RAIA WA MISRI AUA NA KUKATAKATA MIILI YA WENZAKE WAWILI...

KUSHOTO: Eneo ambapo Ibrahi alizika mabaki ya miili ya wenzake wawili. KULIA: Yusuf Ibrahim.
Mtu mmoja mwenye miaka 28 amewafyatulia risasi na kuua wanaume wawili, kuwakata vichwa vyao na mikono na kuwazika kwenye maeneo tofauti, polisi wamesema.
Yusuf Ibrahim, raia wa Misri ambaye anaishi mjini New Jersey, alikamatwa Jumapili iliyopita kuhusiana na mauaji hayo mawili ya kikatili na kushitakiwa kwa mashitaka mawili ya mauaji na kuharamisha mabaki ya binadamu.
Kwa mujibu wa hati ya kukamatwa, Ibrahim alizozana na wanaume hao wawili - wenye umri wa miaka 25 na 27 - ambao alikuwa akifahamiana nao kwenye gari lililoegeshwa nyuma ya nyumba yake iliyoko Buena Vista Februari 3.
Hapo ndipo alipowafyatulia risasi wote wawili kwenye kifua, kuwakatakata na kuvizika vipande vya miili yao tofauti kwenye msitu wa mbao mjini New Jersey. Utambulisho wa watu hao haujawekwa hadharani.
Vyanzo vya habari hatahivyo vilimtaja mmoja wa wanaume hao kuwa ni Amgad Konds mwenye miaka 27. Alihamia Marekani kutoka Misri miaka minne iliyopita, kwa mujibu wa kituo cha NBC.
Mamlaka zinaamini Ibrahim alikuwa akijaribu kutengeneza mazingira magumu ya utambuzi wa watu hao kwa kuwazika vichwa vyao na mikono sehemu tofauti na miili yao.
Mbwa aliyekonda aligundua sehemu za miili hiyo baada ya polisi kutonywa mahali ambapo miili hiyo inaweza kuwa imezikwa.
Ibrahim alionekana akiendesha Mercedes Benz jeupe lililokuwa mali ya mmoja wa wanaume hao. Baadaye lilikutwa limetelekezwa mjini Philadelphia.
Waathirika hao wawili, pia kutoka mjini New Jersey, walikuwa wanaishi chumba kimoja na muuaji, marafiki walikieleza kituo cha NBC10 cha mjini Philadelphia. Mmoja wa wanaume hao alihamia Marekani kutoka Misri miaka minne iliyopita.
Uhusiano wao na Ibrahim bado haujafahamika.

No comments: