JELA KWA KUTUMIA KIMAKOSA WANAFUNZI MESEJI ZA MAPENZI...

Craig Evans anaweza kufikiria mambo yataendelea kuwa shwari baada ya kutuma kwa bahati mbaya meseji za mapenzi kwa watu wote aliowasevu kwenye simu yake badala ya mpenzi wake.
Kocha huyo wa kuogelea mwenye miaka 24 aliishia gerezani kutokana na sheria ya makosa kujamiiana baada ya meseji hiyo kwenda kwa wanafunzi wawili wasichana.
Evans aliandika mwaliko kwa mpenzi wake akimwomba kama angependa wakutane kimwili bila kutumia kinga.
Kwa bahati mbaya, kidole chake kilitereza katika simu yake ya BlackBerry smartphone na kufanya ujumbe huo kusafiri kupitia mfumo wa BlackBerry Messenger kwa namba zote zilizomo katika simu yake.
Lakini pia akajikuta akikabiliana na machungu zaidi kufuatia ujumbe huo kuwafikia na wanafamilia wake, na hivyo kufanya makosa ya Evans kuchukua uzito mkubwa zaidi.
Miongoni mwa waliopokea meseji hiyo walikuwa wasichana wawili wenye umri wa miaka 13 na 14, ambao wanafundishwa na Evans kuogelea katika kituo cha burudani, na hivyo kupelekea kukamatwa kwake na kushitakiwa kwa kusababisha au kushawishi watoto kujihusisha na masuala ya vitendo vya ngono.
Alihukumiwa kifungo cha miezi 18 jela katika mahakama ya Birmingham Julai, mwaka huu.
Stori hiyo iliibuliwa mahakamani wiki hii pale wanasheria walipofika mahakamani kupinga mjini London kuomba aondolewe hatia yake.
Walihoji kwamba 'kushindwa kwa Evans kudhibiti matumizi ya BlackBerry yake' kulifanya 'ugumu kuhukumu kwamba alikuwa amedhamiria kumlenga yeyote'.
Katika meseji hiyo, Evans, mkazi wa Birmingham, alimtaka mpenzi ambaye hakufahamika kama wangeweza kufanya mapenzi 'bila kutumia kinga' na endapo wangependa wafanye kwa 'haraka au taratibu'.
Jaji Lord Justice Elias alisema: "Ishu ya kesi hii ni kwamba hazikuwa meseji za kawaida. Meseji hizo ...zilitumwa kwa kila namba iliyokuwamo katika simu yake, wakiwamo ndugu zake wa familia moja."
Aliongeza: "Ukweli kwamba zilijirudia unaonesha kwamba dhahiri alishindwa kudhibiti matumizi ya BlackBerry yake.
"Ni vigumu kuhuku kwamba alikuwa akimlenga yeyote.
"Kulikuwa na mambo mengi yanayopunguza ukali katika kesi hii."
Jaji huyo aliongeza kuwa hukumu hiyo, ambayo hatahivyo imepunguza hadi miezi tisa, inaweza kusimamishwa kwa muda 'kutokana na mambo yasiyokuwa ya kawaida' na kumwachia huru Evans.

No comments: