CHEKA TARATIBU...

Kibaka kaiba televisheni kwenye nyumba moja bila kujua kuna kichaa anaishi mle ndani. Baada ya kubeba ile televisheni na kuanza kutimua mbio, ghafla kibaka akashangaa anakimbizwa na mtu nyuma yake. Kila akiongeza spidi na yule mtu anaongeza, mwishowe akaamua kusimama na kuhoji kulikoni. Yule jamaa akajibu, "Duh, umesahau rimoti hii hapa!" Kasheshe...

No comments: