MWILI WA BONDIA CAMACHO WAPELEKWA MAREKANI KWA MAZISHI...

Mwili wa bondia Hector 'Macho' Camacho umepakiwa kwenye ndege nchini Puerto Rico jana, tayari kwa safari ya kwenda Marekani, ambako msiba wa faragha umepangwa kufanyika wiki hii.
Kama ilivyoripotiwa awali, mama wa Camacho aliomba ufanyike msiba wa faragha mjini New York, ambako pia atazikwa.
Jumanne iliyopita, mashabiki na waombolezaji nchini Puerto Rico waliweza kushuhudia mwili wa Camacho baada ya jeneza lake kufunuliwa muda mfupi kabla ya kupakiwa kwenye ndege tayari kwa safari.
Misa ya faragha kumwombea marehemu ilifanyika mapema wiki hii.
Camacho alifariki dunia Jumamosi iliyopita kutokana na majeraha aliyopata baada ya kushambuliwa kwa risasi na watu wasiojulikana waliokuwa kwenye gari wiki iliyopita.

No comments: