CHEKA TARATIBU...

Basi moja la abiria likiwa limejaza wanasiasa wa chama kimoja maarufu nchini kwa bahati mbaya likaacha njia na kugonga mti kwenye shamba la mkulima mmoja mzee.
Mkulima akaenda eneo la tukio kuona kilichotokea. Baada ya kujiridhisha kile alichokiona, akaanza kuchimba shimo kubwa na kuwazika wanasiasa wote.
Siku chache baadaye Kamanda wa polisi wa mkoa akapita na kuona basi likiwa bado eneo la tukio, ndipo akasimama na kumuuliza yule mkulima, "Inamaana wote walikufa kwenye ajali hii?"
Mkulima akajibu, "Baadhi yao waliniambia kuwa bado wazima, lakini si unajua jinsi wanasiasa walivyo waongo." Duh, kasheshe…

No comments: