WABUNGE, MAWAZIRI WAOMBOLEZA KIFO CHA CASSIUS KIBASSA...

Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano, Mhe. Anne Makinda (wa pili kushoto), Naibu Spika Mhe. Job Ndugai na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge) William Lukuvi wakihudhuria misa maalumu ya kumwombea Marehemu Cassius Kibassa ambaye alifariki ghafla Aprili 12, mwaka huu mjini Dodoma. Marehemu ambaye ni mtoto pekee wa kiume katika familia yao ya watoto watano, alikuwa ameajiriwa na Bunge kama Mhasibu. Kushoto ni mama mzazi wa marehemu, Consolata Sekalinga. Mungu ailaze roho ya marehemu mahali pema peponi, Amina.

No comments: