VATICAN SASA KUISHI BABA WATAKATIFU WAWILI...

Papa Benedict XVI akisoma taarifa yake ya kujiuzulu. KULIA: Jengo ambapo makazi yake yatakuwa baada ya kujiuzulu.
Kutoka jina jipya na makazi mapya kuelekea ukweli wa kufedhehesha wa kuwa na 'Papa' wawili wanaoishi Vatican, Benedict XVI anaelekea himaya isiyo kwenye ramani pale atakapokuwa Baba Mtakatifu wa kwanza katika karne sita kujiuzulu.
Kiongozi huyo mwenye miaka 85 amechagua kusukuma siku zake katika nyumba ya zamani ya masista hatua chache kutoka St Peter's Basilica, akiongeza uwezekano kwamba atagongana na mrithi wake katika misingi ya kawaida.
Kwa miezi, wafanyakazi wa ujenzi wamekuwa wakikarabati jengo la ghorofa nne lililoambatana na nyumba kubwa ya utawa kwenye bustani za Vatican ambako masista wameishi miaka michache kwa wakati mmoja katika nyumba ya utawa.
Vifaa vya ujenzi vimeonekana vikiwekwa mbele ya nyumba hiyo wakati mabomba ya plastiki yakishushwa chini kutoka ghorofa ya juu na kuwekwa kwenye kontena la mizigo.
Hiyo ilitokana na ughafla wa uamuzi wa Benedict kujiuzulu kwamba hata maofisa hao wachache waliofahamu hilo ilikuwa siku moja kabla ya kuingia kwenye makazi yake ustaafu.
Jumba hilo la utawa la Mater Ecclesiac lilijengwa mwaka 1992 kwenye kiwanja cha makazi ya zamani ya mtunza bustani wa Vatican.
Papa Yohanne Paulo II alitaka makazi ndani ya uzio wa Vatican kutunza amri za kidini zinazotazamwa sana, na zaidi ya miaka amri kadhaa tofauti zitaanza kutumika katika miaka michache, alisema Giovanni Maria Vian, mhariri wa gazeti la L'Osservatore Romano la Vatican.
Masista waliamriwa kuhama makazi hayo Oktoba na ukarabati ukaanza haraka baada ya hapo.
Jengo hilo la utawa lina vyumba 12, kanisa lake dogo na maktaba na mara moja lilitumika kama ofisi za Vatican Radio.
Benedict ametembelea nyumba hiyo ya utawa mara kadhaa kwa miaka mingi na kusali misa mahali hapo mara tatu, mwaka 2005, 2006 na 2009.
Katika wakati wa mapumziko yake, Benedict anapendelea kupiga piano, kutazama DVD za vichekesho zisizo za rangi na kujisomea.

No comments: