KIBAKA AINGIA MLANGO WA JIRANI AKIDHANI KWA RIHANNA...

Mtu mmoja amekamatwa nje ya nyumba ya mwimbaji Rihanna iliyoko Southern California katika Pacific Palisades ... baada ya majirani kumuona mtu akiangaza angaza na kumkamata juzi usiku, imefahamika.
Vyanzo vya kisheria vimeeleza ... mtuhumiwa huyo aliwaeleza polisi mtu mmoja alimtumia baruapepe akimwelekeza jinsi ya kuingia kwenye nyumba hiyo ... hivyo alikwenda kwenye jengo hilo na kufuata maelekezo hayo.
Imeelezwa maelekezo hayo yalifanya kazi ... sababu mtu huyo aliweza kuingia ndani ya nyumba hiyo ... ambako alidaiwa kupeleleza kwa muda kabla ya majirani kugundua kilichokuwa kikiendelea.
Vyanzo vimeeleza ... majirani walikwenda kwenye nyumba hiyo na kumkabili mtu huyo -- na hatimaye kumshikilia baada ya kujiridhisha kwamba haishi pale. Polisi waliitwa eneo la tukio na kumchukua mtu huyo chini ya ulinzi.
Mtu huyo kwa sasa anachunguzwa kwa ujambazi.
Polisi wamesema mtu huyo hakuwahi kuingia kwenye nyumba ya Rihanna ... lakini, badala yake aliingia mlango mwingine akiamini kwamba ilikuwa ni nyumba ya Rihanna.
Alikamatwa nje ya jengo hilo ... na si nyumbani kwa Rihanna.

No comments: