MAREKANI YAIKABIDHI TANZANIA MTAMBO WA MAWASILIANO



Serikali ya Marekani umeikabidhi Tanzania mtambo  wa mfumo wa mawasiliano wa masafa marefu, utakaowezesha kuona vyombo vilivyopo majini.
Hayo yalisemwa jana na Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Pereira Silima katika tukio la kukabidhiwa mtambo huo, lililofanyika Dar es Salaam.
Alisema mtambo huo uliokabidhiwa, utasaidia kuona vyombo vyote vilivyopo majini  na utasaidia kufanya mapinduzi  na utaangalia usalama maeneo ya pwani.
Pia, alisema mtambo huo, utasaidia kufichua dawa za kulevya, ambazo zinasafirishwa baharini na suala la kupambana na uvuvi holela unaofanyika baharini.
“Tunapenda kuwafahamisha watanzania wategemee kuwa vijana wao watakuwa salama na dawa za kulevya kwani mtambo huu utafichua kila kitu,” alisema Silima.
Aidha, aliishukuru serikali ya Marekani kwa msaada huo na aliwaahidi kuutumia vizuri na kuulinda ipasavyo.
Naibu Mkuu wa Polisi, Abdulrahman Kaniki katika maoni yake alisema mtambo waliopewa upo kidijitali zaidi, hivyo jeshi limepanga kutoa mafunzo kwa wafanyakazi wake ili kuwezesha kutumia mtambo huo.

No comments: