2014年1月22日水曜日

MZAHA WA LEO...

Tarehe huwa zinavutia sana hasa kwa wale wanaokuwa ofisini. Utasikia: "Mi nina hamu kweli ya matembele."
Mwingine atadakia: "We acha tu, halafu upate na dagaa wako uchanganye na nyanya chungu, mbona unaweza kumaliza ugali kilo nzima!" Halafu mwingine naye utasikia: "Halafu ugali wenye uwe wa dona, utakoma!" Swali linakuja: Hivi ni kweli wafanyakazi hasa waajiriwa tarehe hizi za mwanzoni mwa mwaka huwa hawana hamu ya vyakula vizuri, mfano Chips, ndizi za kuchoma, soseji au nyama choma? Kazi kwako....

0 件のコメント: