Baadhi ya wafanyabiashara na wakazi wa jiji la Dar es Salaam wakikusanya mabaki ya mali zao mapema jana baada ya moto mkubwa kuteketeza soko la Mchikichini, maeneo ya Karume, Ilala Dar es Salaam usiku wa kuamkia jana. Soko hilo ni maarufu sana kwa biashara ya mitumba ambapo limekuwa likikusanya sehemu kubwa ya 'wamachinga'. Chanzo cha moto huo bado hakijafahamika.

No comments: