Stella Manyanya. |
Kuibuka kwa biashara ya binadamu kunakoendelea kuimarika duniani, kumemtia shaka Mkuu wa Mkoa wa Rukwa, Stella Manyanya na kuonya taasisi zinazochukua watoto na kuwalea bila taarifa zao kufahamika.
Manyanya alitoa onyo hilo juzi kutokana na taarifa ya kuwapo kituo cha elimu na malezi ya Kiislamu cha Nourul Hudaa Islamic Center Muzdalifa (MICO) kilichoko mjini hapa licha ya kuwa hakipo kisheria, lakini hata orodha ya watoto wanaolelewa hapo haifahamiki.
Pia viongozi wanaoendesha kituo hicho hawafahamiki huku daftari linaloonesha watoto hao wanakotoka au taarifa za wazazi wao halipo.
Kutokana na hali hiyo, Mkuu wa Mkoa alilazimika kutengua uamuzi wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya ya Sumbawanga iliyoamuru kufungwa kituo cha MICO baada ya kushindwa kukidhi vigezo muhimu ikiwa ni pamoja na kutosajiliwa.
Manyanya alifikia uamuzi huo jana jioni baada ya watoto 190 na walimu wao wawili, Hamisi Matope na Ustaadh Idrisa Majundo kutoka kituo hicho kilichopo eneo la Nelson Mandela mjini hapa, kuandamana hadi katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, ili waonane naye.
Akimweleza Mkuu wa Mkoa katika kikao cha dharura kilichofanyika katika jengo la Ofisi ya Mkuu wa Mkoa na kuhudhuriwa na Katibu Tawala wa Mkoa, Salum Chima, mmoja wa walimu wa kituo hicho Matope alidai walilazimika kuwapeleka watoto hao ili Mkuu wa Mkoa awape malazi, kwa kuwa kituo chao kimeamriwa kufungwa na Manispaa ya Sumbawanga.
“Tumeamriwa kufunga kituo chetu na watoto warudishwe kwao hadi kitakapokidhi hadhi ya kuwa chuo, sasa tumewaleta watoto hawa kwa Mkuu wa Mkoa, ili awape malazi hadi watakapoweza kurejeshwa kwao, kwa kuwa sasa hawana pa kulala,“ alisema Matope.
Watoto hao kwa mujibu wa Majundo baadhi yao ni yatima kutoka sehemu mbalimbali za Mkoa wa Rukwa na mikoa ya jirani ya Mbeya, Katavi na Kigoma, ambapo baadhi yao wanasoma shule za msingi na sekondari mjini hapa.
Wengi wao hawakuwa tayari kuzungumza na mwandishi wa habari hizi kwa kile walichodai kuwa wamekatazwa na walimu wao kusema lolote kuhusu malezi yao.
Hata hivyo, mtoto aliyejitambulisha kwa jina la Maka Salumu (15) wa Kigoma, alionesha ujasiri na kudai kuwa waliandamana ili kumshinikiza Mkuu wa Mkoa awape malazi na chakula, hadi watakaporejea kwao kwani kituo chao kimefungwa kwa amri ya Manispaa.
“Mtoto mdogo miongoni mwetu ana umri wa miaka saba, miye nililetwa kituoni na bibi yangu nikitoka Kigoma, sasa kimefungwa hatuna pa kulala, hivyo tumekuja hapa ikiwezekana tulale hapa hapa ofisini kwa Mkuu wa Mkoa, hadi tutakaporejeshwa kwetu,“ alisema Salumu.
Katibu Tawala wa Mkoa, Chima alifafanua sababu za kufungwa kwa kituo hicho.
Alisema watoto katika kituo hicho walikuwa wakikabiliwa na kadhia mbalimbali zikiwamo za kulala chini sakafuni huku sakafu hiyo ikiwa na imelowa maji hata kwa waliokuwa wagonjwa, kushinda na njaa.
Licha ya kuwa kituo hicho hakijasajiliwa lakini watoto hao walikuwa hawana sehemu ya kupikia, huku majengo ya kituo hicho yakiwa chakavu na yasiyofaa kabisa kwa matumizi ya binadamu, kwani hata vyumba vya kulala watoto hao sakafu zina mashimo.
“Miye binafsi nilishafika kituoni hapo, pamoja na matatizo hayo pia hakijasajiliwa, hivyo hakipo kisheria na hata utunzaji kumbukumbu zake si mzuri kwani hakina hata daftari la orodha ya watoto hao sambamba na kuwa hata idadi yao haijulikani pia viongozi wanaongoza kituo hicho hawafahamiki kabisa,“ alisema Chima.
Ndipo Manyanya licha ya kuwashukuru kufanya maandamano ya amani, pia aliagiza wapewe miezi miwili zaidi ili waboreshe upungufu uliojitokeza.
Pia alimwagiza Chima afanye ukaguzi wa mara kwa mara katika kituo hicho, ili kuhakikisha kama upungufu uliojitokeza umerekebishwa na kuboreshwa pia wapewe wataalamu watakaowasaidia kuhakikisha kinasajiliwa kisheria.
“Lazima idadi na majina na wanakotoka ifahamike, si sahihi kulea watoto ambao hawafahamiki wazazi wao wako wapi lazima na watoto wenyewe wafahamishe walipo wazazi wao,“ alisisitiza.
Manyanya alitoa onyo hilo juzi kutokana na taarifa ya kuwapo kituo cha elimu na malezi ya Kiislamu cha Nourul Hudaa Islamic Center Muzdalifa (MICO) kilichoko mjini hapa licha ya kuwa hakipo kisheria, lakini hata orodha ya watoto wanaolelewa hapo haifahamiki.
Pia viongozi wanaoendesha kituo hicho hawafahamiki huku daftari linaloonesha watoto hao wanakotoka au taarifa za wazazi wao halipo.
Kutokana na hali hiyo, Mkuu wa Mkoa alilazimika kutengua uamuzi wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya ya Sumbawanga iliyoamuru kufungwa kituo cha MICO baada ya kushindwa kukidhi vigezo muhimu ikiwa ni pamoja na kutosajiliwa.
Manyanya alifikia uamuzi huo jana jioni baada ya watoto 190 na walimu wao wawili, Hamisi Matope na Ustaadh Idrisa Majundo kutoka kituo hicho kilichopo eneo la Nelson Mandela mjini hapa, kuandamana hadi katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, ili waonane naye.
Akimweleza Mkuu wa Mkoa katika kikao cha dharura kilichofanyika katika jengo la Ofisi ya Mkuu wa Mkoa na kuhudhuriwa na Katibu Tawala wa Mkoa, Salum Chima, mmoja wa walimu wa kituo hicho Matope alidai walilazimika kuwapeleka watoto hao ili Mkuu wa Mkoa awape malazi, kwa kuwa kituo chao kimeamriwa kufungwa na Manispaa ya Sumbawanga.
“Tumeamriwa kufunga kituo chetu na watoto warudishwe kwao hadi kitakapokidhi hadhi ya kuwa chuo, sasa tumewaleta watoto hawa kwa Mkuu wa Mkoa, ili awape malazi hadi watakapoweza kurejeshwa kwao, kwa kuwa sasa hawana pa kulala,“ alisema Matope.
Watoto hao kwa mujibu wa Majundo baadhi yao ni yatima kutoka sehemu mbalimbali za Mkoa wa Rukwa na mikoa ya jirani ya Mbeya, Katavi na Kigoma, ambapo baadhi yao wanasoma shule za msingi na sekondari mjini hapa.
Wengi wao hawakuwa tayari kuzungumza na mwandishi wa habari hizi kwa kile walichodai kuwa wamekatazwa na walimu wao kusema lolote kuhusu malezi yao.
Hata hivyo, mtoto aliyejitambulisha kwa jina la Maka Salumu (15) wa Kigoma, alionesha ujasiri na kudai kuwa waliandamana ili kumshinikiza Mkuu wa Mkoa awape malazi na chakula, hadi watakaporejea kwao kwani kituo chao kimefungwa kwa amri ya Manispaa.
“Mtoto mdogo miongoni mwetu ana umri wa miaka saba, miye nililetwa kituoni na bibi yangu nikitoka Kigoma, sasa kimefungwa hatuna pa kulala, hivyo tumekuja hapa ikiwezekana tulale hapa hapa ofisini kwa Mkuu wa Mkoa, hadi tutakaporejeshwa kwetu,“ alisema Salumu.
Katibu Tawala wa Mkoa, Chima alifafanua sababu za kufungwa kwa kituo hicho.
Alisema watoto katika kituo hicho walikuwa wakikabiliwa na kadhia mbalimbali zikiwamo za kulala chini sakafuni huku sakafu hiyo ikiwa na imelowa maji hata kwa waliokuwa wagonjwa, kushinda na njaa.
Licha ya kuwa kituo hicho hakijasajiliwa lakini watoto hao walikuwa hawana sehemu ya kupikia, huku majengo ya kituo hicho yakiwa chakavu na yasiyofaa kabisa kwa matumizi ya binadamu, kwani hata vyumba vya kulala watoto hao sakafu zina mashimo.
“Miye binafsi nilishafika kituoni hapo, pamoja na matatizo hayo pia hakijasajiliwa, hivyo hakipo kisheria na hata utunzaji kumbukumbu zake si mzuri kwani hakina hata daftari la orodha ya watoto hao sambamba na kuwa hata idadi yao haijulikani pia viongozi wanaongoza kituo hicho hawafahamiki kabisa,“ alisema Chima.
Ndipo Manyanya licha ya kuwashukuru kufanya maandamano ya amani, pia aliagiza wapewe miezi miwili zaidi ili waboreshe upungufu uliojitokeza.
Pia alimwagiza Chima afanye ukaguzi wa mara kwa mara katika kituo hicho, ili kuhakikisha kama upungufu uliojitokeza umerekebishwa na kuboreshwa pia wapewe wataalamu watakaowasaidia kuhakikisha kinasajiliwa kisheria.
“Lazima idadi na majina na wanakotoka ifahamike, si sahihi kulea watoto ambao hawafahamiki wazazi wao wako wapi lazima na watoto wenyewe wafahamishe walipo wazazi wao,“ alisisitiza.
No comments:
Post a Comment