CHEKA TARATIBU...

Jamaa mmoja kapita sehemu isiyoruhusiwa kwenye kambi moja ya jeshi. Fasta akapewa adhabu ya kupakia matofali 1,000 kwenye lori lililokuwa jirani. Baada ya kupakia matofali 900, jamaa akakumbuka mkuu wa ile kambi walisoma naye. Akampigia simu na mambo yalikuwa hivi. JAMAA: Haloo mkuu, vijana wako wamenipa adhabu ya kupakia matofali kwenye lori. MKUU: Aah, hao wajinga sana, hawajui kama tumesoma wote? Sasa hebu yashushe halafu uje ofisini! Duh, balaa...

No comments: