ni pamoja na daraja lililopo km 517.2 kati ya Stesheni za Bahi na Kintinku. Kazi ya ujenzi wa daraja ilianza mwezi Juni 2012 na inatarajiwa kukamilika Aprili 2013. Ujenzi wa daraja hili unaofanywa na kampuni ya CCECC utagharimu shilingi bilioni 3.6.
Mheshimiwa Spika, tatizo la uharibifu wa miundombinu ya reli katika eneo la  Kilosa hadi Gulwe linasababishwa kwa kiasi kikubwa na  shughuli za binadamu hususan kilimo kinachoambatana na ukataji wa miti kwenye milima na kilimo karibu na njia ya reli. Kutokana na shughuli hizi, mvua kubwa zinaponyesha mchanga mwingi na magogo husombwa kuelekea kwenye tuta la reli na kusababisha makalvati na madaraja kuziba na maji kupita juu ya njia ya reli na hivyo kuharibu miundombinu iliyopo. Kufuatia uharibifu huo na kwa vipindi tofauti, kazi za kuimarisha tuta la reli, kujenga makalvati na madaraja yaliyosombwa na kuimarisha makalvati na madaraja yaliyobaki imekuwa ikiendelea kufanyika. Naomba kuchukua fursa hii kuwaomba wananchi walio karibu na njia ya reli kuzingatia sheria ya reli kwa kutofanya shughuli katika eneo la hifadhi ya reli (railway reserve) ambayo ni mita 15 kutoka kwenye njia ya reli sehemu za miji na mita 30 nje ya miji.
Mheshimiwa Spika, katika juhudi za kutafuta ufumbuzi wa kudumu wa kuharibiwa kwa reli katika maeneo ya Kilosa hadi Gulwe, RAHCO imesaini mkataba na mshauri mwelekezi (CPCS Transcom-Canada) kwa ajili ya kufanya utafiti wa namna ya kuboresha njia ya reli na kuongeza ufanisi wa reli (Tanzania Railway Upgrading and Performance Improvement Study). Kazi hii inafadhiliwa na Benki ya Dunia. Moja ya hadidu za rejea katika mkataba huu ni kutoa ushauri unaoelekeza namna ya kupata suluhu ya kudumu kumaliza tatizo la uharibifu wa miundombinu ya reli linalotokana na mafuriko katika sehemu kati ya Kilosa na Gulwe. Aidha, RAHCO inaangalia uwezekano wa kufufua mabwawa ya kupunguza kasi ya maji maarufu kwa jina la Punguza kwa kushirikiana na Halmashauri husika.
Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2011/2012 RAHCO imesaini mkataba na mkandarasi kwa ajili ya kutandika mataruma na reli nzito (ratili 80 kwa yadi sawa na kilo 40 kwa mita) kutoka stesheni ya Kitaraka hadi stesheni ya Malongwe umbali wa km 89. Eneo hili lilikuwa na reli nyepesi (ratili 56.2 kwa yadi sawa na kilo 28 kwa mita) na ambazo zimechakaa sana na hivyo husababisha ajali mara kwa mara. Kazi hii itaanza mwezi Septemba 2012 na kumalizika mwezi Septemba 2013 kwa gharama ya shilingi bilioni 29.2. Reli na mataruma yatakayotandikwa yalinunuliwa kwa fedha kutoka Benki ya Dunia kiasi cha Dola za Marekani milioni 30.6 na shilingi bilioni 10.9 kutoka Serikali ya Tanzania.
Mheshimiwa Spika, katika kipindi cha 2011/2012, RAHCO ilikamilisha ujenzi wa kituo cha kuhifadhia makasha (Inland Container Depot) cha Shinyanga kwa gharama ya shilingi bilioni 3.36 chenye uwezo wa kuhifadhi makasha 500 ya futi 20 au makasha 200 ya futi 40. Kituo hiki kimejengwa kurahisisha kupakia au kupakua makasha kutoka kwenye malori kwenda au kutoka kwenye mabehewa (intermodal handling) na kuhifadhi makasha yanayoshushwa kutoka kwenye mabehewa. Aidha, RAHCO imesaini mkataba na mkandarasi wa kujenga kituo cha kuhifadhi makasha mjini Mwanza chenye uwezo sawa na kituo cha Shinyanga kwa kusudio hilo hilo. Mkandarasi alikabidhiwa eneo la kazi tarehe 25 Aprili 2012 na ujenzi unatarajiwa kukamilika mwezi Aprili 2013 kwa gharama ya shilingi bilioni 3.1. Serikali ya Ubelgiji imefadhili mitambo mitano ya kushusha, kupanga na kupakia makasha kwa ajili ya vituo vya Ilala, Shinyanga na Mwanza. Mitambo hiyo iliyogharimu Euro 1,660,500 ilikabidhiwa kwa RAHCO tarehe 29 Septemba 2011.
Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2011/2012 RAHCO iliendelea na juhudi za kuimarisha njia ya reli kati ya Kaliua hadi Mpanda. Reli chakavu na zenye uzito mdogo wa ratili 45 kwa yadi (sawa na kilo 22 kwa mita) zilipangwa kubadilishwa kutoka km 144.0 hadi km 149.0 kati ya Mto Ugala na Katumba na kutoka km 80.7 hadi km 84.9 kati ya Lumbe na Mto Ugala. Hadi mwezi Mei 2012 kilometa 5.5 zilikuwa zimebadilishwa. Tuta la reli kutoka km 24.0 hadi km 29.0 kati ya Kaliua na Ugala River, lilipanuliwa kutoka mita 1.5 hadi mita 2.5.
Mheshimiwa Spika, ili kuongeza uwezo wa reli ya Kati kutoa huduma kwa kiwango cha kimataifa, Serikali kwa kushirikiana na serikali za Rwanda na Burundi zimemwajiri mshauri mwelekezi (CANARAIL Consultants Inc.) kwa ajili ya kufanya upembuzi wa kina (detailed engineering study) wa mradi wa uendelezaji na ujenzi wa reli kutoka Dar Es Salaam–Isaka-Keza (km 1,287), Keza-Kigali (km 186) na Keza-Musongati (km 197) kwa kiwango cha Kimataifa (standard gauge-1435mm). Kazi hiyo ilianza tarehe 17 Februari 2012 na inatarajiwa kukamilika Februari 2013.
Mheshimiwa Spika, Serikali ya Uganda imeonyesha nia ya kutumia bandari ya Tanga kupitishia mizigo yake inayoingia au kutoka nje. Ili kutimiza azma hiyo, Serikali za Tanzania na Uganda zimekubaliana kujenga njia ya reli kutoka Arusha hadi Musoma, kuboresha bandari ya Musoma (au ijengwe mpya) na kuboresha reli ya Tanga hadi Arusha kwa kiwango cha kimataifa, kujenga bandari mpya iitwayo Kampala eneo la Bukasa (Kampala). Reli hii inatarajiwa ijengwe kwa kiwango cha Kimataifa. Mshauri mwelekezi ambaye atafanya usanifu wa awali wa ujenzi wa reli hiyo ya Arusha hadi Musoma amepatikana kwa gharama ya shilingi bilioni 5.7 na kazi hiyo inatarajiwa kuanza mwezi huu Agosti 2012 na kukamilika baada ya miezi tisa. Kwa reli itokayo Tanga kwenda Arusha, amepatikana mshauri mwelekezi ambaye atafanya usanifu wa kina (detailed engineering design) wa kujenga reli hiyo kuanzia bandari mpya ya Mwambani Tanga hadi Arusha kwa gharama ya shilingi bilioni 5.02. Kazi hii inatarajiwa kuanza Agosti 2012 na kukamilika baada ya miezi tisa. 
Mheshimiwa Spika, Wizara kupitia RAHCO iliwasiliana na Manispaa ya Tanga na kutengewa ekari 150 katika eneo la Mwambani kwa ajili ya kujenga sehemu ya kupanga mabehewa (marshalling yard). RAHCO ilimweka mshauri mwelekezi kwa ajili ya kufanya tathmini ya fidia kwa wananchi wa maeneo hayo. Mshauri mwelekezi ameshakabidhi ripoti na jumla ya shilingi bilioni 5.5 zitahitajika kulipa fidia. Fidia hiyo itaanza kulipwa mwezi Septemba 2012.
Mheshimiwa Spika, kwa kuwa hapo baadaye kuna mpango wa kujenga reli ya Dar es Salaam hadi Kigali (Rwanda) na Musongati (Burundi) kupitia Isaka kwa kiwango cha kimataifa (standard gauge-1435mm) na mshauri mwelekezi ameanza kazi ya kufanya upembuzi (detailed engineering study) kwa reli hiyo, kuna nia pia ya kujenga reli ya Tabora hadi Kigoma, Kaliua hadi Mpanda na Isaka hadi Mwanza kwa kiwango hicho. RAHCO imepata mtaalam mwelekezi atakayefanya usanifu wa kina wa reli ya Tabora-Kigoma na Kaliua – Mpanda. Kazi hii inatarajiwa kuanza Agosti 2012 na kukamilika baada ya miezi tisa kwa gharama ya shilingi bilioni 5.5. Aidha, RAHCO imepata mtaalam atakayefanya usanifu wa kina wa reli ya Isaka hadi Mwanza. Kazi hii inatarajiwa kuanza Agosti 2012 na kukamilika baada ya miezi tisa kwa gharama ya shilingi bilioni 4.53
Mheshimiwa Spika, Mamlaka ya Reli ya Tanzania na Zambia (TAZARA) iliendelea kutoa huduma za uchukuzi lakini kwa kiwango kisichoridhisha kutokana na uchakavu wa miundombinu, injini, mabehewa na mitambo mbalimbali. Aidha, TAZARA imekuwa na matatizo makubwa ya uongozi yanayotokana na sheria iliyoianzisha na muundo wa Mamlaka, masuala ambayo Baraza la Mawaziri la TAZARA limeshaazimia kuunda Tume ya pamoja ya kupitia upya masuala haya. 

Wakati TAZARA ina uwezo wa kusafirisha tani milioni 5 kwa mwaka, uwezo wake umeshuka sana kutoka tani milioni 1.2 mwaka 1992/1993 hadi tani 339,094 mwaka 2011/2012. Aidha, TAZARA ambayo inaweza kusafirisha abiria milioni 3 kwa mwaka, imeweza kusafirisha abiria 793,231 kwa mwaka 2011/2012. 
Mheshimiwa Spika, mwaka 2011/2012 Bunge lako tukufu liliarifiwa kuwa TAZARA kupitia Itifaki ya 14 imepewa mkopo usiokuwa na riba wa shilingi bilioni 59.85 kutoka Serikali ya Jamhuri ya Watu wa China. Mkopo huo ulitumika katika kutekeleza kazi zilizokusudiwa ikiwa ni pamoja na ununuzi wa vichwa vipya sita vya treni vinavyotarajiwa kupokelewa mwezi Agosti, 2012; Mabehewa mapya 90 ya mizigo yamepokelewa na tayari yanafanyakazi; kuagiza vipuri vya kukarabati vichwa sita kutoka kampuni ya GE – USA na vipuri tayari vimeanza kuwasili; Ukarabati wa vichwa vitatu vya sogeza CK6 unaendelea na utakamilishwa mwezi Novemba, 2012; na Vipuri kwa ajili ya ukarabati wa mashine nne za kunyanyua mizigo tayari vimewasili na inatarajiwa kuwa kazi ya ukarabati itakamilika Februari 2013
Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2012/2013 Serikali za Tanzania na Zambia zitaendelea kuchukua hatua za kutatua matatizo ya kifedha na uendeshaji wa TAZARA. Katika kutimiza azma hii, tarehe 26 Machi 2012, Serikali za Tanzania, Zambia na China zilitia saini Itifaki ya 15 kwa ajili ya kuipatia TAZARA mkopo usiokuwa na riba wa shilingi bilioni 67.2. Mkopo huo utatumika kuimarisha TAZARA kwa kugharamia miradi mbalimbali ikiwamo ununuzi wa malighafi ya utengenezaji wa mataruma ya reli kwa zege, ununuzi wa injini za njia kuu, ukarabati mkubwa wa mabehewa ya abiria, ununuzi wa kreni za mizigo na za okoa, ununuzi wa mataruma ya mbao, vipuri vya mitambo ya kiwanda cha mataruma na kokoto, vipuri vya reli na kugharamia mafunzo kwa wafanyakazi wa kada mbalimbali hasa ufundi na utawala. Kupitia Itifaki ya 15, Serikali ya Jamhuri ya Watu wa China imetoa msaada kwa ajili ya kufanya upembuzi yakinifu ili kubaini maeneo ya kuikarabati reli ya TAZARA, pamoja na usanifu wa reli ya Mlimba – Liganga na Kiwira – Uyole kwenye madini ya chuma na makaa ya mawe. Msaada huo wa Serikali ya Jamhuri ya Watu wa China unaweka msingi imara wa mabadiliko katika utendaji kazi wa Mamlaka.

Huduma za usafiri wa Reli Jijini Dar es Salaam
Mheshimiwa Spika, kutokana na tatizo la msongamano wa magari jijini Dar es Saalaam, Wizara yangu katika kipindi cha muda mfupi inakusudia kuanza kutoa huduma za usafiri wa abiria kwa njia ya reli kwa lengo la kupunguza msongamano barabarani. Katika mwaka 2011/2012 Wizara kupitia RAHCO, TRL na TAZARA ilifanya tathmini ya gharama za kuanzisha huduma za reli. Kwa kuanzia huduma hii itatolewa kutoka stesheni ya reli Dar es Salaam hadi Ubungo Maziwa (Km 12) na kutoka Mwakanga hadi Kurasini kupitia stesheni ya Dar es Salaam (Km 34.5).
Mheshimiwa Spika, kwa njia ya reli kati ya stesheni ya Dar es Salaam hadi Ubungo, kiasi cha shilingi bilioni 4.75 zitatumika kwa ajili ya ukarabati wa njia, injini tatu (3) za treni na mabehewa kumi na nne (14) ya abiria. Fedha hizi zimepatikana na kazi ya ukarabati wa njia ya reli, injini na mabehewa imeanza na inatarajiwa kukamilika Oktoba 2012. RAHCO inaendelea na kazi za kukarabati njia na tayari mataruma mabovu zaidi ya 1,500 yamekwishabadilishwa na kazi ya kuweka sawa mataruma ili yakae pembe mraba na reli (squaring) imekwishafanywa kwa umbali wa km 10.5. Aidha, kazi za ujenzi na uimarishaji wa tuta lililoharibika na kufukua mifereji ya kupitisha maji taka zinaendelea. Mradi huu unakabiliwa na changamoto mbalimbali, kubwa zaidi ikiwa ni uvamizi wa maeneo ya hifadhi ya njia ya reli uliofanywa na wananchi baada ya njia kukaa bila kutumika kwa muda mrefu, ufinyu wa eneo la kugeuzia vichwa vya treni sehemu ya Ubungo Maziwa na ukosefu wa maeneo ya kuegesha magari katika vituo. RAHCO inaendelea kushirikiana na Halmashauri za Jiji la Dar es Salaam ili kupata ufumbuzi wa changamoto hizi kwa mujibu wa sheria na taratibu zilizowekwa. Huduma hii itaanza kwa kuwa na treni mbili ambazo zitatoa huduma asubuhi na jioni kuanzia Jumatatu hadi Jumamosi. Treni moja itaanzia stesheni ya Dar es Salaam na nyingine Ubungo Maziwa na kupishana maeneo ya Buguruni kwa Mnyamani. Treni hizi zitasimama kwenye vituo sita (6) vifuatavyo: Stesheni ya Dar es Salaam, Kamata, Buguruni kwa Mnyamani, Tabata Matumbi, Mabibo na Ubungo Maziwa. Kila treni itakuwa na mabehewa sita yenye uwezo wa kubeba abiria waliokaa na wale waliosimama takriban 1,000 kila safari.
Mheshimiwa Spika, mpango huu utawezesha kuwa na jumla ya safari nane (8) za treni asubuhi na nane (8) jioni hususan wakati wa mahitaji makubwa ya huduma (peak hours). Muda wa safari kati ya stesheni ya Dar es Salaam na Ubungo Maziwa unakadiriwa kuwa dakika 35. Kwa utaratibu huu inakisiwa kwamba treni hizi mbili zitaweza kusafirisha watu takriban 16,000 kwa siku. Napenda kuchukua fursa hii kutoa wito kwa wafanyabiashara hapa nchini kuwekeza kwenye mradi wa maegesho ya magari eneo la Ubungo. Kwa kuanzia, Chuo cha Taifa cha Usafirishaji kimetenga eneo la ekari 4 (kati ya ekari 45 inazomiliki) kwa ajili ya maegesho ya magari. Hii itawawezesha watu wenye magari wanaotokea maeneo ya Kibaha, Kiluvya, Mbezi, na Kimara kuelekea mjini waweze kuegesha magari yao Ubungo na kupanda treni kwenda Stesheni ya Dar es Salaam.. 
Mheshimiwa Spika, kwa upande wa reli ya TAZARA jumla ya shilingi milioni 838 zinahitajika kwa ajili ya ukarabati wa injini tatu (3) za treni na mabehewa kumi na nne (14). Hivi sasa, kazi za ukarabati wa injini na mabehewa zinaendelea. Kazi hizi zinatarajiwa kukamilika ifikapo Oktoba, 2012. Huduma hii ya treni inatarajiwa kutolewa kati ya vituo vya Dar es Salaam, Kwa fundi umeme, Yombo, Kwa Limboa, Lumo Kigilagila, Barabara ya Kitunda, Kipunguni B, Moshi Bar, Majohe, Shule ya Sekondari Magnus, Mwakanga, Chimwaga, Maputo, Mtoni relini, Kwa Azizi Ali relini hadi Kurasini. Kuanza kwa usafiri huu kutachangia kupunguza msongamano wa magari jijini Dar es Salaam na kuwezesha watu kufika katikati ya jiji haraka zaidi.

Udhibiti wa Huduma za Usafiri wa Nchi kavu na Majini
Mheshimiwa Spika, SUMATRA imeendelea kuchukua hatua za kusogeza huduma zake karibu zaidi na wateja kwa kuwapunguzia muda wa kusafiri kwenda kufuata huduma kwa kufungua ofisi zake katika mikoa mbalimbali. Hadi sasa, Mamlaka ina ofisi katika mikoa kumi na tano (15) na inaendelea kutoa huduma katika mikoa sita (6) kwa kupitia ofisi za Katibu Tawala wa Mikoana inatarajia kufungua ofisi katika mikoa ya Singida, Shinyanga na Ruvuma mwezi huu wa Agosti 2012.

Udhibiti wa Huduma za Usafiri wa Reli
Mheshimiwa Spika, katika kipindi cha Julai 2011 hadi Juni 2012, SUMATRA ilifanya ukaguzi wa miundombinu ya reli kutoka Dar-es-Salaam hadi Kigoma, Kaliua hadi Mpanda na Tabora hadi Mwanza. Kufuatia ukaguzi huo Mamlaka ilitoa maelekezo kwa TRL na RAHCO kurekebisha upungufu yaliyobainika ikiwa ni pamoja na kufanya matengenezo ya njia, kuyafanyia marekebisho mabehewa 9 yaliyobainika kuwa na kasoro kubwa na kutekeleza mpango wa usalama.

Udhibiti wa Huduma za Usafiri kwa Njia ya Barabara
Mheshimiwa Spika, katika kipindi cha mwaka 2011/2012 SUMATRA iliendelea kufuatilia masharti ya leseni za usafiri kwa magari ya abiria na mizigo kwa kufanya kaguzi. SUMATRA ilifanya kaguzi 426 ambapo magari 1,765 yalikamatwa kwa makosa mbalimbali yakijumuisha kuzidisha nauli, kutofuata ratiba na kutokuwa na madereva wawili kwa baadhi ya mabasi ya masafa marefu. Mamlaka ilichukua hatua kadhaa ikiwa ni pamoja na kusimamisha leseni za mabasi za makampuni 23. Aidha, SUMATRA ilikagua ubora wa huduma zinazotolewa kwa mabasi katika njia kuu za masafa marefu nchini na yaendayo nje ya nchi. SUMATRA imetoa maelekezo mbalimbali kwa wahusika kufanya marekebisho katika maeneo yenye upungufu ili kuinua viwango vya ubora wa huduma. 
Mheshimiwa Spika, ajali za barabarani zimeendelea kuwa tatizo kubwa hapa nchini pamoja na jitihada mbalimbali za kupunguza tatizo hili. Ajali hizi zimesababisha madhara makubwa ikiwa pamoja na vifo, ulemavu na upotevu wa mali. Aidha, ajali zimekuwa zikiigharimu Serikali fedha nyingi kwa kugharamia matibabu ya waathirika. 

Katika ajali 23,986 zilizotokea mwaka 2011 mabasi 3,698 yalihusika ikilinganishwa na jumla ya ajali 24,665 zilizotokea mwaka 2010 na kuhusisha mabasi 4,102. Katika kipindi hicho idadi ya mabasi yaliyohusika katika ajali ilipungua kwa asilimia kumi (10%) sawa na mabasi 404. Aidha, vifo vilivyotokana na ajali za mabasi kwa mwaka 2011 vilitokea vifo 700 ikilinganishwa na vifo 640 vilivyotokea mwaka 2010 sawa na ongezeko la aslimia 9.37.
Mheshimiwa Spika, usafiri wa kutumia pikipiki umekuwa na maanufaa makubwa kwenye maeneo ambayo vyombo vingi vya usafiri haviwezi kufika au hufika kwa shida. Aidha, usafiri kwa njia ya pikipiki umeongeza ajira kwa wananchi na hasa vijana. Hata hivyo, vyombo hivi vimekuwa na rekodi mbaya ya usalama kwa kuhusika na ajali na uhalifu. Katika kipindi cha mwaka 2011 kulikuwa na ajali 5,384 za pikipiki  ikilinganishwa na ajali 4,363 zilizotokea mwaka 2010 sawa na ongezeko la 23%, vifo 945 vilivyotokea mwaka 2011 ikilinganishwa na vifo 683 vilivyotokea mwaka 2010 sawa na ongezeko la 38%, na majeruhi 5,506 katika mwaka 2011 ikilinganishwa na majeruhi 4,471 mwaka 2010 sawa na ongezeko la 23%.
Mheshimiwa Spika, katika kupambana na tatizo la ajali za waendesha pikipiki na abiria SUMATRA imekuwa ikishirikiana na Jeshi la Polisi ili kuhakikisha kuwa waendesha pikipiki wamepata mafunzo na leseni za udereva, pikipiki zinakuwa na bima, waendeshaji na abiria wanavaa kofia za kinga, na pikipiki hazipakii zaidi ya abiria mmoja. Aidha, SUMATRA kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi na Halmashauri zote itaendelea kutoa elimu kwa waendesha pikipiki na kusimamia utekelezaji wa masharti ya leseni za usafirishaji kwa lengo la kupunguza ajali. 
Mheshimiwa Spika, katika kukabiliana na tatizo la ajali za magari barabarani, SUMATRA imeendelea kuhakikisha kwamba wenye mabasi na magari ya mizigo wanakuwa na nyaraka muhimu ikiwa ni pamoja na hati ya ukaguzi wa gari (vehicle inspection report) kutoka Jeshi la Polisi na Hati ya Bima kabla ya kupewa leseni. Aidha, SUMATRA imeendelea kusimamia masharti ya leseni ikiwa ni pamoja na madereva kufuata muda uliopangwa kwenye ratiba. Katika kipindi cha Julai, 2011 hadi Juni, 2012 Mamlaka ilisimamisha leseni 102 za mabasi  yanayomilikiwa na makampuni 20 kutokana na kukiuka masharti ya Leseni na hasa kuhusika na ajali. Mamlaka itaendelea kuchukua hatua kali kwa wote wanaotoa huduma za usafiri wenye kuvunja sheria na kanuni zilizopo. Aidha, kampeni ya uhamasishaji na elimu kwa umma iliyoanzishwa na Mamlaka mwaka 2010 kwa kukutana na Makamanda wote wa usalama barabarani wa mikoa kila mwaka, kuendesha vipindi vya redio mara moja kwa wiki, kutoa makala kwenye magazeti, kutoa vipeperushi na kukutana na wadau, itapewa umuhimu zaidi katika mwaka huu wa fedha kwa kuanzisha vipindi vya majadiliano na wadau katika redio na luninga na kuandaa midahalo kuhusu muswada muhimu wa sheria ya utafutaji na uokoaji kwa ajali za anga na majini.

USAFIRI NA UCHUKUZI MAJINI
Huduma za Uchukuzi katika Maziwa
Mheshimiwa Spika, Kampuni ya Huduma za Meli (MSCL) ilianzishwa chini ya sheria ya Makampuni Sura 212 mnamo tarehe 08/12/1997. Kampuni hii ilianzishwa kutokana na kilichokuwa kitengo cha Shirika la Reli Tanzania (TRC Marine Division). Kutokana na kukosekana kwa mtaji stahiki wa kuendesha shirika hili, ufanisi wake umekuwa wa matatizo.
Mheshimiwa Spika, kwa kuzingatia umuhimu wa huduma za usafiri wa meli katika maziwa, katika mwaka 2010/2011 Serikali iliwasiliana na Washirika wa Maendeleo kuisaidia MSCL kukarabati vyombo vyake vya usafiri vilivyopo katika maziwa. Tayari Serikali ya Denmark imekubali kufadhili mradi wa ujenzi wa meli tatu katika maziwa ya Victoria, Tanganyika na Nyasa kwa meli moja kila ziwa. Upembuzi yakinifu wa mradi huo ulifanywa na Kampuni ya OSK-Ship Tech A/S kuanzia tarehe 24 Machi, 2011 na kukamilika Novemba, 2011. Kwa sasa Serikali ya Denmark inafanyia kazi upembuzi huo na mradi huu unatarajiwa kuanza mwaka 2013. Mradi huu unahusisha pia ukarabati wa meli za MV. Victoria, MV. Umoja na MV. Serengeti. Aidha, Serikali ya Ujerumani imekubali kukarabati meli ya MV. Liemba.
Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2011/2012 Serikali iligharamia bima za meli na matengenezo makubwa ya meli ya MV.Songea. Matengenezo haya yamefanyika nchini Malawi na yamekamilika tarehe 25/07/2012. Meli hiyo kwa sasa iko kwenye majaribio. Aidha, meli ya MV.Clarias iliyokuwa imesimama kutokana na ubovu ilifanyiwa matengenezo na kuanza kutoa huduma tangu tarehe 4/6/2012.
Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2011, Kampuni ya Huduma za Meli ilisafirisha jumla ya tani 62,110 ikilinganishwa na malengo ya mwaka ya kusafirisha tani 111,805. Hii ni pungufu ya tani 49,695 sawa na asilimia 44. Aidha, abiria 290,208 walisafirishwa katika kipindi cha mwaka 2011 ikilinganishwa na lengo la kusafirisha abiria 408,464. Utendaji halisi ukilinganishwa na malengo, kuna upungufu wa abiria 118,256 sawa na asilimia 29. Utendaji huu pia ni pungufu ya abiria 35,387 sawa na asilimia 11 ikilinganishwa na abiria 325,595 waliosafirishwa mwaka 2010. Katika kipindi cha Januari hadi Machi, 2012 Kampuni imeweza kusafirisha jumla ya abiria 46,206 na jumla ya tani za mzigo 18,527. Aidha, katika kipindi cha mwaka 2012/2013, Kampuni ya Huduma za Meli imepanga kusafirisha jumla ya abiria 355,736 na jumla ya tani za mizigo 150,000. 
Huduma za Uchukuzi Baharini
Mheshimiwa Spika, huduma za usafiri wa masafa marefu baharini inatolewa na Kampuni ya SINOTASHIP ambayo inamilikiwa kwa pamoja na Serikali za Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Jamhuri ya Watu wa China kwa asilimia 50 kila mmoja. Kampuni hii ilianzishwa mwaka 1967. Katika mwaka 2011 kampuni ilitumia meli yake moja ya masafa marefu baharini yenye uwezo wa kubeba tani 57,000 kwa wakati mmoja kwa kufanya safari 8 badala ya 6 zilizopangwa na kusafirisha jumla ya tani 405,000. Katika mwaka 2012, kampuni ya SINOTASHIP inatarajia kusafirisha  jumla ya tani 450,000 za shehena. 
Mheshimiwa Spika, katika kipindi cha mwaka 2011/2012, Kampuni ya SINOTASHIP iliendelea kukabiliana na changamoto mbalimbali ikiwa ni pamoja na uharamia katika bahari ya Hindi, Pwani ya Afrika Mashariki na Somalia na kuyumba kwa uchumi wa dunia. Katika kupambana na changamoto hizi kwa mwaka 2012/2013, Kampuni itaendelea kutafuta na kuhudumia shehena zinazosafirishwa kwa tozo kubwa ili kuongeza mapato yake. Aidha, SINOTASHIP itaangalia uwezekano wa kutoa huduma za usafiri katika maziwa kwa kuanza na Ziwa Victoria. Utafiti wa kuangalia uwezekano huo ulianza mwezi Juni 2012 na unatarajiwa kukamilika ifikapo Septemba 2012. 

Huduma za Bandari

Mheshimiwa Spika, bandari ni moja ya miundombinu muhimu sana katika nchi na kichocheo cha ukuaji wa biashara, uchumi na ustawi wa taifa.  Takwimu zinaonyesha kuwa asilimia 85 ya biashara yote duniani inapitia na kusafirishwa kwa kutumia bandari. Serikali kupitia Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari imejizatiti kuendelea kuimarisha Bandari zetu ili ziweze kutoa huduma bora zaidi.
Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2011/2012, Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari ililenga kuhudumia tani milioni 12.000 na makasha  510,300. Katika kipindi hicho jumla ya tani milioni 12.084 zilihudumiwa, ikilinganishwa na tani milioni 11.157 zilizohudumiwa mwaka 2010/2011, ongezeko la tani 927,000 sawa na asilimia 8.3. Aidha, jumla ya makasha 530,089 yalihudumiwa ikilinganishwa na makasha 467,749 yaliyohudumiwa mwaka 2010/2011, ongezeko la makasha 62,340 sawa na asilimia 13.3.  Kitengo cha TICTS kilihudumia makasha 355,105 na Mamlaka ikahudumia makasha  174,984, sawa na asilimia 33 ya makasha yote..  
Mheshimiwa Spika, katika kipindi cha 2011/2012 jumla ya tani milioni 3.275 kwenda na kutoka nchi jirani zilihudumiwa katika bandari ya Dar es Salaam ambayo ni ongezeko la tani 106,000, ikilinganishwa na tani milioni 3.169 zilizohudumiwa mwaka 2010/2011. Shehena hii imekuwa ikiongezeka kwa kasi ndogo licha ya jitihada za TPA kwa kushirikiana na wadau wengine kuvutia wateja toka nchi jirani kutumia bandari zetu. Jitihada hizi zinakabiliwa na utendaji hafifu wa miundombinu ya usafirishaji. Kwa mfano, kati ya mwaka 2001 na 2011, mgao (market share) wa Bandari ya Dar es Salaam kwa shehena ya Uganda umepungua kutoka asilimia 6 hadi asilimia 1 kutokana na utendaji hafifu wa reli. Kutokana na changamoto hii, Wizara imeunda vikosi kazi viwili; kikosi cha kwanza kuangalia uwezekano wa kuunganisha huduma za Bandari na Reli na cha pili kuangalia maeneo ya ushirikiano kati ya Bandari, Reli na wadau wengine (kwa mfano TRA) ili kuharakisha uondoshaji wa mizigo bandarini. Taarifa za vikosi kazi hivyo zitatolewa hivi karibuni.
Mheshimiwa Spika, hata hivyo Bandari zetu zinaendelea kukabiliwa na changamoto mbalimbali hususan ukuaji mkubwa wa shehena kama vile makasha kwa asilimia 18.9, magari kwa asilimia 13.1, mafuta kwa asilimia 12.6, kichele kwa asilimia 9.6 na shehena ya “break Bulk”  kwa asilimia 6 kwa mwaka
Mheshimiwa Spika, katika kukabiliana na changamoto hizo, Serikali kupitia TPA inatekeleza Mpango Kabambe (Port Master Plan) ambao umeainisha dira ya maendeleo. Baadhi ya miradi mikuu ambayo imeainishwa na Mpango huo na utekelezaji wake umeanza katika bandari ya Dar es Salaam ni pamoja na ujenzi wa gati 13 na 14 unaoenda sambamba na kupanua na kuongeza kina cha lango la kuingilia meli, kuimarisha na kuongeza kina cha gati namba 1 hadi 7, kujenga kituo kikubwa cha kuhifadhia mizigo eneo la Kisarawe (Cargo Freight Centre - CFC), ujenzi wa boya la mafuta (SPM) na kuimarisha kitengo cha sasa cha KOJ.
Mheshimiwa Spika, maandalizi ya utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa gati namba 13 na 14 yanaendelea kwa kuzingatia maelekezo ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania yaliyotolewa katika mkutano wake wa saba. Zoezi la uhakiki wa gharama za mradi linaendelea vizuri na tayari taarifa ya awali imewasilishwa. Matarajio ya kupata mkopo kutoka benki ya EXIM ya China kwa mradi huo ni mazuri. 
Mheshimiwa Spika, utekelezaji wa mradi wa kuimarisha Gati Na. 1-7 katika bandari ya Dar es Salaam upo katika hatua ya usanifu wa kina na umelenga kufanya yafuatayo:
Kuongeza kina cha magati namba 1 hadi 7 kutoka kati ya mita 5 hadi 9 kufikia mita  14;
Ujenzi wa gati maalumu la kuhudumia meli za magari (Roll on Roll off berth);
Kuongeza uwezo wa kuhudumia shehena ya nafaka kwa kujenga mfumo wa kupakua shehena hiyo kwa kutumia teknolojia ya mikanda (conveyer belt). 
Mhandisi Mshauri M/S INROS LACKNER AG ya Ujerumani ameajiriwa kufanya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina. Kazi hii ilianza tarehe 22 Juni 2012 na inatarajiwa kukamilika Desemba 2012 ambapo mchakato wa utekelezaji utaanza.
Mheshimiwa Spika, kuhusu kuongeza eneo la kuhifadhi mizigo, Serikali kupitia TPA ina mpango wa kujenga kituo kikubwa cha kuhifadhia mizigo nje ya Jiji la Dar es salaam kitakachokuwa kinapokea mizigo ya Zambia, Malawi, DR Congo, Burundi na Rwanda. Upembuzi yakinifu wa awali umekamilika na unapendekeza kituo hiki kujengwa maeneo ya Kisarawe, kilomita 40 kutoka katikati ya Jiji la Dar es Salaam. Kituo hicho kitasaidia kupunguza msongamano wa mizigo bandarini na malori katika barabara za Jiji. Taratibu za kumpata Mtaalamu Mshauri wa kufanya Upembuzi yakinifu zinaendelea kwa ufadhili wa Benki ya Dunia. 
Mheshimiwa Spika, Miradi iliyoainishwa kwa ajili ya kuongeza uwezo wa bandari kuhudumia shehena ya mafuta ni pamoja na Ujenzi wa Boya la Mafuta (SPM) na kuimarisha kitengo cha sasa cha KOJ. Boya la sasa SPM linabadilishwa na kuweka boya kubwa ambalo litakuwa na uwezo wa kupakua mafuta mchanganyiko. Uwezo wa boya jipya ni kuhudumia meli za mafuta zenye tani 150,000 kwa wakati mmoja ikiwa ni mara tatu ya uwezo wa sasa wa KOJ ambao ni tani 45,000 tu. Awamu ya kwanza ya ujenzi ilianza mwaka 2011 na inahusu ubadilishaji wa boya na mabomba ambayo inatarajiwa kukamilika mwezi huu wa Agosti 2012. Awamu ya pili inahusu ujenzi wa matanki ya kuhifadhi mafuta kwa muda kabla ya kusambazwa (custody transfer). Kazi hii imepangwa kukamilika katika mwaka wa fedha 2012/2013. Mradi huu utagharimu kiasi cha dola za kimarekani milioni 69 kati ya hizo Dola za Kimarekani milioni 60 ni fedha za mkopo toka benki ya CRDB. Aidha, kukamilika kwa mradi huu, kutafanikisha lengo la Serikali la kuagiza mafuta kwa wingi (bulk procurement) ili kupunguza gharama za usafirishaji na hatimaye gharama kwa mtumiaji.
Mheshimiwa Spika, katika kipindi cha miaka 5 iliyopita, shughuli za utafutaji wa mafuta na gesi katika kina kirefu cha Bahari ya Hindi Ukanda wa Mtwara zimevutia makampuni mengi kutaka kuwekeza katika eneo hili na kutaka kutumia bandari ya Mtwara kama kituo maalum (supply base). Hivi sasa kampuni za Ophir (Uingereza), BG (Uingereza), Statoil (Norway) na Petrobras (Brazil) zimeweka “supply base” katika bandari ya Mtwara. Wizara kupitia TPA kwa kutambua fursa hii, imekodisha eneo lenye ukubwa wa mita za mraba 104,558 kwa kampuni ya BG kwa mkataba wa miaka mitano kuanzia mwaka 2011.   
Mheshimiwa Spika, mpango uliopo hivi sasa ni kuanzisha ukanda huru ndani ya bandari ya Mtwara (Mtwara Free Port Zone), eneo ambalo litatumiwa na Kampuni zinazotoa huduma kwa kampuni za uchimbaji mafuta na gesi. Eneo la hekta 110 limetengwa kwa ajili ya ujenzi wa ukanda huru. Eneo la Ukanda huru limepangwa kuendelezwa kwa awamu. Awamu ya kwanza itahusu ujenzi wa miundombinu (Basic Infrastructure) katika eneo la hekta 10 kwa ajili ya Makampuni ya utafiti wa mafuta na gesi. Kamati imeundwa inayojumuisha wataalamu kutoka EPZA, TPDC, TBA, Wizara ya Uchukuzi, Kampuni za utoaji huduma za uchimbaji na TPA. Kamati hiyo imekamilisha michoro ya eneo la awamu ya kwanza na hatua ya kumpata Mkandarasi wa kujenga itakamilika mwezi Oktoba 2012.  
Mheshimiwa Spika, TPA iliajiri Mshauri Mwelekezi kufanya Upembuzi Yakinifu wa upanuzi wa Bandari ya Mtwara. Mshauri huyo amependekeza mpango wa matumizi ya eneo jipya la Msanga Mkuu lenye ukubwa wa hekta 2623 na aliwasilisha rasimu ya taarifa ya mwisho tarehe 14 Juni 2012 ambayo ilijadiliwa na kukubaliwa na wadau huko Mtwara. Hatua inayofuata ni kuandaa michoro kwa ajili ya ujenzi wa gati mpya nne kwa wakati mmoja. Ujenzi umepangwa kuanza katika kipindi cha mwaka wa fedha 2012/2013.
Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia  TPA imetekeleza na inatekeleza miradi ya kuboresha bandari za maziwa na bandari ndogo ndogo kama ifuatavyo:
Kuondoa mchanga katika gati ya bandari ya Kigoma kwa kutumia “Dredger” iliyonunuliwa na TPA. Matengenezo ya Chelezo kwa ajili ya ukarabati wa meli yalikamilika mwezi Septemba 2011;
Ujenzi wa maghala mawili na ukarabati wa barabara inayoingia bandari ya Kasanga uliokamilika mwezi Septemba, 2011;
Ujenzi wa ghala la mizigo na uzio katika bandari ndogo ya Kiwira katika Ziwa Nyasa uliokamilika Juni 2012;
Ujenzi wa yadi ya kuhifadhia makasha na barabara ya kuingia Bandari ya Bukoba uliokamilika mwezi Agosti 2011;
Kazi ya ujenzi wa yadi ya kuhifadhia makasha katika bandari ya Tanga iliyokamilika mwezi Desemba 2011.

Miradi mingine inayoendelea kutekelezwa ni kama ifuatavyo:

Ujenzi wa magati manne madogo katika Ziwa Tanganyika katika maeneo ya Kipiri, Lagosa, Sibwesa, na Karema, unaendelea. Ujenzi wa gati la Kipiri utakaokamilika Septemba 2012, ujenzi wa gati la Karema utakaokamilika Disemba 2012, ujenzi wa gati la Sibwesa na Lagosa utakamilika   Februari  2013;
Ujenzi wa magati mawili katika bandari ndogo za Kagunga na Kibirizi ulio katika hatua ya zabuni na unaotarajiwa kuanza katika mwaka wa fedha 2012/2013;
Ujenzi wa gati la Mafia unaoendelea na unaotarajiwa kukamilika mwezi Septemba 2012.
Mheshimiwa Spika, umuhimu wa Bandari ya Bagamoyo unatokana na ongezeko la shehena na tatizo la bandari ya Dar es Salaam kuwa na eneo finyu la upanuzi.  Bandari ya Bagamoyo inajengwa kufanikisha shughuli za EPZA ambazo zitaendelezwa Bagamoyo. Mradi umefanyiwa upembuzi yakinifu mwaka 2010 na imeonyesha ni wa manufaa. Ripoti imependekeza ujenzi wa bandari ya kisasa yenye kina cha mita 14 na hivyo kuruhusu meli kubwa zenye uwezo wa kubeba makasha 7,000 hadi 8,000. Jumla ya ekari 1500 zimetengwa kwa ajili ya mradi huu. Hatua iliyofikiwa hivi sasa ni kuwa TPA imemwajiri Mtaalamu kutoka Chuo Kikuu cha Ardhi kufanya tathmini ya eneo kwa ajili ya kubainisha gharama za fidia na hatua za umiliki wa eneo.
Mheshimiwa Spika, pamoja na kwamba TICTS bado haijawekeza kikamilifu kwenye vifaa kuweza kuhudumia mizigo kwa ufanisi bandarini na kitengo cha makasha cha TPA bado hakijajingea uwezo mkubwa wa vifaa vya kuhudumia makasha bandarini hivyo kusababisha ucheleweshwaji wa meli, TICTS sasa wanakamilisha ujenzi wa reli katika gati Na 8 ili waweze kupokea mtambo mkubwa wa kupakulia makasha (Ship to Shore Gantry Crane) ifikapo mwezi Novemba, 2012. Aidha, mipango ipo mbioni ya kutumia reli ya TRL kusafirisha makasha hadi kituo cha ICD cha Ubungo. 
Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2012/2013, Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari imelenga kuhudumia jumla ya tani milioni 12.65 yakiwemo makasha 576,300 ikilinganishwa na tani milioni 12.084 yakiwemo makasha 530,089 yaliyohudumiwa mwaka 2011/2012. Makasha 170,000 yahudumiwa na kitengo cha makasha TPA. Kitengo cha TICTS kimelenga kuhudumia makasha  406,300 sawa na ongezeko la makasha 14,700 ikilinganishwa na makasha 357,105 yaliyohudumiwa mwaka 2011/2012. 
Mheshimiwa Spika, Wizara kupitia Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari katika kipindi cha mwaka wa fedha 2012/2013 imepanga kutekeleza miradi muhimu ifuatayo: ujenzi wa magati Na. 13 na 14 katika Bandari ya Dar es Salaam, ujenzi wa magati manne (4) katika Bandari ya Mtwara, mradi wa kuwaweka pamoja watoa huduma (Single Window System), ujenzi wa gati Bandari ya Kiwira, awamu ya pili ya ujenzi wa SPM, mradi wa Integrated Security System, ukarabati wa Bandari za Maziwa na ununuzi wa vifaa mbalimbali kwa bandari zote. Gharama za kutekeleza miradi hiyo ni shilingi bilioni 482.403. Kati ya hizo asilimia 19.6, sawa na shilingi bilioni 94.819 zitatokana na mapato ya Mamlaka na asilimia 80.04 sawa na shilingi bilioni 387.584 zitatoka kwa wahisani, mikopo na wawekezaji binafsi.

Udhibiti wa Usalama wa Vyombo vya Usafiri Majini
Mheshimiwa Spika, SUMATRA imeendelea kusimamia Usalama na Ulinzi wa vyombo vya usafiri majini kwa kuzingatia itifaki na mikataba mbalimbali ya kimataifa iliyoridhiwa na nchi yetu na kusimamiwa na Shirika la Kimataifa linaloratibu Usafiri wa Majini (International Maritime Organization-IMO). Aidha, SUMATRA kwa kuzingatia Sheria ya Usafiri Majini (Merchant Shipping Act, 2003) Namba 21 ya mwaka 2003 na kanuni zake, imeendelea kutekeleza majukumu mbalimbali ya usalama, ulinzi na uhifadhi wa mazingira  majini. 
Mheshimiwa Spika, hadi Juni 2012, masjala ya Tanzania Bara inayosimamiwa na SUMATRA ilikuwa na jumla ya Meli 100. Meli hizo zilisajiliwa kwa mujibu wa Merchant Shipping Act 2003. Masharti ya usajili yanajumuisha umri wa meli ambao hauzidi miaka 15 kwa usajili wa kwanza, ubora wa meli kwa ujumla wake, vifaa vya usalama na umiliki (meli lazima imilikiwe na Watanzania kwa hisa yazaidi ya asilimia hamsini).
Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2011/2012 SUMATRA imeendelea na jukumu la kuhakikisha kwamba vyombo vya usafiri majini vinakidhi viwango vya ubora. SUMATRA imekuwa ikifanya kaguzi za vyombo vya majini mara kwa mara na inapogundulika kuwa vyombo hivyo havikidhi ubora, wenye vyombo hulazimika kuvifanyia marekebisho kabla ya kupewa vyeti vya ubora (Seaworthiness Certificates) na kuendelea kutumika. Katika kipindi cha Julai, 2011 na Juni, 2012 SUMATRA ilikagua jumla ya vyombo vidogo vya usafiri majini 2,949 ikilinganishwa na vyombo 2,076 katika kipindi kama hicho kwa mwaka 2010/2011. Kati ya vyombo hivyo, 1,740 au asilimia 59 vilikidhi viwango vya usalama na kupewa vyeti. Aidha, vyombo 1,209 sawa na asilimia 41 vilishindwa kukidhi vigezo na kuzuiliwa kufanya kazi majini. Sababu kubwa ya kushindwa vigezo ilikuwa ni kukosa vifaa vya kujiokoa na hasa mavazi ya kujiokolea (life-jackets). Kwa vyombo vikubwa vya usafiri majini, yaani vile vyenye tani 50 na kuendelea, SUMATRA ilifanya jumla ya kaguzi 186 ikilinganishwa na kaguzi 118 katika kipindi cha mwaka 2010/2011. Meli 4 zilikutwa na kasoro na kuzuiliwa kufanya kazi.
Mheshimiwa Spika, pamoja na kufanya kaguzi za mara kwa mara katika vyombo vya majini, SUMATRA imeendelea kutoa elimu ya usafiri salama kwa waendeshaji wa vyombo, wamiliki, abiria na wadau. Wamiliki na waendeshaji vyombo wameendelea kuelimishwa ili wawe waangalifu na kuchukua tahadhari wakati wote na hasa miezi ya Mei, Juni na Julai ambapo ajali nyingi hujitokeza kutokana na upepo mkali. Aidha, msisitizo umekuwa ukitolewa kwa wamiliki wa vyombo vya majini kuwa na mavazi ya kujiokolea (Life jackets) na kuwaelimisha wasafiri kuhusu jinsi ya kutumia mavazi hayo kabla ya kuanza safari. Kutokana na umuhimu wa mavazi ya kujiokoa na wajibu uliowekwa kisheria wa kila chombo cha majini kuwa na vifaa hivyo, Wizara yangu inaiagiza SUMATRA kuhakikisha kwamba vyombo vyote vya abiria vya majini haviondoki bandari yoyote nchini bila kuwa na mavazi ya kujiokolea kwa idadi stahiki.  
Mheshimiwa Spika, SUMATRA imeendelea kuthibitisha sifa za wafanyakazi katika vyombo vya usafiri majini na kutoa vyeti kwa mujibu wa mkataba wa Kimataifa unaosimamia viwango vya mafunzo, utoaji vyeti na uangalizi wa wafanyakazi melini wa mwaka 1978 kama ulivyofanyiwa marekebisho mwaka 1995 (International Convention on Standards of Training, Certification and Watchkeeping for Seafarers 1978 as amended). Idadi ya vyeti vilivyotolewa na Mamlaka baada ya mabaharia kupata mafunzo kutoka Chuo cha Bahari cha Dar es Salaam (DMI) katika kipindi cha Julai 2011 hadi Juni 2012 ni 7,481 ikilinganishwa na vyeti 6,128 vilivyotolewa katika kipindi kama hicho kwa mwaka 2010/2011.
Mheshimiwa Spika, katika kipindi cha Julai, 2011 hadi Juni 2012, idadi ya ajali za vyombo vya majini zilizoripotiwa Tanzania zilikuwa 15 ambapo jumla ya watu 581 waliokolewa na 17 kupoteza maisha ikilinganishwa na ajali 9 zilizoripotiwa mwaka 2011 ambapo watu 91 waliokolewa na 51 kupoteza maisha. Kuimarika kwa mfumo wa upashanaji habari za matukio ya ajali majini kwa kutumia Kituo cha Utafutaji na Uokoaji (Maritime Rescue Coordination Centre-MRCC) kilichopo Dar es Salaam kumesaidia upatikanaji wa taarifa za matukio ya ajali na uokoaji. Aidha, Kituo kiliendelea kuratibu shughuli za utafutaji na uokoaji katika pande zote mbili za Jamhuri ya Muungano. 
Mheshimiwa Spika, Kituo cha MRCC hufanya kazi saa 24 kila siku na kimeendelea pia kuratibu masuala ya kuzuia uchafuzi wa mazingira baharini, kutambua meli katika mwambao wa nchi yetu kwa kutumia mtandao wa vifaa vya Automatic Identification System (AIS), kufuatilia meli zikiwa masafa marefu kutumia mfumo wa Long Range Identification and Tracking of Ships (LRIT), kupokea na kutoa habari za uharamia kupitia kituo maalum (Information Sharing Centre) chini ya Makubaliano ya Djibouti (Code of Conduct Concerning the Repression of Piracy and Armed Robbery Against Ships in the Western Indian Ocean and the Gulf of Aden (Djibouti Code of Conduct)). Makubaliano haya yanajumuisha nchi 19 katika ukanda huu na kuna vituo vitatu vya kupashana habari za uharamia kikiwemo cha Dar es Salaam kilichopo kwenye MRCC.
Mheshimiwa Spika, pamoja na kwamba suala la uchukuzi majini si suala la Muungano na Serikali zetu mbili zina vyombo viwili vya  udhibiti na usimamizi wa masuala ya usalama majini yaani, SUMATRA na Zanzibar Maritime Authority (ZMA) ambavyo vinasimamiwa na sheria mbili tofauti, Wizara ya Uchukuzi ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Wizara ya Miundombinu na Mawasiliano ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar zimeelekezwa na Mamlaka za juu za Serikali zetu mbili kuhakikisha kuwa SUMATRA na ZMA zinafanya kazi kwa karibu na ushirikiano na kuoanisha taratibu zao za kazi katika usajili, ukaguzi na uhakiki wa vyombo vya majini na wadau, taratibu za utafutaji na uokoaji na kubadilishana taarifa muhimu. 
Mheshimiwa Spika, SUMATRA ilitoa leseni 29 kwa Makampuni ya Uwakala wa Meli katika kipindi cha Julai 2011 hadi Juni 2012. Aidha, katika usajili wa Makampuni ya kuondosha mizigo Bandarini, Mamlaka ilisajili na kutoa hati za usajili kwa makampuni 573 katika kipindi cha Julai 2011 hadi Juni 2012, ukilinganisha na makampuni 604 yaliyosajiliwa kipindi kama hicho mwaka 2010/2011.

USAFIRI NA UCHUKUZI KWA NJIA YA ANGA

Huduma za Viwanja vya Ndege
Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2011/2012, Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA) iliendelea kuhudumia viwanja vya ndege kwa kuzingatia sera ya kuwezesha viwanja vya ndege kujiendesha kibiashara, kujitosheleza kwa mapato na kujitegemea. Miongoni mwa mambo muhimu ambayo Mamlaka iliendelea kuyafanya ni pamoja na upanuzi na uendelezaji wa viwanja vya ndege nchini na matengenezo ya kawaida ya viwanja vya ndege ili kuwezesha ndege kutua na kuruka kwa usalama. 
Mheshimiwa Spika, katika kipindi cha mwaka wa fedha 2011/2012 idadi ya safari za ndege ziliongezeka kwa asilimia 15.8 kutoka jumla ya safari za ndege 132,225 mwaka 2010/2011 hadi kufikia safari za ndege 153,068 mwaka 2011/2012. Aidha, idadi ya abiria iliongezeka kwa asilimia 20.9 kutoka jumla abiria 2,271,497 mwaka 2010/2011 na kufikia idadi ya abiria 2,745,743 mwaka 2011/2012. Vilevile katika kipindi cha mwaka wa fedha 2011/2012, tani za mizigo  ziliongezeka kwa asilimia 9.5 kutoka tani za mizigo 26,024.9 mwaka 2010/2011 hadi kufikia tani za mizigo 28,492.5 mwaka 2011/2012. Takwimu hizi ni kwa viwanja vinavyoendeshwa na Mamlaka ya Viwanja vya Ndege tu.
Mheshimiwa Spika, katika  kipindi cha mwaka wa fedha 2011/2012 Serikali kupitia Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania ilikamilisha ukarabati na upanuzi wa Kiwanja cha Ndege cha Mpanda kwa kiwango cha lami kwa gharama ya shilingi bilioni 30. Kiwanja hiki sasa kina uwezo wa kuhudumia ndege zenye uwezo wa kuchukua abiria hamsini (50) na kina hadhi ya kiwanja cha mkoa. Kuhusu kiwanja cha ndege cha Kimataifa cha Songwe, kazi ya ujenzi wa barabara ya kutua na kurukia ndege pamoja na ujenzi wa barabara ya kuingia kiwanjani na maegesho ya magari vimekamilika. Kazi za ujenzi wa maegesho ya ndege (Apron) na majengo zinaendelea na zinategemea kukamilika mwishoni mwa mwaka huu.
Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2011/2012 Mamlaka ya Viwanja vya Ndege imekamilisha pia ukarabati wa jengo la abiria katika Kiwanja cha Ndege cha Mtwara kwa gharama ya shilingi. milioni 500 na jengo hilo limeanza kutumika tarehe 15 Julai 2012. Aidha, katika kiwanja cha ndege cha Arusha, Mamlaka ya Viwanja vya Ndege imekamilisha ukarabati wa barabara ya kurukia ndege kiwango cha lami kwa mita 420 na hivyo kufanya urefu wa barabara hiyo kwa kiwango cha lami kuwa mita 1,620 kwa gharama ya shilingi bilioni 1.7. 
Mheshimiwa Spika, kazi za uboreshaji wa Viwanja vya ndege vya Tabora, Kigoma na Bukoba zilianza katikati ya mwezi Desemba 2011 baada ya kusainiwa kwa mikataba ya kazi mwezi Septemba 2011. Kazi za ujenzi katika viwanja hivi zitahusu uboreshaji wa miundombinu, yaani barabara za kutua na kurukia ndege (runways), barabara za viungo (taxiways) na maegesho ya ndege kwa kiwango cha lami, ujenzi wa majengo ya abiria na usimikaji wa taa za kuongoza ndege kutua usiku na hivyo kuwezesha viwanja hivyo kutumika kwa saa 24. Ukarabati wa viwanja hivi unagharamiwa kwa pamoja kati ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania (kwa asilimia 17) na Benki ya Dunia (kwa asilimia 83). Aidha kazi za ukarabati wa kiwanja cha ndege cha Mafia kwa kiwango cha lami zimeanza. Mradi huu unagharamiwa kwa pamoja kati ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Marekani kupitia Shirika la Changamoto za Millenia (MCC).  
Mheshimiwa Spika, kuhusu Kiwanja cha ndege cha Mwanza, Mkataba kwa ajili ya utekelezaji wa mradi wa ukarabati na upanuzi wa Kiwanja hiki umesainiwa tarehe 11 Juni 2012. Mkandarasi wa mradi huu alikabidhiwa eneo la ujenzi tarehe 29 Juni 2012 na anatarajiwa kuanza kazi rasmi mwezi Oktoba 2012. Mradi huu utahusisha ujenzi wa jengo jipya la abiria (passenger terminal building), ujenzi wa jengo la kuongozea ndege (control tower), ujenzi wa jengo la mizigo (cargo terminal), maegesho ya ndege na magari, pamoja na urefushaji wa barabara ya kurukia na kutua ndege kwa mita 500. Mradi huu unagharamiwa kwa pamoja kati ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Benki ya Kiarabu ya Maendeleo ya Afrika (BADEA) na Mfuko wa Maendeleo wa Nchi zinazozalisha na kuuza mafuta nje ya nchi zao kwa wingi (OPEC).
Mheshimiwa Spika, ili kuboresha usalama wa viwanja vya ndege nchini katika mwaka wa fedha 2011/2012, Mamlaka ilinunua na kusimika vifaa maalum vya ukaguzi wa abiria na mizigo kama ifuatavyo:- mashine za ukaguzi (X–ray Machines) mpya kwenye viwanja vya Bukoba, Lake Manyara, Arusha, Mwanza na Shinyanga, “Walk Through Metal Detectors” mpya kwa viwanja vya ndege vya Mwanza, Arusha, Mtwara, Tanga, Lake Manyara, Musoma, Bukoba na Shinyanga na “Hand-Held Metal Detectors” kwa viwanja vyote vya mikoani. Aidha, katika mwaka wa fedha 2011/2012, Mamlaka ya Viwanja vya Ndege iliandaa miongozo mbalimbali ya uendeshaji wa viwanja vya ndege kwa viwanja vya Mpanda, Lindi, Songea, Mafia, Nachingwea na Lake Manyara na hatimaye kupatiwa hati za uendeshaji wa viwanja vya ndege (aerodrome certificates) kwa viwanja vya Lake Manyara, Bukoba, Mpanda na Mafia kwa mujibu wa miongozo inayotolewa na Shirika la Usafiri wa Anga Duniani (ICAO).
Mheshimiwa Spika, Mamlaka ya Viwanja vya Ndege iliendelea na juhudi za kuboresha huduma za zimamoto katika viwanja vya ndege, katika mwaka wa fedha wa 2011/2012 Mamlaka ilinunua vifaa mbalimbali vya zimamoto pamoja na dawa za zimamoto kwa matumizi ya viwanjani kulingana na mahitaji. Mamlaka pia ilinunua magari mapya manne (4) ya zimamoto kwa gharama ya shilingi bilioni 5.6 na tayari yapo katika viwanja vya ndege vya JNIA (magari mawili), Arusha (gari moja) na Mwanza (gari moja). Aidha, ili kuimarisha shughuli za uokoaji na uzimaji moto viwanjani wakati wa ajali za ndege, Mamlaka iliweza kufanya mazoezi ya namna ya kukabiliana na majanga ya moto na dharura katika viwanja vya ndege vya Julius Nyerere (JNIA), Tabora, Shinyanga na Lake Manyara. Vile vile Mamlaka ya Viwanja vya Ndege inaendelea na juhudi za kutwaa umiliki wa ardhi kwa maeneo mapya kwa ajili ya viwanja vipya vya ndege. Maeneo hayo ni Bagamoyo (Pwani), Isaka (Shinyanga), Kisumba (Sumbawanga), Msalato (Dodoma), Ngungungu (Manyara) na Omukajunguti (Kagera). 
Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2012/2013 Serikali itaendelea na utekelezaji na ukamilishaji wa miradi mbalimbali inayoendelea. Miradi hiyo ni pamoja na:-
Kuimarisha na kuboresha Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA) kwa kujenga jengo jipya la abiria na majengo mengine ya huduma za ndege na abiria ambao umetengewa shilingi bilioni 2.13. Aidha, Serikali inaendelea kukamilisha taratibu za kupata mkopo kwa ajili ya kugharamia mradi huu;
Kukamilisha ujenzi wa kiwanja kipya cha Kimataifa cha Ndege cha Songwe (Mbeya) ambapo shilingi bilioni 17.5 zimetengwa;
Kuendelea na uboreshaji wa kiwanja cha ndege cha Mwanza ambapo shilingi bilioni 18.0 zimetengwa; 
Kukamilisha ukarabati wa Kiwanja cha ndege cha Bukoba ambapo shilingi bilioni 20.55 zimetengwa;
Kukamilisha ukarabati wa Kiwanja cha ndege cha Kigoma ambapo shilingi bilioni 19.5 zimetengwa;
Kukamilisha ukarabati wa Kiwanja cha ndege cha Tabora ambapo shilingi bilioni 12.8 zimetengwa; 
Kukarabati kiwanja cha ndege cha Arusha kwa kujenga jengo la abiria na maegesho ya ndege ambapo shilingi bilioni 1.52 zimetengwa;
Kuanza ukarabati wa viwanja vya ndege vya Shinyanga na Sumbawanga ambapo Benki ya Uwekezaji ya Ulaya (EIB) imekubali kugharamia.

Aidha, TAA itaendelea kufanyia matengenezo viwanja vingine vya ndege kwa kutumia mapato yake ili viendelee kutoa huduma kwa usalama. Vile vile TAA itaendelea kutekeleza miradi mbalimbali  ikiwa ni pamoja na usimikaji wa mfumo  wa uhakiki wa abiria na mizigo (CUTE System), ufungaji wa mitambo ya umeme wa dharura katika viwanja vya ndege vya JNIA, Mafia na Mtwara, kuweka vivuko vipya vya abiria (Aerobridges) JNIA kwa kutumia mapato yake.
Mheshimiwa Spika, pamoja na kuendelea kutekeleza majukumu yake, TAA inakabiliwa na changamoto mbalimbali zikiwemo  uwezo mdogo wa kifedha ikilinganishwa na mahitaji ya ukarabati na uendelezaji wa miundombinu ya viwanja, uvamizi wa maeneo ya viwanja vya ndege unaokwamisha juhudi za upanuzi wa miundombinu. Changamoto nyingine ni matukio ya vitendo vya kigaidi na uhalifu dhidi ya usafiri wa anga duniani, mabadiliko ya kasi ya matumizi ya teknolojia katika usafiri wa anga duniani na kutokuwa na Chuo cha zimamoto nchini chenye uwezo wa kutoa mafunzo endelevu ya kukidhi mahitaji.

Huduma za Usafiri wa Ndege
Mheshimiwa Spika, katika kipindi cha 2011/2012 mwezi Novemba 2011 Kampuni ya Ndege Tanzania ilifanikiwa kuanza safari za Dar es Salaam kwenda Tabora na Kigoma kwa kutumia ndege ya Dash-8 yenye uwezo wa kubeba abiria 50. Katika kipindi cha tarehe 1 Novemba, 2011 hadi kufikia Februari, 2012, Kampuni imesafirisha abiria 8,342 ikilinganishwa na abiria 7,584 waliosafirishwa katika kipindi hicho hicho katika mwaka wa fedha 2010/2011. Ongezeko hili ni sawa na asilimia 10.
Mheshimiwa Spika, mwezi Aprili, 2012 Ndege moja ya kampuni aina ya Dash 8-Q300 ilipata ajali ilipokuwa inajiandaa kuruka kwenye Kiwanja cha Ndege cha Kigoma. Katika ajali hiyo, abiria wote waliokuwa kwenye ndege walitoka salama ingawa ndege iliharibika vibaya. Ili kuendelea kutoa huduma, mwezi Mei, 2012 Kampuni ilikodi ndege aina ya Boeing 737-500 ambayo inatoa huduma katika viwanja vya Dar es salaam, Kilimanjaro, Mwanza na Comoro. Katika kipindi cha mwaka 2011/2012 ATCL imeendelea kukabiliana na changamoto mbalimbali ikiwa ni pamoja na gharama kubwa za uendeshaji, madeni, mtaji mdogo na upungufu wa wataalam hususan marubani na wahandisi wa ndege. Kampuni imeendelea kukabiliana na changamoto hizo kwa kushirikiana na Serikali.
Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2012/2013, ATCL itaendelea kutoa huduma kwa kutumia ndege ya kukodi aina ya Boeing 737-500 na ndege yake aina ya Dash 8-Q300 ambayo kwa sasa inafanyiwa matengenezo makubwa hapa nchini ambayo yatakamilika katikati ya mwezi huu wa Agosti, 2012. Aidha, kwa kutumia fedha ambazo Kampuni imelipwa shilingi bilioni 12.2 kutokana na bima ya ajali ya ndege iliyotokea mwezi Aprili, 2012, kati ya fedha hizo shilingi bilioni 10.6 zitatumika kama malipo ya awali kwa ajili ya kununua ndege mbili mpya. ATCL pia itaendelea kutoa mafunzo kwa wafanyakazi wake katika nyanja mbalimbali. 
Mheshimiwa Spika, Wakala wa ndege za Serikali (TGFA) umeendelea kutoa huduma za usafiri wa ndege kwa Viongozi Wakuu wa Serikali. Katika mwaka 2011/2012, Serikali kupitia TGFA imefanya matengenezo makubwa na ya kawaida kwa ndege zake kwa lengo la kuhakikisha kuwa ziko katika hali nzuri na salama. Katika mwaka 2012/2013, Serikali kupitia TGFA itaendelea kuzifanyia matengenezo ndege hizo kwa kufuata ratiba ya matengenezo ya ndege hizo (Maintenance Schedule) ili kuhakikisha usalama wake. Aidha, Serikali itaendelea kutoa mafunzo kwa marubani na wahandisi ili kuhuisha leseni zao za kuhudumia ndege hizo.
Udhibiti wa Usalama wa Usafiri wa Anga
Mheshimiwa Spika, Sekta ndogo ya usafiri wa anga imeendelea kukua. Idadi ya abiria waliotumia usafiri huu iliongezeka kutoka abiria 3,472,115 mwaka 2010/2011 na  kufikia abiria  4,034,152 mwaka 2011/2012 sawa na ongezeko la asilimia 16. Katika kipindi cha mwaka 2012/2013 idadi ya abiria inakadiriwa kufikia 4,327,977 ambalo ni ongezeko la asilimia 7. Idadi ya abiria waliosafiri kwenda na kutoka nje ya nchi iliongezeka kutoka 1,602,562 mwaka 2010/2011 na  kufikia abiria 1,873,476 mwaka 2011/2012, hii ikiwa ni ongezeko la asilimia 17. Aidha abiria wa ndani wameongezeka kutoka abiria 1,869,553 mwaka 2010/2011 na  kufikia abiria 2,160,676 mwaka 2011/2012, sawa na ongezeko la asilimia 16. Sababu kubwa ya ongezeko la abiria wa ndani ni kukua kwa uchumi  nchini, ukiwemo utalii na kuongezeka kwa uwezo wa ubebaji (available seat capacity) kutoka viti 2,440 mwaka 2010/2011 hadi viti 2,636 mwaka 2011/2012. 
Mheshimiwa Spika, kwa upande wa safari za ndege (aircraft movements), kulikuwa na ongezeko la asilimia  11 kutoka safari 193,250 mwaka 2010/2011 hadi safari  214,460 mwaka 2011/2012. Kati ya hizi, safari za kimataifa zimeongezeka kutoka safari 31,992 mwaka 2010/2011 hadi kufikia safari 37,088 mwaka 2011/2012, sawa na ongezeko la asilimia  16.  Safari za ndege humu nchini pia zimeongezeka kutoka safari  161,258 mwaka 2010/2011 hadi kufikia safari 177,372 mwaka 2011/2012, sawa na ongezeko la asilimia  10. 
Mheshimiwa Spika, katika kipindi cha mwaka 2011/2012, mizigo iliyobebwa kwa kutumia usafiri wa anga imepungua kutoka tani 31,710.6 mwaka 2010/2011 hadi tani 31, 683.4. Wizara na taasisi zake zitaendelea na juhudi zake za kupata mashirika ya ndege yatakayotoa huduma za kubeba mizigo katika kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Kilimanjaro na Mwanza. Juhudi hizo zinategemea kuongeza mizigo itakayobebwa kufikia tani 40,000 mwaka 2012/2013.
Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2011/2012, makampuni ya ndege kumi na mbili (12) yalipewa leseni mpya ili kutoa huduma ya usafiri wa ndege ndani na nje ya nchi baada ya kutimiza masharti. Hadi kufikia Juni 2012 jumla ya makampuni ya ndege hamsini na mbili (52) tayari yalikuwa yameidhinishwa kutoa huduma hiyo ya usafiri wa ndege. Katika kipindi cha mwaka 2012/2013, inatarajia  kutoa leseni mpya kwa makampuni (6) ya ndege na kufanya jumla ya makampuni ya ndege yatakayokuwa yameidhinishwa kutoa huduma ya usafiri wa anga kufikia hamsini na nane (58) sawa na ongezeko la asilimia kumi na mbili (12).
Mheshimiwa Spika, kuhusu mikataba ya usafiri wa anga (Bilateral Air Services Agreements-BASA) kati ya Tanzania na nchi nyingine, Wizara ya Uchukuzi, imeendelea kufanya mazungumzo na nchi mbalimbali ili kuipitia mikataba hiyo upya kwa ajili ya kukidhi mahitaji ya soko na hali halisi ya maendeleo na mabadiliko katika sekta hii. Katika kipindi cha mwaka 2011/2012, Mikataba kati ya Tanzania na Misri, Afrika Kusini na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo ilipitiwa upya. Aidha, tumeendelea kulegeza vikwazo vya kibiashara katika sekta hii ndogo ya Usafiri wa Anga, kulingana na Makubaliano ya Yamoussoukro (YD), huku tukizingatia jukumu la Serikali la kulinda makampuni yetu ya ndege ya ndani. 
Mheshimiwa Spika, hadi kufikia mwaka 2011/2012, Tanzania ilikuwa imeingia makubaliano (BASA) na nchi arobaini na tisa (49). Kati ya mikataba hiyo  ni nchi 19 tu ambazo mashirika yake ya ndege yanatoa huduma kati yake na Tanzania. Katika mwaka 2011/2012, idadi ya mashirika yanayotoa huduma kupitia utaratibu wa “BASA” ni ishirini na tatu (23). Aidha, safari za ndege kati ya nchi hizo na Tanzania zilikuwa mia moja na ishirini (120) kwa wiki. Katika mwaka 2012/2013, tunatarajia kuwa na makampuni ishirini na sita (26) ambapo safari za ndege zitaongezeka kufikia zaidi ya mia moja na thelathini (130) kwa wiki. Hii itatokana na upitiaji upya wa mikataba, ukuaji wa sekta ya utalii na uwekezaji nchini.
Mheshimiwa Spika, katika kipindi cha mwaka 2011/2012, zilitokea ajali mbili (2) na matukio kumi (10) ikilinganishwa na ajali tano (5) na matukio nane (8) yaliyotokea katika kipindi cha 2010/2011. Miongoni mwa ajali zilizotokea mwaka 2011/2012, ajali moja ilihusisha ndege aina ya  Piper PA 34-220T yenye usajili 5H-QTE iliyoanguka ikielekea Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Kilimanjaro mwezi  Novemba, 2011. Aidha, ajali nyingine ilihusisha ndege ya ATCL aina ya Dash 8-Q300 ambayo ilipata ajali katika Kiwanja cha ndege cha Kigoma wakati ikijiandaa kuruka mwezi Aprili, 2012. Uchunguzi wa vyanzo vya ajali hizi unaendelea. 
Mheshimiwa Spika, lengo la Mamlaka ni kuendelea kuboresha usimamizi na kuhakikisha ajali zinapungua mwaka hadi mwaka pamoja na safari kuongezeka. Mamlaka ya Usafiri wa Anga imejipanga kusimamia kwa karibu utekelezaji wa Kanuni na taratibu za  usalama wa usafiri wa anga kwa makampuni na watumishi kwenye sekta hii ya usafiri wa anga hapa nchini. Mamlaka inaendelea  kushirikiana na nchi nyingine katika Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC), mashirika na Jumuiya nyingine mbalimbali katika kuinua na kudumisha hali ya usalama wa usafiri wa anga.  
Mheshimiwa Spika, hali ya usalama wa viwanja vya ndege na anga la Tanzania imeendelea kuimarika kwa kudhibiti shughuli za ukaguzi wa kuingia katika viwanja vya ndege na ndani ya ndege kwa taratibu za kiusalama zilizowekwa kwa mujibu wa sheria. Taratibu za ukaguzi zimeimarishwa  kwa lengo la kuzuia matukio yoyote ya uhalifu katika viwanja vya ndege, hasa kufuatia matukio ya mashambulizi ya mabomu katika nchi jirani za Uganda na Kenya. Jukumu hili limeendelea kufanywa kwa ushirikiano kati ya Mamlaka ya Usafiri wa Anga, Viwanja vya Ndege, makampuni ya ndege na vyombo vya ulinzi na usalama. Aidha, katika kipindi cha 2011/2012 hakuna matukio ya kutisha ya kiusalama yaliyotokea katika sekta hii ndogo hapa Tanzania. 
Mheshimiwa Spika, pamoja na juhudi zote hizi, bado zipo changamoto za miundombinu ya majengo ya abiria ambayo uwezo wake hauendani na ukuaji wa haraka wa sekta hii ndogo.  Pia, ukosefu wa uzio katika viwanja vingi  na upungufu wa vifaa vya ukaguzi wa abiria na mizigo katika baadhi ya viwanja vyetu bado ni changamoto.  
Mheshimiwa Spika, Tanzania kama mwanachama wa Shirika la Kimataifa la Usafiri wa Anga (ICAO) imeingia katika makubaliano ya kutekeleza mpango mpya ujulikanao kama Continuous Monitoring Approach (CMA) ambao unawezesha ICAO kubaini kiwango cha utekelezaji wa kanuni za kimataifa za usafiri wa anga. Chini ya mpango huu, Tanzania na nchi nyingine zitawasilisha taarifa zake ICAO za udhibiti wa usafiri wa anga kwa njia ya mtandao. Kazi ya ICAO ni kuzihakiki ili kuona kama zimekidhi viwango vinavyotakiwa. Kutokana na ripoti hizi, ICAO itachukua hatua ya kuzikagua na kusaidia nchi hizo ili zifikie viwango stahiki.    
Mheshimiwa Spika, Mamlaka inatarajia kuanza kutoa huduma za uongozaji ndege katika kiwanja kipya  cha Songwe ambacho kipo katika hatua za mwisho za ujenzi. Hivi sasa kwa kushirikiana na Uongozi wa Mkoa wa Mbeya, Mamlaka ya Usafiri wa Anga imemilikishwa eneo sehemu ya Iwambi ambapo mtambo maalumu wa kuongozea ndege zitakazotua katika Kiwanja cha ndege cha Songwe utafungwa. Hatua iliyofikiwa kwa sasa ni kuanza kazi ya ujenzi wa jengo ambalo mtambo huo unaojulikana kama ‘Non Directional Beacon (NDB)’ utafungwa. Mtambo kama huu pia utafungwa katika Kiwanja cha Ndege cha Shinyanga na Mafia katika mwaka 2012/2013. Aidha, taratibu za awali zinakamilishwa ili huduma za uongozaji ndege katika Kiwanja cha ndege cha Bukoba zianze kutolewa ifikapo Desemba 2013.
Mheshimiwa Spika, Mamlaka ya Usafiri wa Anga imeweza kufunga mitambo mipya  ya kuongozea ndege (NDB) katika Viwanja vya ndege vya Dodoma, Pemba, na Arusha. Hatua za kuandaa na kukamilisha mifumo na ramani ya taratibu za maandalizi ya utuaji wa ndege (Instrument Approach Procedures) kwa viwanja vya ndege vya Zanzibar na Mwanza zimekamilika na kupitishwa kwa ajili ya matumizi ya marubani. Mchakato wa kukamilisha ramani kama hizo kwa viwanja vya Arusha na Songwe unaendelea na utakamilika katika mwaka 2012/2013. Kwa upande wa mawasiliano ya anga, Mamlaka ya Usafiri wa Anga inaendelea na mchakato wa kubadilisha kutoka mfumo wa mawasiliano kupitia njia za ardhini na kwenda kwenye mfumo wa satelaiti ambao ni bora na wa uhakika. Aidha, mchakato wa  kutumia mfumo mpya na wa kisasa wa teknolojia ya ufuatiliaji safari za ndege (Automatic Dependent Surveillance – Broadcast  au ADS-B) katika  anga  la Tanzania unaendelea vizuri na awamu ya kwanza ya utekelezaji itaanza katika mwaka wa fedha 2012/2013.  
Mheshimiwa Spika, kwa kushirikiana na Idara ya Upimaji na Ramani (Survey and Map Division - SMD), katika Wizara ya Ardhi na Maendeleo ya Makazi, Mamlaka ya Usafiri wa Anga imeweza kutengeneza na kusambaza ramani (World Aeronautical Charts - WAC) zinazohitajika kwa matumizi ya usafiri wa anga. Mamlaka ya Usafiri wa Anga pia inaendelea na mchakato wa kubainisha alama (coordinates) za viwanja vya ndege vya Dar es Salaam, Arusha, Zanzibar, Mafia, Iringa, Shinyanga na Tabora kwa kutumia mfumo wa satelaiti (World Geodatic System-WGS 84). Hatua zaidi zinaendelea kuchukuliwa na Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania ili kuoanisha mfumo wetu na mifumo ya kimataifa ya upashanaji habari wa safari za ndege (ICAO New Flight Plan). Nchi zote duniani zinatakiwa kukamilisha mpango huu ifikapo tarehe 15 Novemba 2012. Napenda kulifahamisha Bunge lako tukufu kwamba Mamlaka ya Usafiri wa Anga imeanza utaratibu wa kutekeleza mpango  huo mpya.

HUDUMA ZA HALI YA HEWA
Mheshimiwa Spika, katika Mwaka wa fedha 2011/2012, Mamlaka ya Hali ya Hewa imeendelea kuboresha utoaji wa huduma za hali ya hewa nchini, ambapo vituo saba vilivyo chini ya zoezi la Quality Management Systems (QMS) vimeongezewa wafanyakazi, kufungwa vifaa vipya na baadhi ya vifaa kufanyiwa uhakiki (calibration). Mamlaka ilifanyiwa tena ukaguzi wa Kimataifa kwa utoaji wa huduma bora za hali ya hewa kwa ajili ya Usafiri wa Anga mnamo mwezi Disemba 2011 na kuthibitishwa tena kuendelea kukimiliki Cheti cha (ISO 9001:2008). Aidha, kituo cha kupima hali ya hewa ya anga za juu (Upper Air Station) katika Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA) kimeboreshwa kwa kufungwa mtambo mpya wa kisasa wa kufuatilia mwenendo wa hali ya hewa kwa anga za juu. 
Mheshimiwa Spika, Mamlaka ya Hali ya Hewa imeendelea kutimiza jukumu lake la kuiwakilisha nchi katika Jumuiya za Kimataifa katika masuala ya Hali ya Hewa. Hivi karibuni Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Hali ya Hewa, Dr. Agnes Kijazi ameteuliwa kuwa mjumbe wa Baraza kuu (Executive Council) la Shirika la Hali ya Hewa Duniani (WMO). Kufuatia uteuzi huo, Tanzania kupitia Mamlaka ya Hali ya Hewa imepewa jukumu la kuwa mratibu (focal point) wa Shirika hilo katika masuala ya hali ya hewa, maji na mazingira.
Mheshimiwa Spika, kupitia mradi wa Afrika Mashariki wa kutoa tahadhari juu ya matukio ya hali mbaya ya hewa (Severe Weather Forecasting Demonstration Project), Mamlaka imetengeneza na kuanza kutumia “software” kutoa tahadhari juu ya matukio ya hali mbaya ya hewa katika mikoa ya nchi za Afrika Mashariki iliyo karibu na Ziwa Victoria. Taratibu za kutumia ujuzi huo kwa maeneo mengine zinaendelea kukamilishwa. Viwango vya usahihi wa utabiri wa hali ya hewa vimeendelea kuwa bora ambapo kwa sasa usahihi wa utabiri wa msimu umefikia asilimia 84 na utabiri wa kila siku umefikia asilimia 82.7. Mamlaka iliweza kutabiri na kufuatilia mwenendo wa msimu wa mvua za vuli ambazo zilisababisha mafuriko na kuharibu miundombinu na mali za wananchi na baadhi ya wananchi kupoteza maisha katika baadhi ya maeneo hapa nchini mwezi Desemba 2011.
Mheshimiwa Spika, Mamlaka ya Hali ya Hewa (TMA) katika mpango wake wa kuhakikisha miundombinu ya hali ya hewa inaendelea kuimarika, Kituo cha Hali ya Hewa Mkoani Katavi kimeanza kufanya kazi, hivyo kuongeza idadi ya vituo vikuu vya hali ya hewa kutoka 27 na kufikia 28. Mamlaka pia inaendelea na uboreshaji wa miundombinu yake ya kukusanya takwimu za hali ya hewa ambapo mitambo saba ya kupima hali ya hewa inayojiendesha yenyewe imenunuliwa kwa gharama ya shilingi 160,099,284 na taratibu za kuifunga katika vituo mbalimbali zinaendelea. Aidha, TMA imeimarisha mfumo wa mawasiliano ya hali ya hewa kwa kuboresha mtambo wa kukusanya na kusambaza taarifa za hali ya hewa (Transmet) ambapo jumla ya shilingi 122,589,879 zilitumika. Uboreshaji huo umeongeza uwezo wa mtambo huo na kwa sasa unatumika kutuma taarifa za hali ya hewa kwa njia ya elektroniki kwenda kwenye vyombo vya habari. Utaratibu huu umepunguza gharama za kusambaza taarifa hizo. Mamlaka imeendelea kuboresha karakana ya kutengeneza vifaa vya hali ya hewa iliyopo Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere kwa kufunga mtambo wa kuhakiki “Barometers” uliogharimu shilingi 134,918,784. Jumla ya “Barometers” 7 za vituo vilivyo chini ya mradi wa QMS zimefanyiwa uhakiki (calibration). Hapo awali Mamlaka ilikuwa inalazimika kuvisafirisha vifaa hivyo (Barometers) mpaka Nairobi-Kenya kwa ajili ya kuvifanyia uhakiki.
Mheshimiwa Spika, pamoja na mafanikio hayo, Mamlaka iliendelea kukabiliwa na changamoto mbalimbali ambazo ni uchache wa mtandao wa vituo vya kupimia hali ya hewa na hivyo kuathiri usahihi wa utabiri kutokana na kukosekana kwa wigo mpana wa kupata taarifa za maeneo husika, uchakavu wa vifaa vya hali ya hewa na upatikanaji wa vifaa vya kisasa ili kuendana na mabadiliko ya teknolojia, upungufu wa wafanyakazi, kutokuwa na mfumo wa kisasa wa kuhifadhi taarifa na takwimu za hali ya hewa baada ya mfumo uliokuwa unatumiwa awali kupitwa na wakati na pia kuboresha Chuo cha Hali ya Hewa Kigoma.
Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2012/2013, TMA itaendelea kuboresha huduma za hali ya hewa kwa ajili ya maendeleo ya kiuchumi na kijamii pamoja na utoaji wa tahadhari juu ya hali mbaya ya hewa kwa ajili ya usalama wa watu na mali zao. Katika kipindi hiki, Mamlaka inatarajiwa kukamilisha ununuzi wa Rada ya pili ambayo itafungwa Mwanza. Mkataba wa kutengeneza Rada hiyo yenye thamani ya shilingi bilioni 3.615 ulisainiwa tarehe 18 Machi 2012. Mamlaka itaanza taratibu za ununuzi wa Rada ya tatu ya hali ya hewa na kupanua mtandao wa vituo vya hali ya hewa nchini kwa kuanza ujenzi wa kituo cha kupima hali ya hewa huko Manyara. Aidha, Mamlaka inatarajia kununua mitambo minne (4) ya kupima hali ya hewa inayojiendesha yenyewe (Automatic Weather Station).
Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2012/2013 TMA pia inatarajia kununua mtambo wa kuchambua taarifa za hali ya hewa kwa ajili ya kutoa utabiri (NWP-Computer cluster), na kuboresha Studio ya hali ya hewa kwa kufunga vifaa vya kisasa ili kutoka katika mfumo wa Analojia na kutumia Digitali, kushirikiana na taasisi mbalimbali zikiwemo za elimu ya juu katika kufanya tafiti za mabadiliko ya hali ya hewa na mazingira, kuendeleza ushirikiano na vyuo vikuu hapa nchini ili kuanzisha shahada ya hali ya hewa na kupunguza gharama kubwa za kusomesha wafanyakazi nje ya nchi, kuanzisha mtandao wa wadau wa hali ya hewa ili kuhakikisha upatikanaji na usambazaji wa taarifa za hali ya hewa kwa watumiaji walio wengi na kwa wakati, kushirikiana na kampuni ya “Starfish mobile” ya Tanzania kuanza kutoa huduma za hali ya hewa kupitia ujumbe wa simu za mkononi (SMS) na kuendelea kuboresha huduma za hali ya hewa kwa sekta ya usafiri wa anga ili kuhakikisha kuwa mafanikio yaliyopatikana ya kupata cheti cha ubora kinachotambuliwa na Shirika la Viwango Duniani (ISO) yanaendelezwa.
C. MAENDELEO NA MAFUNZO YA WATUMISHI 
Mheshimiwa Spika, ubora wa utendaji kazi unatokana na ubora na umahiri wa wafanyakazi. Kwa kutambua umuhimu huo, Wizara pamoja na Taasisi zilizo chini yake imeendelea kutoa mafunzo mbalimbali yenye lengo la kuboresha taaluma za wafanyakazi wake. Katika kipindi cha 2011/2012, jumla ya watumishi 1,930 walihudhuria mafunzo mbalimbali ndani na nje ya nchi. Kati ya hao, watumishi 109 walipatiwa mafunzo ya muda mfupi na 276 muda mrefu nje ya nchi. Aidha, watumishi 293 walipatiwa mafunzo ya muda mfupi na 1,252 mafunzo ya muda mrefu ndani ya nchi. 
Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2012/2013, Wizara pamoja na Taasisi zake itaendelea na utaratibu wa kupeleka watumishi mafunzoni kwa awamu kulingana na upatikanaji wa fedha kwa lengo la kuwaongezea ujuzi, ufanisi, na tija katika kufanya kazi zao. Jumla ya watumishi 2,167 watapatiwa mafunzo ya ndani na nje ya nchi.  Kati ya hao, watumishi 252 watahudhuria mafunzo ya muda mfupi nje ya nchi, 159 mafunzo ya muda mrefu nje ya nchi, 304 mafunzo ya muda mfupi ndani ya nchi na 1,452 mafunzo ya muda mrefu ndani ya nchi. 
Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2011/2012 Wizara pamoja na Taasisi zake ziliajiri watumishi 370, watumishi 473 walithibitishwa kazini na watumishi 599 walipandishwa vyeo. Katika mwaka 2012/2013, Wizara na Taasisi zimepanga kuajiri watumishi 637, kuthibitisha kazini watumishi 343 na kupandisha vyeo watumishi 934.

D. TAASISI ZA MAFUNZO
Mheshimiwa Spika, vyuo vya mafunzo ni muhimu katika kukuza na kuendeleza taaluma ya sekta ya uchukuzi na hali ya hewa nchini. Wizara imeendelea kuvihudumia vyuo hivi kulingana na uwezo wa kifedha. Vyuo vilivyo chini ya Wizara ni Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT), Chuo cha Bahari Dar es Salaam (DMI), Chuo cha Hali ya Hewa Kigoma,  Chuo cha Usafiri wa Anga Dar es Salaam, Chuo Cha Bandari na Chuo Cha Reli Tabora.

Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT)
Mheshimiwa Spika, Chuo Cha Taifa Cha Usafirishaji kilianzishwa mwaka 1975, kama Chuo cha mafunzo chini ya Shirika la Taifa la Usafirishaji kwa lengo la kutoa mafunzo katika sekta ya usafirishaji na uchukuzi.  Mwaka 1982, Chuo kilipanda hadhi na kuwa Chuo Cha Elimu ya Juu, chini ya Wizara ya Mawasiliano na Uchukuzi kupitia sheria ya Bunge Na.24 ya mwaka 1982 na tangazo la Serikali Na. 91 la tarehe 01 Julai, 1983. 
Mheshimiwa Spika, tangu kuanzishwa kwa Chuo mwaka 1975 hadi kufikia Juni 2012, Chuo kimeweza kutoa mafunzo ya muda mrefu kwa jumla ya wataalamu 2,291 wenye sifa za Astashahada, Stashahada na Shahada ya Kwanza katika fani za Menejimenti ya Lojistiki na Usafirishaji, Kupokea na Kupeleka Shehena, Uhandisi wa Magari, Ukaguzi wa Magari na Teknolojia ya Habari na Mawasiliano. Pia katika kipindi hicho, jumla ya wataalamu 29,542 walihudhuria na kuhitimu mafunzo ya muda mfupi ya ueledi wa matumizi ya vyombo vya moto vinavyotumia barabara na usalama wake.
Mheshimiwa Spika, katika jitihada za kuboresha usalama  barabarani, Wizara ya Uchukuzi inafanya mazungumzo na Wizara ya Viwanda na Biashara ili jukumu la kukagua magari yaliyotumika (used vehicles) yanayoingia nchini lifanywe na Chuo Cha Taifa Cha Usafirishaji. Chuo tayari kimepokea msaada wa seti nne (4)  za vifaa vya kisasa vya ukaguzi wa magari kutoka Benki ya Dunia. Vifaa hivyo vina uwezo wa  kukagua magari  800 kwa siku. Chuo pia kiliendelea na ujenzi wa Kituo Cha Rasilimali Mafunzo (Learning Resource Centre), jengo la ghorofa sita lenye ukubwa wa mita za mraba  9,648. 
Mheshimiwa Spika, ili kukabiliana na upungufu mkubwa wa wataalam katika sekta ya uchukuzi, Chuo katika mwaka wa masomo 2011/2012, kilianzisha kozi mpya tano  (5) katika ngazi ya Stashahada ya Uzamili (Post-Graduate Diploma) ikiwa ni katika hatua ya maandalizi ya kuanzisha shahada za Uzamili katika fani zifuatazo: ''Procurement and Logistics Management'', ''Logistics and Transport Management'', ''Port and Shipping Management'', ''Air Transport Management'', na ''Travel and Tourism Management''. 
Mheshimiwa Spika, katika kukabiliana na changamoto ya upungufu wa wataalamu wa usafiri wa anga, Chuo kinatarajia kuanzisha kozi za marubani na mafundi wa ndege katika Viwanja vya ndege vya Tanga na Dodoma. Chuo pia kitaendesha kozi za wahudumu wa ndege kwa lengo la kuboresha huduma zitolewazo katika ndege. Mafunzo hayo yatatolewa kwa wanafunzi kwa kuzingatia sifa mbalimbali ikiwa ni pamoja na elimu ya kidato cha nne au sita, wenye uwezo wa kuongea kwa ufasaha lugha ya Kiswahili na Kiingereza na sifa za urembo au utanashati zinazotambulika na vyombo husika. Aidha, Chuo kimepanga kufanya tafiti, ushauri elekezi na kutoa machapisho katika sekta ya uchukuzi na usafirishaji. Vile vile, Chuo kitaendelea na ujenzi wa jengo la Kituo Cha Rasilimali Mafunzo na kukarabati majengo ili kuboresha mazingira ya kufundishia na kujifunzia.
Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2012/2013, Chuo kimepanga kuinua kiwango cha ubora wa taaluma itolewayo, kwa kuhuisha mitaala ili kukidhi taratibu za ithibati zilizowekwa na Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi (NACTE), kuanzisha kozi mpya tano (5), tatu (3) katika ngazi ya Stashahada ya Uzamili (Post-Graduate Diploma) ambazo ni “Post-Graduate Diploma in Railway Transport Management, Transport Economics” na “Road Safety”, moja (1)  katika ngazi ya Shahada ya kwanza yaani “Bachelor of Science in Transportation Engineering” pamoja na kozi za mafundi wa ndege, na kuongeza udahili wa wanafunzi wa kozi za muda mrefu kwa asilimia 80 kutoka wanafunzi 393 katika mwaka 2011/2012 hadi wanafunzi 700. Aidha, Chuo kimepanga kufanya tafiti elekezi na kutoa machapisho katika sekta ya uchukuzi na usafirishaji. 
Chuo cha Bahari Dar es Salaam (DMI)
Mheshimiwa Spika, Tanzania imebahatika kuwa na ukanda mrefu wa Bahari ya Hindi wenye urefu wa kilometa 800. Aidha, Tanzania pia inamiliki sehemu kubwa ya Ziwa Victoria, Ziwa Tanganyika na Ziwa Nyasa. Kutokana na jiografia hii nchi yetu ina hadhi ya “Maritime State”. Kwa kutambua umuhimu wa sekta ya Bahari kwenye kuchangia uchumi wa Taifa letu, Wizara ilianzisha Chuo cha Bahari kwa sheria ya Bunge Na.21 ya mwaka 1991 ili kiweze kutoa mafunzo kwa wataalamu mbalimbali katika sekta. Tangu kuanzishwa kwake, Chuo kimedahili jumla ya wanafunzi 37,822 wa kozi fupi na ndefu na ambao wameajiriwa katika sekta ya bahari ndani na nje ya nchi. Kwa mwaka 2011/2012 pekee, Chuo kimedahili jumla ya wanafunzi 6,227.
Mheshimiwa Spika, Chuo kimeweza kuongeza wigo wa mafunzo kwa maafisa wa ngazi zote za ubaharia na kinatarajia kutoa mafunzo kwa wataalamu wa sekta ya bahari kwa ngazi ya shahada. Aidha, ili kukidhi ongezeko la mahitaji ya wataalamu katika sekta, Chuo kiliingia makubaliano na Chuo Kikuu cha Bahari cha Dalian (Dalian Maritime University) cha Jamhuri ya Watu wa China mwaka 2007. Pamoja na makubaliano hayo, Chuo Kikuu cha Bahari cha Dalian kimekubali kujenga tawi lake ndani ya Chuo cha Bahari DMI ili kuharakisha upatikanaji wa vitendea kazi na majengo, madarasa, maabara, ofisi, na kumbi za mikutano (auditorium). Napenda kutoa pongezi na shukrani zangu za dhati kwa niaba ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa Serikali ya Jamhuri ya Watu wa China kuruhusu Chuo Kikuu cha Bahari cha Dalian kujenga tawi lake ndani ya Chuo cha Bahari cha DMI. Pia napenda kutoa shukrani zangu kwa Sekta binafsi (Tanzania Private Sector Foundation) kwa kukiwezesha Chuo kupata vitendea kazi vyenye thamani ya Dola za Kimarekani 1,300,000. Tunawaomba na wadau wengine pia wajitokeze kuchangia taasisi za mafunzo.
Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2011/2012, Chuo cha DMI kimepata ithibati (accreditation) kutoka NACTE na pia kimetunukiwa hadhi ya ubora na kuwa ‘Centre of Excellence’ na Jumuiya ya Afrika ya Mashariki katika taaluma ya mafunzo ya sekta ya bahari katika ukanda wa Afrika Mashariki. Chuo kimetunukiwa heshima nyingine na Shirika la Kimataifa linaloratibu usafiri wa majini (International Maritime Organisation) na kuwa kwenye hadhi ya vyuo vinavyotambulika (white list).  Aidha, kutokana na uwezo wa kitaalamu, IMO imekiteua Chuo cha Bahari kuendesha mafunzo ya kuwaandaa wapambanaji dhidi ya uharamia (Piracy) katika Bahari ya Hindi yanayotekelezwa chini ya makubaliano ya Djibouti (Djibouti Code of Conduct 2009).
Mheshimiwa Spika, kwa kuzingatia umuhimu wa sekta ya bahari kwenye kuchangia uchumi wa Taifa letu na ukuaji wa Chuo cha Bahari, Wizara kwa kushirikiana na wadau wengine imekipatia Chuo eneo kilipo hivi sasa na tayari  kimepata hati miliki ya eneo hilo. Aidha, Chuo kimepata eneo la ekari mia tano (500) Wilayani Mkuranga kwa madhumuni ya kuanzisha mafunzo ya ukakamavu na nidhamu kazini (Cadetship Training).

Chuo cha Usafiri wa Anga Dar es Salaam
Mhesimiwa Spika, Chuo cha Usafiri wa Anga Dar es Salaam kinaendesha mafunzo kuhusu sekta ya anga katika maeneo ya taaluma za uongozaji ndege, mafundi wa mitambo ya kuongozea ndege, wataalamu wa mawasiliano kwa urukaji (aeronautical information officers) na wataalam wa usalama na upekuzi (aviation security). Chuo kinatoa mafunzo kwa wanafunzi kutoka hapa nchini na pia kutoka nje ya nchi. Katika mwaka 2011/2012, Chuo kimetoa mafunzo kwa wanafunzi 146. Kati ya hao wanafunzi 117 ni Watanzania na 29 ni kutoka nje ya nchi. Chuo kina usajili wa mpango wa mafunzo wa ICAO (TRAINAIR - Plus) na taratibu za kukisajili NACTE zinaendelea. Lengo ni kukamilisha taratibu za usajili katika mwaka 2012/2013 na kukitangaza Chuo ili kuongeza idadi ya wanafunzi kwa asilimia 20. Aidha, mpango wa kukipanua chuo upo katika hatua za awali ambapo kwa sasa juhudi zinafanyika kwa kushirikiana na uongozi wa Mkoa wa Pwani ili kupata eneo la kutosha kwa ujenzi wa chuo kipya. Lengo ni kukiwezesha chuo hiki kutoa mafunzo katika nyanja mbalimbali za usafiri wa anga.  Mwezi Juni 2012, Chuo cha Usafiri wa Anga Tanzania (CATC) kilitunukiwa cheti cha ubora (ISO 9001:2008) baada ya kukidhi viwango vya ubora vya kimataifa katika utoaji mafunzo. Cheti kama hicho kilitolewa kwa Mamlaka ya Usafiri wa Anga mwezi Novemba 2011 kutokana na ubora wa huduma zake. 
Chuo cha Hali ya Hewa Kigoma
Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2011/2012, Wizara kupitia Mamlaka ya Hali ya Hewa imeendelea kuhudumia Chuo cha Hali ya Hewa Kigoma. Katika kipindi hicho, wanafunzi 45 walimaliza mafunzo na kupangiwa kazi katika vituo mbalimbali vya hali ya hewa hapa nchini. Wanafunzi 39 walianza masomo ya hali ya hewa katika ngazi ya awali (Meteorological Technician Mid-Level) tarehe 7 Machi 2012 na wengine 28 katika ngazi ya kati (Meteorological Technician Senior Level) na wanatarajiwa kuhitimu masomo yao ifikapo Desemba 2012. Aidha, Chuo kimeongezewa walimu wawili ili kuendelea kujenga uwezo katika utoaji wa mafunzo ya hali ya hewa. Katika mwaka 2012/2013, Chuo kitaendelea kutoa mafunzo ya awali na ya kati katika fani ya hali ya hewa, kutoa mafunzo kwa wafanyakazi ndani na nje ya nchi kwa nia ya kuwaongezea uwezo na kuendelea kufuatilia mahitaji ya kupata usajili wa NACTE. 
Chuo cha Bandari Dar es Salaam
Mheshimiwa Spika, Chuo cha Bandari Dar es Salaam kiko chini ya Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA) na kimeanzishwa kwa ajili ya kutoa elimu ya masuala ya Bandari. Aidha, kwa kuzingatia miongozo inayotolewa na NACTE, Chuo hiki kimeendelea kutoa mafunzo ya kuwaendeleza wafanyakazi wa Mamlaka ya Bandari katika fani zote za shughuli za Bandari ili kuongeza tija na ufanisi ikiwa ni pamoja na kutoa huduma za ushauri (Consultancy) na kuendesha kozi fupi za jioni. Katika kipindi cha mwaka wa fedha 2011/2012, jumla ya wanafunzi 2,150 walihitimu mafunzo mbalimbali na inatarajiwa katika mwaka wa fedha 2012/2013, kitahitimisha wanafunzi 2,300. 
Mheshimiwa Spika, Katika kipindi cha mwaka wa fedha 2012/2013, Mamlaka imepanga mikakati ya kuendeleza chuo ikiwa ni pamoja na kukipa vifaa bora na vya kisasa kwa ajili ya kufundishia na kuboresha elimu ya wakufunzi kwa asilimia 50 kufikia kiwango cha Shahada ya Uzamili (Masters Degree). Mikakati mingine ni kukarabati madarasa na ofisi za Chuo. Aidha, Chuo kitapitia, kuboresha, kuendeleza na kutekeleza mitaala inayokidhi mahitaji ya sekta ya bandari kwa viwango vya Kimataifa. Changamoto inayoikabili Chuo kwa sasa ni ukosefu wa majengo na eneo la mafunzo kwa vitendo.
Chuo cha Reli Tabora
Mheshimiwa Spika, Chuo cha Reli Tabora kilianzishwa mwaka 1947 kwa lengo la kutoa mafunzo ya ukarani. Baada ya Jumuiya ya Afrika Mashariki kuvunjika, Chuo kiliboreshwa ili kuweza kutoa mafunzo ya “Station Masters”, Udereva wa treni, Ishara na Mawasiliano na “Train Guards”. Chuo kiliendelea kupanuka kwa kufungua tawi la Morogoro kwa ajili ya kuendesha mafunzo ya udereva wa treni.
Mheshimiwa Spika, utendaji wa Chuo ulishuka kufuatia zoezi la ubinafsishaji wa Shirika la Reli Tanzania (TRC) mwaka 1997 na kufuatiwa na zoezi la kupunguza wafanyakazi (Retrenchment) lililofanyika mwaka 2007. Kwa sasa Chuo kina wakufunzi sita. Kati ya hao, wanne wako katika Chuo cha Reli Tabora na wawili wako katika tawi la Morogoro. Jumla ya wakufunzi 16 wanahitajika katika Chuo cha Reli Tabora na tawi la Morogoro. Kwa sasa hivi Chuo kinatumia wataalam walioko TRL kama wakufunzi wa muda (part-time) ili kuziba pengo lililopo.
Mheshimiwa Spika, katika kipindi cha mwaka 2011/2012 chuo kiliendesha kozi mbili za “Station Masters” na “Train Guards”. Kozi ya “Train Guards” ilianza mwezi Mei 2011 ikiwa na wanafunzi 23 na kukamilika mwezi Aprili 2012. Aidha, kozi ya “Station Masters” ilianza mwezi Mei 2011 ikiwa na wanafunzi 17 na kukamilika Aprili 2012. Kwa mwaka 2012/2013, Chuo kimepanga kuendesha mafunzo ya “Station Masters”, Ukaguzi wa njia ya reli, Madereva wa treni pamoja na “Train Guards”.

E. USHIRIKI KATIKA JUMUIYA MBALIMBALI  

Ushiriki Katika Jumuiya Ya Afrika Ya Mashariki (EAC) 
Mheshimiwa Spika, Wizara imeendelea kushiriki kwenye mikutano mbalimbali ya Jumuiya ya Afrika Mashariki. Katika ushirikiano huu, Jumuiya imekamilisha mkakati wa kuendeleza sekta ya uchukuzi (EAC Transport strategy and road development). Katika mkakati huu miradi mbalimbali imeainishwa kwa ajili ya utekelezaji. Miradi hii ni pamoja na ile inayounganisha nchi wanachama wa Jumuiya na ndani ya nchi kwa nia ya kurahisisha ufanyaji biashara katika Jumuiya. Miradi hiyo inajumuisha reli, bandari, usafiri wa anga,  usafiri wa majini, barabara na vituo vya mipakani. 
Mheshimiwa Spika, Tanzania kama nchi mwanachama wa Jumuiya imeshiriki katika mikutano ya kuondoa vikwazo visivyo vya kiforodha (Non Tariff Barriers –NTB) ili kurahisisha uchukuzi na biashara miongoni mwa nchi wanachama. Maeneo yenye vikwazo visivyo vya kiforodha ni pamoja na taasisi nyingi kujihusisha na kupima ubora wa bidhaa. Katika kusimamia suala hili Jumuiya imeanza kufanya utafiti kuhusu utaratibu wa kisheria wa kusimamia uondoshwaji wa vikwazo visivyo vya kiforodha. 
Mheshimiwa Spika, kuhusu usafiri wa reli, nchi wanachama wameandaa Mpango Kabambe wa uendelezaji wa reli (The East African Railway Master Plan). Kazi inayoendelea ni maandalizi ya mwongozo wa kisheria na kiutendaji kuhusu ushirikishwaji wa Sekta binafsi (Public Private Partnerships - PPPs) utakaosaidia kuendeleza reli za kikanda.
Mheshimiwa Spika, kwa upande wa usafiri majini, Tanzania imeendelea kushirikiana na nchi nyingine wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki katika kupambana na vitendo vya kiharamia katika Bahari ya Hindi kwa kushirikiana na Shirika la Kimataifa linalosimamia Usafiri Majini (IMO), Umoja wa Afrika (AU), Mamlaka ya Maendeleo ya Nchi za Kanda ya Mashariki (Intergovernmental Authority on Development-IGAD) pamoja na kuandaa makubaliano ya ushirikiano wa kupambana na kuzuia vitendo vya kiharamia. Aidha, imekubaliwa kuwa Kituo cha Utafutaji na Uokoaji katika maziwa kijengwe mkoani Mwanza. 

Ushiriki katika Jumuiya ya Nchi za Kusini mwa Afrika (SADC)
Mheshimiwa Spika, Wizara ina jukumu la kuendeleza Miundombinu ya Uchukuzi nchini ili kuweza kuiunganisha nchi yetu na Nchi Wanachama wa SADC. Kwa sasa Nchi Wanachama wa SADC wanaendelea kukamilisha Mpango Kabambe wa Uendelezaji wa Miundombinu (Regional Infrastructure Development Master Plan–RIDMP). Mshauri Mwelekezi amekamilisha rasimu ya taarifa ya Mpango huo. Taarifa hiyo imejadiliwa na kupitishwa na Kikao cha Baraza la Mawaziri wa Uchukuzi wa Nchi Wanachama kilichofanyika Angola mwezi Juni 2012. Wizara iliwasilisha miradi mbalimbali ambayo imejumuishwa katika mpango huo. Miradi hiyo inahusu reli, bandari, viwanja vya ndege, na hali ya hewa. 
Mheshimiwa Spika, Hivi sasa Jumuiya mbili za EAC na SADC zimeanzisha eneo huru la kibiashara kwa ushirikiano na COMESA. Lengo la ushirikiano huu ni kurahisisha ufanyaji biashara kwa kuoanisha taratibu za kibiashara na usafiri katika Jumuiya hizi tatu ikiwa ni pamoja na kuendeleza miundombinu ya usafiri wa majini, anga na reli na huduma za hali ya hewa.
F. MASUALA MTAMBUKA 

Utunzaji wa Mazingira
Mheshimiwa Spika, Utunzaji wa mazingira ya uchukuzi ni muhimu katika kuimarisha huduma na miundombinu ya uchukuzi nchini. Wizara imeendelea kuhakikisha kuwa utekelezaji wa miradi ya maendeleo na utoaji wa huduma za uchukuzi zinazohusika na Bandari, Viwanja vya Ndege, barabara na Reli unazingatia Sheria, Kanuni, taratibu na Mikataba ya Kimataifa ya Uhifadhi wa mazingira ambayo nchi yetu ni mwanachama. 
Mheshimiwa Spika, Katika mwaka wa 2011/2012, Wizara yangu imeweza kutekeleza mambo mbalimbali yanayolenga kuimarisha usalama na uhifadhi wa mazingira ya uchukuzi majini. Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni mwanachama wa Mradi wa kukabiliana na umwagikaji wa mafuta kutoka kwenye meli katika Bahari ya Hindi (GEF – Western Indian Ocean Marine Highway Development and Marine Contamination Prevention – WIOMHP). Mradi huu unasimamiwa na Kamisheni ya Bahari ya Hindi (Indian Ocean Commission – IOC). Katika kutekeleza mradi huo, Kamisheni ya Bahari ya Hindi imetoa msaada wa vifaa vya kukabiliana na umwagikaji wa mafuta baharini vyenye thamani inayofikia shilingi milioni 190. Baadhi ya vifaa hivi ni pamoja na: Matanki ya kukusanyia mafuta, mipira ya kuzuia mafuta yasienee baharini, mipira ya kupeleka mafuta nje ya bahari, pampu na vinyonya mafuta.
Mheshimiwa Spika, Wizara pia imeandaa rasimu ya Mpango wa Taifa wa kukabiliana na matukio/majanga ya kumwagika mafuta baharini (The National Oil spill Response Contigency Plan) na Mpango wa Taifa wa kukabiliana na matukio/majanga ya kumwagika sumu au shehena hatari baharini (the National Hazardous and Noxious substances Response Contigency Plan). Taifa letu litafaidika na kuwepo kwa mipango hii ili kujiandaa vema na majanga yanayoweza kujitokeza kutokana na mwambao wa Tanzania kuwa karibu na njia kuu (Mozambique channel) ya meli zinazobeba kiasi kikubwa cha mafuta na shehena hatarishi kwa mazingira ambapo tishio la kumwagika mafuta au shehena za hatari linaweza kujitokeza.
Mheshimiwa Spika, miaka ya hivi karibuni utafiti umeonyesha kuwa katika mwambao wa bahari wa nchi yetu kuna kiasi kikubwa cha gesi na mafuta. Hivyo, kumekuwepo na alama mbalimbali zisizohamishika zilizosimikwa baharini kuonyesha mahali ilipo miundombinu ya utafutaji na uchimbaji wa mafuta na gesi. Pamoja na baraka hizo, nchi yetu imekuwa kwenye mapambano makubwa dhidi ya vitendo viovu vya magaidi na maharamia wanaoshambulia meli zinazoleta biashara ya kimataifa kwenye bandari zetu au kupita kwenye mwambao wetu. Uzoefu kutoka nchi zilizoendelea unaonyesha kuwa magaidi na maharamia hao wanaweza kushambulia alama hizi. Hivyo, ili nchi yetu iweze kulinda usalama wa uchukuzi baharini, kuhifadhi mazingira ya bahari na kukabiliana na vitendo viovu dhidi ya alama zisizohamishika zilizosimikwa baharini, Wizara yangu inaendelea na taratibu za kuridhia Itifaki ya Kimataifa kuhusu namna ya kukabiliana na vitendo viovu dhidi ya alama zilizosimikwa baharini ya mwaka 1988. 
Mheshimiwa Spika, uhifadhi na utunzaji wa mazingira katika huduma za uchukuzi wa Reli na barabara ni moja ya changamoto kubwa inayoikabili Wizara yangu. Changamoto hizo ni pamoja na msongamano mkubwa wa vyombo vya uchukuzi hasa  mijini ambao umesababisha kuwepo kwa kelele nyingi, moshi, utupaji ovyo wa mabaki ya mafuta na vilainisha mitambo, taka ngumu na laini na uchafu mwingine unaoathiri afya za binadamu, mimea na wanyama. Wananchi wamekuwa wakifanya shughuli za kijamii kwenye hifadhi ya miundombinu ya uchukuzi kama kulima, kuchoma moto kwa ajili ya shughuli za uwindaji, kukata miti, kujenga nyumba na kufanya biashara katika maeneo ya hifadhi ya miundombinu. Kila mwaka, Serikali imekuwa ikitumia fedha nyingi kukarabati maeneo ya reli, barabara, fukwe na viwanja vya ndege yaliyoharibiwa kutokana na shughuli za binadamu. Napenda kutoa rai kwa wananchi wanaoishi na kufanya shughuli zao katika maeneo haya waache vitendo hivi ili kulinda miundombinu hii muhimu kwa manufaa ya Taifa letu. 
Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2012/2013, Wizara imejipanga kuleta katika Bunge lako Tukufu miswada na Itifaki zilizotajwa hapo juu kwa ajili ya kupata kibali na kukamilisha mipango ya kitaifa niliyoitaja. Aidha, kanuni mbalimbali kuhusu uhifadhi wa mazingira katika kuimarisha huduma na miundombinu ya uchukuzi zitaandaliwa. Wizara imejipanga kuanza kutoa elimu kwa umma kuhusu umuhimu wa utunzaji wa mazingira kwenye maeneo ya hifadhi ya miundombinu ya uchukuzi na kwenye huduma za uchukuzi. Elimu itakayotolewa ni pamoja na kufanya mikutano na wananchi wa sehemu husika, matangazo ya kwenye redio na luninga na kuandaa vipeperushi.  
Udhibiti wa UKIMWI 
Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2011/2012, Wizara iliunda Kamati ya kushughulikia masuala ya UKIMWI. Aidha, ilifanya mkutano na wadau wa Sekta ya Uchukuzi kuhusu namna ya kujikinga na maambukizi ya virusi vya UKIMWI. Katika mwaka 2012/2013, Wizara imepanga kuendesha semina mbalimbali kwa watumishi kuhusu ugonjwa wa UKIMWI na pia kuwahamasisha watumishi wote wa Wizara kupima afya zao kwa hiari na kuwasaidia watakaokuwa wameathirika kwa kuwapatia lishe bora. 

Mapambano dhidi ya rushwa 
Mheshimiwa Spika, pamoja na juhudi zinazoendelea kupambana na rushwa, suala hili bado linaendelea kuathiri jamii yetu. Katika kipindi cha 2011/2012, Wizara iliweza kuendesha semina mbalimbali ambapo tatizo la rushwa lilijadiliwa na kuwekewa mikakati ya kupambana nalo ikiwa ni pamoja na kuwashawishi wafanyakazi kutoshiriki vitendo vya kutoa au kupokea rushwa. Juhudi hizi zilifanyika kwa kushirikiana na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa. 

Habari, Elimu na Mawasiliano
Mheshimiwa Spika, matumizi ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano imeongeza na kurahisisha kwa kiasi kikubwa ufanisi na utendaji wa sekta mbalimbali za kiuchumi na kijamii. Wizara imeitikia wito wa matumizi ya Serikali–Mtandao kama njia mojawapo ya mawasiliano kwa shughuli za Kiserikali ikiwa ni pamoja na matumizi ya barua pepe za kiofisi na matumizi sahihi ya Kompyuta. Katika mwaka 2011/2012, Wizara iliendelea kutoa Elimu kwa Umma juu ya shughuli mbalimbali zinazotekelezwa na Wizara. Moja ya tukio kubwa na ambalo lilitumika kueleza historia ya Sekta ya Uchukuzi ni lile la Maadhimisho ya miaka 50 ya uhuru wa Tanzania Bara. Makala yenye ujumbe mbalimbali yaliandaliwa kupitia vyombo vya habari, mabango, vipeperushi na majukwaa kwa lengo la kuelimisha umma kuhusu tulikotoka, maendeleo yaliyopatikana, changamoto zilizopo na namna tunavyokabiliana nazo katika Sekta ya Uchukuzi.
Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2012/2013 Wizara itaendelea kuhamasisha matumizi sahihi ya Serikali-Mtandao na kuelemisha umma kupitia tovuti yake yenye anwani  HYPERLINK "http://www.mot.go.tz" www.mot.go.tz. Aidha, Wizara itatumia Mkakati wake wa Mawasiliano kuongeza wigo wa kujitangaza zaidi ili umma wa Watanzania ujue kazi mbalimbali za uchukuzi zinazofanyika kwa maendeleo ya Taifa letu. 

G. SHUKRANI 
Mheshimiwa Spika, napenda kutoa shukrani za dhati kwa wadau wote wa Sekta ya Uchukuzi na Hali ya Hewa ikiwemo sekta binafsi kwa ushirikiano wao katika kutimiza malengo yetu. Kwa namna ya pekee naomba kutambua mchango wa M/S Said Salim Bakhresa, East African Rail Hauliers, CRDB, na TIB kwa michango yao katika maendeleo ya Uchukuzi. Shukrani zetu pia ziwaendee Washirika wetu wa maendeleo katika kutekeleza programu na mipango yetu ya Sekta. Washirika hao ni pamoja na Mashirika ya Kimataifa na Taasisi za Kimataifa zinazochangia katika kuboresha utoaji huduma na miundombinu ya sekta zetu. Nchi na mashirika hayo ni pamoja na Shirika la Kimataifa la Usafiri wa Majini (IMO), Shirika la Kimataifa la Usafiri wa Anga (ICAO), Shirika la Hali ya Hewa Duniani (WMO), UNESCO, Benki ya Dunia (WB), Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB), Benki ya Kiarabu ya Maendeleo ya Afrika (BADEA), Kuwait Fund, Jamhuri ya Korea, OPEC Fund, Umoja wa Nchi za Ulaya, Afrika Kusini, Uingereza, Marekani, Uholanzi, Japan, European Investment Bank(EIB), India, China, Denmark, Norway, Ubelgiji, Ujerumani, Urusi, Sweden, Ufaransa, Finland, Singapore na wengine wengi. Tunaomba waendelee kushirikiana nasi katika kuimarisha Sekta yetu na kufanikisha malengo yetu.
Mheshimiwa Spika, napenda kuishukuru tena Kamati ya Bunge ya Miundombinu na Waheshimiwa Wabunge  wa Bunge lako Tukufu kwa michango na ushirikiano waliotupa katika kuboresha huduma zitolewazo na Wizara.
Mheshimiwa Spika, napenda kutoa shukrani za dhati kwa viongozi wenzangu katika Wizara kwa ushirikiano wanaonipa wakati wa kutekeleza majukumu yangu ya kila siku. Shukrani hizi ziende kwa Naibu Waziri, Mhe. Dkt. Charles John Tizeba (Mb.), Katibu Mkuu Mhandisi Omar Abdallah Chambo, Naibu Katibu Mkuu, Ndg. John Thomas Mngodo, Wakuu wa Idara, Wakuu wa Vitengo, Viongozi wa Taasisi zilizo chini ya Wizara pamoja na watumishi wote wa Wizara na Taasisi. Na mimi naahidi kushirikiana nao bega kwa bega katika kuendeleza, kuboresha miundombinu na huduma za uchukuzi na hali ya hewa hapa nchini. Nawashukuru sana.  

H. MAOMBI YA FEDHA
Mheshimiwa Spika ili Wizara iweze kutekeleza majukumu na malengo yake katika mwaka wa fedha 2012/2013, naomba Bunge lako tukufu liidhinishe jumla ya shilingi 317,710,481,000. Kati ya fedha hizo, shilingi 64,952,351,000 ni kwa Matumizi ya Kawaida na shilingi 252,758,130,000 ni kwa ajili ya Miradi ya Maendeleo. Fedha za Matumizi ya Kawaida zinajumuisha shilingi 37,062,651,000 za mishahara ya watumishi na shilingi 27,889,700,000 fedha za Matumizi Mengineyo (OC). Fedha za Miradi ya Maendeleo zinajumuisha shilingi 189,780,000,000 fedha za ndani na shilingi 62,978,130,000 fedha za nje.
Mheshimiwa Spika, napenda kwa mara nyingine nitoe shukurani zangu za dhati kwako binafsi na kwa Waheshimiwa Wabunge kwa kunisikiliza. Hotuba hii inapatikana pia katika tovuti ya Wizara kwa anuani ya:  HYPERLINK "http://www.mot.go.tz" www.mot.go.tz.
Mheshimiwa Spika, pamoja na hotuba, jedwali la miradi yote itakayotekelezwa katika mwaka 2012/2013 pamoja na kiasi cha fedha kilichotengwa kutekeleza miradi hiyo imeoneshwa katika Kiambatisho Na.1. Naomba Kiambatisho hicho kichukuliwe kama sehemu ya hoja hii. 
Mheshimiwa Spika, naomba kutoa hoja.

78 comments:

Anonymous said...

Thank you for another wonderful article. The place else may anybody get that type
of info in such a perfect manner of writing? I have a presentation next
week, and I am on the search for such information.
Also see my web page :: cigarettes online

Anonymous said...

My brother suggested I might like this website. He was entirely right.
This post actually made my day. You can not imagine simply how much time I had spent for this info!
Thanks!
Have a look at my site - make money online for free

Anonymous said...

It's perfect time to make a few plans for the long run and it is time to be happy. I have read this post and if I may just I wish to counsel you few fascinating things or suggestions. Maybe you can write subsequent articles referring to this article. I want to read more issues about it!
Check out my web page :: best acne treatment for women

Anonymous said...

I every time used to read post in news papers but now as I
am a user of internet therefore from now I am using net for articles, thanks to web.
Feel free to surf my web site :: 11isfree.com

Anonymous said...

Greetings! I know this is kinda off topic but I was wondering which blog platform are you using for this website?
I'm getting sick and tired of Wordpress because I've had problems with
hackers and I'm looking at alternatives for another platform. I would be awesome if you could point me in the direction of a good platform.

Feel free to visit my blog Plumbing And Bathrooms Gauteng

Anonymous said...

Greetings! Very useful advice in this particular article!

It is the little changes that make the greatest changes.

Many thanks for sharing!

Look into my web site ... fat loss South Africa

Anonymous said...

Hey! I could have sworn I've been to this site before but after reading through some of the post I realized it's new to me.
Anyhow, I'm definitely delighted I found it and I'll be bookmarking and checking back often!


Also visit my web page ... cosmetic jewelry KwaZulu Natal health care products KwaZulu Natal

Anonymous said...

Thanks very nice blog!

Feel free to visit my weblog - herbalife food supplements Johannesburg

Anonymous said...

Hello, yeah this piece of writing is actually pleasant and I have learned lot of things from it
regarding blogging. thanks.

Have a look at my weblog :: collapsible gas cylinder cages Gauteng collapsible gas cylinder cages Gauteng

Anonymous said...

I have read several good stuff here. Certainly worth bookmarking for revisiting.
I wonder how a lot effort you put to create the
sort of excellent informative site.

Also visit my site :: Reservation software Durban

Anonymous said...

Hello there! I could have sworn I've been to this blog before but after checking through some of the post I realized it's new to me.
Nonetheless, I'm definitely glad I found it and I'll be bookmarking and checking back frequently!


My page house removals Cape Town

Anonymous said...

Howdy, i read your blog from time to time and i own a similar one and i was just wondering if you get a lot of spam responses?
If so how do you stop it, any plugin or anything you can recommend?
I get so much lately it's driving me mad so any help is very much appreciated.

my webpage :: plumbing and maintenance Randburg

Anonymous said...

I believe this is one of the so much significant information for me.
And i'm happy studying your article. However want to observation on few common things, The site style is ideal, the articles is in point of fact nice : D. Good job, cheers

Stop by my website: More info

Anonymous said...

Hey There. I found your blog using msn. This is an extremely well written article.
I will make sure to bookmark it and return to read more of your useful info.
Thanks for the post. I will definitely comeback.


Visit my homepage - office recycling Century City

Anonymous said...

Hi there, just wanted to tell you, I loved this post. It was inspiring.
Keep on posting!

my blog post: click here

Anonymous said...

Awesome post.

Look into my web blog: Infromtion Site

Anonymous said...

I am sure this post has touched all the internet people, its
really really pleasant paragraph on building up new web site.


Here is my website: More info

Anonymous said...

What i don't realize is actually how you are no longer really a lot more smartly-favored than you may be right now. You are very intelligent. You recognize thus significantly on the subject of this matter, produced me for my part consider it from a lot of numerous angles. Its like women and men aren't involved unless it's something to do with Woman gaga! Your personal stuffs great. At all times care for it up!

my page wedding flowers Gauteng

Anonymous said...

Nice post. I learn something new and challenging on websites I stumbleupon every day.

It's always helpful to read articles from other authors and use a little something from other web sites.

Here is my web blog - visit url

Anonymous said...

Wow that was unusual. I just wrote an very long comment but after I clicked submit my comment didn't appear. Grrrr... well I'm not
writing all that over again. Regardless, just wanted to say excellent blog!



Feel free to visit my website - Visit here

Anonymous said...

I have read so many content regarding the blogger lovers but this piece of writing is in fact a
fastidious article, keep it up.

Also visit my blog post ... dstv services in Cape Town

Anonymous said...

We absolutely love your blog and find nearly all of your post's to be just what I'm looking for.
can you offer guest writers to write content for you? I wouldn't mind creating a post or elaborating on a number of the subjects you write in relation to here. Again, awesome site!

My webpage - large format digital printing South Africa

Anonymous said...

Hello! I just wanted to ask if you ever have any trouble
with hackers? My last blog (wordpress) was hacked and I ended up losing many
months of hard work due to no data backup. Do you have any solutions to stop hackers?



Here is my website - specialised sales Gauteng

Anonymous said...

In fact no matter if someone doesn't understand after that its up to other users that they will assist, so here it takes place.

Here is my web-site - click here

Anonymous said...

First off I want to say fantastic blog! I had a quick question in
which I'd like to ask if you do not mind. I was interested to find out how you center yourself and clear your mind prior to writing. I have had a tough time clearing my thoughts in getting my thoughts out there. I truly do take pleasure in writing but it just seems like the first 10 to 15 minutes tend to be lost just trying to figure out how to begin. Any suggestions or tips? Thanks!

Here is my web blog Visit Website

Anonymous said...

Great post. I was checking continuously this blog and I'm impressed! Extremely helpful information specially the last part :) I care for such information a lot. I was seeking this certain information for a long time. Thank you and good luck.

Feel free to visit my webpage ... corporate gifts South Africa

Anonymous said...

What's up, always i used to check weblog posts here early in the daylight, for the reason that i like to find out more and more.

Here is my web site - party hire Western Cape

Anonymous said...

Can I just say what a comfort to find someone that really knows what they're discussing on the web. You definitely realize how to bring an issue to light and make it important. More and more people ought to check this out and understand this side of your story. I can't
believe you are not more popular because you certainly have the gift.


my web page; mattresses Mpumalanga

Anonymous said...

Hi to every body, it's my first pay a quick visit of this weblog; this blog contains amazing and genuinely fine information designed for readers.

Here is my blog ... website

Anonymous said...

It's actually a nice and helpful piece of information. I'm happy
that you just shared this helpful info with us.
Please keep us up to date like this. Thanks for sharing.

Here is my website ... More info

Anonymous said...

This is a really good tip especially to those fresh to the blogosphere.
Brief but very precise info… Many thanks for sharing this one.
A must read article!

Also visit my homepage ... dyno tuning South Africa

Anonymous said...

I would like to thank you for the efforts you've put in writing this site. I'm hoping to check out the same high-grade content by you later
on as well. In fact, your creative writing abilities has inspired me
to get my own website now ;)

my webpage ... website link

Anonymous said...

I am really loving the theme/design of your weblog. Do
you ever run into any internet browser compatibility issues?

A small number of my blog readers have complained about my blog not operating correctly in Explorer but looks great in Opera.
Do you have any ideas to help fix this problem?

Check out my blog post: exclusive wedding cakes Johannesburg

Anonymous said...

You have made some good points there. I looked on the internet for more info about the
issue and found most people will go along with your views on this web site.



Look at my weblog; suppliers of gym equipment Johannesburg suppliers of gym equipment Johannesburg

Anonymous said...

I always spent my half an hour to read this webpage's content every day along with a mug of coffee.

My blog post ... click url

Anonymous said...

Its like you read my mind! You appear to know a lot about this, like you wrote the book in it or
something. I think that you could do with a few pics to drive the message home
a little bit, but other than that, this is excellent blog.
An excellent read. I will definitely be back.

Take a look at my blog post :: click url

Anonymous said...

Nice blog here! Also your website loads up very fast!
What host are you using? Can I get your affiliate link to your host?
I wish my website loaded up as quickly as yours lol

Anonymous said...

I love your blog.. very nice colors & theme. Did you design this website yourself
or did you hire someone to do it for you?
Plz respond as I'm looking to construct my own blog and would like to find out where u got this from. appreciate it

Feel free to visit my site :: Visit here

Anonymous said...

Howdy just wanted to give you a quick heads up.
The text in your content seem to be running off the screen in Safari.
I'm not sure if this is a format issue or something to do with browser compatibility but I thought I'd post to let
you know. The design and style look great though! Hope you get the issue resolved soon.
Kudos

my homepage :: Visit website

Anonymous said...

I think this is among the most significant info for
me. And i'm glad reading your article. But should remark on some general things, The web site style is perfect, the articles is really great : D. Good job, cheers

My blog post ... Visit here

Anonymous said...

Its like you read my mind! You seem to know a lot about this, like you wrote the book in it or something.
I think that you can do with a few pics to drive the
message home a bit, but other than that, this is fantastic blog.
A fantastic read. I'll certainly be back.

my homepage; IT consulting Johannesburg

Anonymous said...

My brother suggested I might like this blog. He
was entirely right. This post actually made my day.
You cann't imagine simply how much time I had spent for this info! Thanks!

my website :: business of architecture

Anonymous said...

This website definitely has all the information and facts I needed concerning this subject and didn't know who to ask.

Here is my weblog; wedding photography Cape town

Anonymous said...

Wow, superb blog format! How lengthy have you been blogging for?
you make running a blog glance easy. The entire look of your web site is wonderful, let alone the content material!


Check out my web page :: tax And consulting

Anonymous said...

Hey there would you mind letting me know which webhost you're utilizing? I've loaded your blog in 3 completely different internet browsers and I must
say this blog loads a lot faster then most. Can you suggest a good hosting provider at a reasonable price?
Thanks a lot, I appreciate it!

My web blog :: car rentals Johannesburg life style

Anonymous said...

There is certainly a lot to know about this issue.
I really like all of the points you've made.

Feel free to visit my site: conti suits Johannesburg

Anonymous said...

My coder is trying to convince me to move to .net from PHP.
I have always disliked the idea because of the expenses.
But he's tryiong none the less. I've been using WordPress on
several websites for about a year and am anxious about switching to
another platform. I have heard good things about blogengine.
net. Is there a way I can transfer all my wordpress posts into it?
Any kind of help would be greatly appreciated!

Here is my web-site :: office planning and layout

Anonymous said...

Hey there just wanted to give you a quick heads up. The text in your article seem to be running off the screen in Internet explorer.
I'm not sure if this is a format issue or something to do with internet browser compatibility but I thought I'd post to
let you know. The layout look great though! Hope you get the issue solved soon.
Thanks

Feel free to surf to my webpage; click this site

Anonymous said...

Aw, this was a very nice post. Taking a few minutes and actual effort to make a very
good article… but what can I say… I put things off a lot and
don't manage to get nearly anything done.

Have a look at my blog post ... More information

Anonymous said...

Hello there! I simply want to offer you a big thumbs up
for the excellent info you have here on this post.
I am returning to your site for more soon.

Also visit my web-site Click here

Anonymous said...

Today, I went to the beachfront with my kids. I found
a sea shell and gave it to my 4 year old daughter
and said "You can hear the ocean if you put this to your ear." She put the shell to her ear and screamed.
There was a hermit crab inside and it pinched her
ear. She never wants to go back! LoL I know this is entirely off
topic but I had to tell someone!

Stop by my homepage - visit this site

Anonymous said...

It is appropriate time to make some plans for the future and
it is time to be happy. I have read this post and if I could I desire to suggest you some interesting things or
tips. Perhaps you can write next articles referring to this article.

I wish to read more things about it!

Review my webpage ... click this site

Anonymous said...

I was pretty pleased to find this great site. I want to to thank
you for ones time for this particularly wonderful read!
! I definitely savored every little bit of it and i also have you saved as a favorite to see new stuff on your blog.


my site - More information

Anonymous said...

When I originally commented I clicked the "Notify me when new comments are added" checkbox and now each time a
comment is added I get four emails with the same comment.
Is there any way you can remove people from
that service? Thank you!

Anonymous said...

It's appropriate time to make some plans for the future and it's time to be happy.
I've read this post and if I could I wish to suggest
you some interesting things or suggestions. Maybe you can write next articles referring
to this article. I desire to read even more things about it!

Anonymous said...

I don't know whether it's just me or if
perhaps everyone else encountering problems with your site.
It looks like some of the text in your content
are running off the screen. Can someone else please
provide feedback and let me know if this is happening to them too?
This may be a issue with my web browser because I've
had this happen previously. Cheers

Anonymous said...

Wow, this piece of writing is good, my younger sister is analyzing these kinds of things, therefore I am going to convey her.

Anonymous said...

Hey! This is my first visit to your blog! We are a collection of volunteers
and starting a new initiative in a community
in the same niche. Your blog provided us useful information to
work on. You have done a extraordinary job!

Anonymous said...

Hmm it looks like your blog ate my first comment (it was
extremely long) so I guess I'll just sum it up what I had written and
say, I'm thoroughly enjoying your blog. I too am an aspiring blog writer but I'm still new
to everything. Do you have any helpful hints for beginner blog writers?
I'd certainly appreciate it.

Anonymous said...

Greetings! This is my first visit to your blog!

We are a group of volunteers and starting a new initiative in a community in the same niche.

Your blog provided us valuable information to work
on. You have done a marvellous job!

Anonymous said...

Thank you for sharing your thoughts. I truly
appreciate your efforts and I am waiting for your next write ups thank you once again.

Anonymous said...

Does your website have a contact page? I'm having trouble locating it but, I'd like to send
you an email. I've got some creative ideas for your blog you might be
interested in hearing. Either way, great website and I look forward
to seeing it grow over time.

Anonymous said...

For newest information you have to go to see internet and on internet I
found this site as a most excellent web site for
most up-to-date updates.

Anonymous said...

Hello, i think that i saw you visited my web site thus i came to “return the
favor”.I am attempting to find things to improve my site!I suppose its ok to use a few of your ideas!!

Anonymous said...

After exploring a handful of the blog posts on your website, I really appreciate your technique of writing a
blog. I saved it to my bookmark site list and will be checking back soon. Please check out my web site too and let me know
your opinion.

Anonymous said...

Wow, awesome blog layout! How long have you been blogging for?
you made blogging look easy. The overall look of your website is excellent,
let alone the content!

Anonymous said...

I'm extremely pleased to find this web site. I need to to thank you for your time just for this fantastic read!!
I definitely enjoyed every part of it and I have you bookmarked to see new things on your web site.

Anonymous said...

Good day! This is kind of off topic but I need some advice from an established blog.
Is it very hard to set up your own blog? I'm not very techincal but I can figure things out pretty fast.
I'm thinking about setting up my own but I'm not
sure where to begin. Do you have any ideas or suggestions?

Thank you

Anonymous said...

Attractive section of content. I just stumbled upon your site and in accession capital to assert that I get
actually enjoyed account your blog posts. Anyway I'll
be subscribing to your augment and even I achievement you access consistently fast.

Anonymous said...

We are a group of volunteers and opening a new scheme in our community.
Your web site offered us with valuable info to work on. You've
done an impressive job and our entire community will be thankful to
you.

Anonymous said...

When I initially commented I clicked the "Notify me when new comments are added" checkbox and now each time
a comment is added I get four emails with the same comment.

Is there any way you can remove people from that service?
Appreciate it!

Anonymous said...

It's awesome to go to see this web page and reading the views of all friends on the topic of this piece of writing, while I am also zealous of getting knowledge.

Anonymous said...

Write more, thats all I have to say. Literally, it seems as though you relied on the
video to make your point. You obviously know what youre talking about, why waste your
intelligence on just posting videos to your blog when you could be
giving us something enlightening to read?

Anonymous said...

Howdy just wanted to give you a quick heads
up and let you know a few of the picxtures aren't loading properly.
I'm not sure why buut I think its a linking issue. I've tried it in two different internet browsers and botth show the same outcome.

Anonymous said...

Pretty great post. I simply stumbled upon your weblog and wanted to say
that I've truly enjoyed browsing your weblog posts.
After all I'll be subscribing on your feed and I hope you write
again soon!

Anonymous said...

No matter if some one searches for his vital thing,
so he/she wants to be available that in detail, thus that thing is maintained over here.

Anonymous said...

Piece of writing writing is also a excitement, if you be familiar with afterward you can write or else it is complicated to write.

Anonymous said...

Spot on with this write-up, I seriously believe that this website
needs a great deal more attention. I'll probably be returning to read through more, thanks for the advice!