Mkono wa mwanamke mlemavu wa ngozi, Maria Chambanenge, uliokatwa katikati ya wiki hii, umepatikana ukiwa umezikwa porini katika Kijiji cha Miangalua, wilayani Sumbawanga.
Kaimu Kamanda wa Polisi mkoani Rukwa, Peter Ngusa, alionesha mkono huo jana ukiwa umeanza kuharibika kwa Mkuu wa Mkoa, Stella Manyanya.
Akisimulia kisa kilichosababisha mkono huo kukatwa, ambacho sasa ni madai dhidi ya watuhumiwa wa unyama huo, Kamanda Ngusa pia alidai kuwa wameshakamata watuhumiwa watano.
Taarifa za Polisi zinaeleza kuwa mkazi wa kijiji hicho, Linus Silukala (42), ndiye aliyekuwa wa kwanza kukamatwa na anadaiwa ndiye aliyemshawishi mume wa Maria, Gabriel Yohana ili mkono wa mkewe ukatwe wapate utajiri.
Inadaiwa kabla ya ushawishi huo, Silukala alifika katika kitongoji cha Mkoe katika Kijiji cha Miangalua na kufanya urafiki na Gabriel na baadae kumshawishi wamkate Maria mkono.
Kwa mujibu wa madai ya taarifa hizo, baada ya kumkata mkono, Silukala aliahidi kuupeleka kwa mganga wa kienyeji, Peter Kazanda ‘Kaponda’ (53), ili awasaidie wapate utajiri kupita kiasi.
Baada ya kushawishiwa, inadaiwa Gabriel alimshirikisha mdogo wake, Gaudensi Yohana, ambaye inadaiwa ndiye aliyemkata shemeji yake huyo mkono wake wa kushoto.
Inadaiwa Gaudensi na Silukala, ambao wote wako mbaroni, waliufikisha mkono huo kwa Kazanda na kwa pamoja walienda kuuzika mkono huo porini, wakisubiri utakapoanza kuoza na kutoa funza, ndipo nao waanze ‘kuogelea’ kwenye bahari ya ukwasi.
Wakati mkono huo ukipelekwa kwa mganga na kuzikwa, inadaiwa Gabriel, ndio alikuwa amempeleka mkewe hospitali kwa matibabu.
Hata hivyo, inadaiwa wakati wameuzika, Silukala alianzisha mawasiliano na mfanyabiashara wa Sokomatola jijini Mbeya, Mtogwa Suleiman (30), kwa ajili ya biashara ya kuuza mkono huo.
Wakati wakiwa katika mawasiliano hayo, inadaiwa Polisi walimkamata Silukala, ambaye baada ya kubanwa, alianika mtandao mzima wa biashara hiyo ya kinyama.
Kamanda Ngusa alikiri kuwa Silukala alimtaja mganga Kazanda na baadae alimtaja mfanyabiashara wa Sokomatola jijini Mbeya, Mtogwa Suleiman (30), aliyekuwa anunue mkono huo.
Kwa mujibu wa Kamanda Ngusa, kwa kuwa Silukala alikuwa na mawasiliano na mfanyabiashara huyo, polisi walitumia mawasiliano hayo hayo kumnasa.
Alidai Polisi waliweka mtego, kwa kumpigia mfanyabiashara huyo simu na kumuahidi kumpelekea mkono huo, ambapo bila yeye kufahamu kuwa huo ni mtego, ‘alijilengesha’ mikononi mwa Polisi.
Wake wenza wa Maria, Honoratha Xevia maarufu Mama Daria na mwenzake Estha Pesambili maarufu Mama Ray, pia wamedai kuwa mgeni aliyefikia nyumbani kwao na kuishi hapo, ni Silukala na kuwa amekamatwa.
“Huyu mgeni, Silukala yeye tulikuwa tukiishi naye nyumbani, akisaidia kupalilia mashamba yetu hapa. Siku hiyo ya tukio saa 10 jioni, aliondoka nyumbani hapa bila ya kutuaga na hakurudi hadi tulipopata taarifa kuwa amekamatwa akihojiwa Polisi mjini Sumbawanga,“ alisema Mama Daria.
Manyanya hakuweza kujizuia na kujikuta akibubujikwa machozi hadharani, baada ya kukabidhiwa mkono huo baada ya kufukiwa porini.
Alijikuta akilia machozi mbele ya Kamati ya Ulinzi na Usalama, pale Kamanda Ngusa alipouonesha hadharani mkono huo juzi saa tatu usiku mbele ya majengo ya Hospitali ya Mkoa wa Rukwa, ambao ulikuwa umevingirishwa na majani ya mgomba.
Mkono huo ulikuwa tayari umeanza kutoa harufu kali na ulipooneshwa tu, mbali na Mkuu wa Mkoa, baadhi ya wajumbe wengine walibubujikwa na machozi ya huzuni.
Manyanya alimwagiza Kamanda wa Polisi Mkoa wa Rukwa, Jacob Mwaruanda, kuhakikisha wote watakaobainika kujihusisha unyama huo wakamatwe na kufikishwa kwenye vyombo vya dola.
“Kitendo hiki ni unyama uliopita ustaarabu wa kibinadamu hivyo naagiza Polisi ihakikishe watuhumiwa wote wanafikishwa mahakamani kwa kuwa tayari ushahidi upo na wenyewe wameonesha mkono huo walikoufukia.
“Tunatarajia hakutakuwa na visingizio vya kutaka kuharakisha kutolewa kwa hukumu ya shauri hilo,” alisema
Maria ambaye ni mama wa watoto wanne, kitinda mimba akiwa na umri wa miezi miwili, bado amelazwa katika Hospitali ya Mkoa wa Rukwa mjini kwa matibabu huku hali yake ikielezwa kuimarika.
Kaimu Kamanda wa Polisi mkoani Rukwa, Peter Ngusa, alionesha mkono huo jana ukiwa umeanza kuharibika kwa Mkuu wa Mkoa, Stella Manyanya.
Akisimulia kisa kilichosababisha mkono huo kukatwa, ambacho sasa ni madai dhidi ya watuhumiwa wa unyama huo, Kamanda Ngusa pia alidai kuwa wameshakamata watuhumiwa watano.
Taarifa za Polisi zinaeleza kuwa mkazi wa kijiji hicho, Linus Silukala (42), ndiye aliyekuwa wa kwanza kukamatwa na anadaiwa ndiye aliyemshawishi mume wa Maria, Gabriel Yohana ili mkono wa mkewe ukatwe wapate utajiri.
Inadaiwa kabla ya ushawishi huo, Silukala alifika katika kitongoji cha Mkoe katika Kijiji cha Miangalua na kufanya urafiki na Gabriel na baadae kumshawishi wamkate Maria mkono.
Kwa mujibu wa madai ya taarifa hizo, baada ya kumkata mkono, Silukala aliahidi kuupeleka kwa mganga wa kienyeji, Peter Kazanda ‘Kaponda’ (53), ili awasaidie wapate utajiri kupita kiasi.
Baada ya kushawishiwa, inadaiwa Gabriel alimshirikisha mdogo wake, Gaudensi Yohana, ambaye inadaiwa ndiye aliyemkata shemeji yake huyo mkono wake wa kushoto.
Inadaiwa Gaudensi na Silukala, ambao wote wako mbaroni, waliufikisha mkono huo kwa Kazanda na kwa pamoja walienda kuuzika mkono huo porini, wakisubiri utakapoanza kuoza na kutoa funza, ndipo nao waanze ‘kuogelea’ kwenye bahari ya ukwasi.
Wakati mkono huo ukipelekwa kwa mganga na kuzikwa, inadaiwa Gabriel, ndio alikuwa amempeleka mkewe hospitali kwa matibabu.
Hata hivyo, inadaiwa wakati wameuzika, Silukala alianzisha mawasiliano na mfanyabiashara wa Sokomatola jijini Mbeya, Mtogwa Suleiman (30), kwa ajili ya biashara ya kuuza mkono huo.
Wakati wakiwa katika mawasiliano hayo, inadaiwa Polisi walimkamata Silukala, ambaye baada ya kubanwa, alianika mtandao mzima wa biashara hiyo ya kinyama.
Kamanda Ngusa alikiri kuwa Silukala alimtaja mganga Kazanda na baadae alimtaja mfanyabiashara wa Sokomatola jijini Mbeya, Mtogwa Suleiman (30), aliyekuwa anunue mkono huo.
Kwa mujibu wa Kamanda Ngusa, kwa kuwa Silukala alikuwa na mawasiliano na mfanyabiashara huyo, polisi walitumia mawasiliano hayo hayo kumnasa.
Alidai Polisi waliweka mtego, kwa kumpigia mfanyabiashara huyo simu na kumuahidi kumpelekea mkono huo, ambapo bila yeye kufahamu kuwa huo ni mtego, ‘alijilengesha’ mikononi mwa Polisi.
Wake wenza wa Maria, Honoratha Xevia maarufu Mama Daria na mwenzake Estha Pesambili maarufu Mama Ray, pia wamedai kuwa mgeni aliyefikia nyumbani kwao na kuishi hapo, ni Silukala na kuwa amekamatwa.
“Huyu mgeni, Silukala yeye tulikuwa tukiishi naye nyumbani, akisaidia kupalilia mashamba yetu hapa. Siku hiyo ya tukio saa 10 jioni, aliondoka nyumbani hapa bila ya kutuaga na hakurudi hadi tulipopata taarifa kuwa amekamatwa akihojiwa Polisi mjini Sumbawanga,“ alisema Mama Daria.
Manyanya hakuweza kujizuia na kujikuta akibubujikwa machozi hadharani, baada ya kukabidhiwa mkono huo baada ya kufukiwa porini.
Alijikuta akilia machozi mbele ya Kamati ya Ulinzi na Usalama, pale Kamanda Ngusa alipouonesha hadharani mkono huo juzi saa tatu usiku mbele ya majengo ya Hospitali ya Mkoa wa Rukwa, ambao ulikuwa umevingirishwa na majani ya mgomba.
Mkono huo ulikuwa tayari umeanza kutoa harufu kali na ulipooneshwa tu, mbali na Mkuu wa Mkoa, baadhi ya wajumbe wengine walibubujikwa na machozi ya huzuni.
Manyanya alimwagiza Kamanda wa Polisi Mkoa wa Rukwa, Jacob Mwaruanda, kuhakikisha wote watakaobainika kujihusisha unyama huo wakamatwe na kufikishwa kwenye vyombo vya dola.
“Kitendo hiki ni unyama uliopita ustaarabu wa kibinadamu hivyo naagiza Polisi ihakikishe watuhumiwa wote wanafikishwa mahakamani kwa kuwa tayari ushahidi upo na wenyewe wameonesha mkono huo walikoufukia.
“Tunatarajia hakutakuwa na visingizio vya kutaka kuharakisha kutolewa kwa hukumu ya shauri hilo,” alisema
Maria ambaye ni mama wa watoto wanne, kitinda mimba akiwa na umri wa miezi miwili, bado amelazwa katika Hospitali ya Mkoa wa Rukwa mjini kwa matibabu huku hali yake ikielezwa kuimarika.
No comments:
Post a Comment