Safari
ya mwisho ya mtoto Nasra Mvungi (4), iliyokuwa ya mateso hapa duniani, imefikia
mwisho jana katika makaburi ya Kola, Manispaa ya Morogoro, bila kusindikizwa na
baba yake mzazi, Rashid Mvungi.
Nasra
kwa zaidi ya miaka mitatu hapa duniani, inadaiwa alikuwa akiishi katika boksi
lililokuwa kitanda, choo, sehemu ya kuchezea na meza yake ya kulia chakula.
Mvungi
alishiriki kwenda jijini Dar es Salaam kuchukua mwili wa mwanawe, na hata jana
wakati wa kutoa mwili katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Morogoro kwenda
kumwosha msikitini, alikuwepo.
Baada
ya hapo mwili ulipelekwa uwanja wa Jamuhuri, ambako Mvungi wakati wote alikuwa
ameketi mstari wa mbele ya jeneza la mwanawe. Uwanjani hapo nasaha mbalimbali
za viongozi wa Serikali na wale wa dini zilitolewa mbele yake.
Baada
ya nasaha za viongozi wa Serikali na dini kumalizika, huku zingine zikimlenga
Mvungi moja kwa moja, mwili wa Nasra ulichukuliwa na kurejeshwa msikitini kwa
ajili ya kuswaliwa, huku Mvungi akichukuliwa na askari Polisi wa Kitengo cha
Upelelezi Mkoa.
Kutokana
na hatua hiyo, baada ya swala mwili wa Nasra ulipelekwa katika makaburi ya Kola
kwa hatua za mwisho za maziko, bila uwepo wa Mvungi.
Akizungumza
na mwandishi makaburini kuhusu sababu za kutohudhuria kwa Mvungi makaburini,
Mkuu wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai wa Mkoa, Japhet Kibona, alisema
isingekuwa busara kumruhusu baba huyo
ashiriki maziko makaburini kutokana na hasira za wananchi.
Hata
Kaimu Shekhe wa Mkoa wa Morogoro, Ally Omar, alipokuwa akitangaza utaratibu wa
kuweka udongo kaburini, ambao kwa kawaida hutaja majina ya wahusika wakuu,
Mvungi hakuwa miongoni mwa waliotarajiwa kumsindikiza Nasra.
Badala
yake katika orodha hiyo ya waliotakiwa kuweka udongo kaburini, Shekhe Omar
alimwita Mkuu wa Mkoa, Joel Bendera,
Mbunge wa Morogoro Mjini, Abdulaziz Abood na Mkuu wa Upelelezi wa Makosa
ya Jinai wa Mkoa, Kibona, ambaye alimwakilisha Kamanda wa Polisi wa Mkoa.
Wengine
waliopata fursa ya kuweka udongo katika kaburi hilo ni Ofisa Ustawi wa Jamii
Mkoa wa Morogoro, Oswin Ngungamtitu na Mkurugenzi wa Kampuni ya Mabasi ya Al
–Saed, Omary Al- Saed, ambaye alijitolea gharama za kusafirisha mwili wa Nasra
kutoka Hospitali ya Taifa Muhimbili
jijini Dar es Salaam na za mazishi yake.
Ingawa
tayari Mvungi anakabiliwa na mashitaka ya kula njama na kufanya ukatili dhidi
ya mtoto huyo, katika Mahakama ya Hakimu Mkazi mjini Morogoro, viongozi
waliotoa nasaha katika uwanja wa Jamuhuri, walijikuta wakishindwa kuacha
kumtaja baba huyo.
Alianza
Mkuu Mkoa, Bendera alisema mateso aliyopata Nasra kwa kufungiwa kwenye boksi kwa zaidi ya
miaka mitatu, ni unyama na umetia aibu Mkoa wa Morogoro.
Alisema
kuwa kitendo hicho si cha kufurahisha kwa binadamu yeyote aliyeumbwa na
Mwenyezi Mungu na aliye na dini. “Unamweka mtoto ndani ya boksi kwa miaka
mitatu wakati wewe unanenepeana na unakuwa na amani? Jamani tuwe na uoga na
Mwenyezi Mungu.”
Aliwataka
viongozi wa serikali za mitaa na vijiji kujenga utamaduni wa kutembelea nyumba
zote, ili kujua watu wote wanaoishi na kuongeza kwamba kungekuwa na utamaduni
huo tangu awali, mtoto Nasra asingefanyiwa ukatili huo.
Pia
alikemea vitendo vya wazazi wa kiume kutelekeza watoto wao: “Haiwezekani
unamzaa mtoto halafu unamtelekeza… nakuhakikishia Mvungi adhabu utaibeba.”
Baada
ya Bendera, Mbunge wa Morogoro, Aziz Abood alisema kitendo kilichofanywa na
walezi wa Nasra si cha kiungwana na kumetia aibu Mkoa wa Morogoro.
Abood
alisema amekuwa akipata shida kutoka kwa wabunge wenzake waliokuwa bungeni,
kutokana na kitengo hicho ambapo wengi
wamekuwa wakihoji kuhusu ukatili aliofanyiwa mtoto huyo.
“Nimekuwa
nikiulizwa kulikoni mkoani Morogoro mmenza kufungia watoto ndani ya
boksi?“Alisema Abood.
Mbunge
huyo aliahidi kushirikiana Mkuu wa Mkoa kuhakikisha sheria inachukuwa mkondo
wake kwa wote waliohusika na ukatili huo na kuongeza kuwa endapo wahusika
watatoka kwa njia za panya, watarudishwa tena ndani.
Pia
aliahidi kumfanyia hitima ya mwisho mtoto huyo, ambayo
inatarajiwa
kufanyika katika uwanja huo huo wa Jamhuri.
Shekhe
Omari alisema ana mashaka na Uislamu wa
wahusika wanaotuhumiwa kwa ukatili kwa mtoto huyo, kwa kuwa ni kinyume
si tu cha sheria, bali pia na maadili ya
dini hiyo kwa kuwa Uisilamu unafundisha upendo.
Alitaka
sheria iangaliwe hata kwa wale majirani wa mama mlezi wa mtoto huyo, ambao
alisema kama wangetoa taarifa mapema yasingetokea hayo yaliyotokea kwa mtoto
Nasra.
“Majirani
waliokuwa wanaishi na yule mama aliyekuwa anamtesa matoto wanachukuliwa hatua
gani?” Alihoji Shekhe Omari.
Alisema
kuwa tendo hilo linaonekana kuwa na imani za kishirikina ndani yake, kwa kuwa
katika hali ya kawaida haiwezekani mtu amfungie mtoto ndani ya boksi huku akiwa
anajisaidia humo na ukaridhika na harufu.
No comments:
Post a Comment