WAZIRI MKUU WA ZAMANI MARGARET THATCHER AFARIKI DUNIA...


Margaret Thatcher.
Waziri Mkuu wa zamani kupitia chama cha Conservative, Margaret Thatcher amefariki dunia mapema leo baada ya kupatwa na kiharusi.
Waziri Mkuu huyo wa kwanza Uingereza na mwanamke pekee kiongozi wa kisiasa amefariki akiwa na umri wa miaka 87, baada ya afya yake kuwa ikizorota kwa zaidi ya muongo mmoja.
Msemaji wake Lord Bell alisema: "Ni kwa huzuni kubwa kwamba Mark na Carol Thatcher wametangaza kuwa mama yao Baroness Thatcher amefariki kutokana na kiharusi asubuhi ya leo".
Malkia amesikitishwa kusikia kifo cha Baroness Thatcher na Mtukufu atatuma ujumbe binafsi wa rambirambi kwa familia ya marehemu, ilisema taarifa ya Buckingham Palace leo.
Waziri Mkuu David Cameron alisema: "Ilikuwa huzuni kubwa niliposikia kifo cha Thatcher. Tumepoteza kiongozi mkubwa, Waziri Mkuu bora na Mwingereza halisi".
Alitarajiwa kurejea mapema kutoka ziara yake ya Ulaya mchana huu kufuatia kifo cha Baroness Thatcher, ilisema taarifa ya Downing Street.
Binti wa kiongozi huyo, ambaye amekuwa Waziri Mkuu aliyekaa madarakani kwa muda mrefu zaidi nchini Uingereza katika karne ya 20, atazikwa kwa heshima zote za kitaifa kwenye kanisa kuu la Mt. Paul.
Tangu kifo cha Winston Churchill, hakuna mwanasiasa yeyote aliyepatiwa heshima kama hiyo. Mazishi yake pia yalifanyika hapo mwaka 1965.
Habari zaidi zitakujia hapa hapa muda mfupi ujao.

No comments: