BINTI WA MIAKA 15 MBARONI KWA MAUAJI YA MAMA YAKE NA BABA WA KAMBO


Msichana mwenye umri wa miaka 15 amekamatwa kwa tuhuma za kumuua mama yake mzazi na rafiki wa kiume wa mama huyo kwa kile alichodai kubakwa na mwanaume huyo, polisi wamesema.

Binti huyo, ambaye hajatajwa jina, alidaiwa kumweleza mama yake kuhusu shambulio alilofanyiwa, lakini mama huyo akagoma kuamini madai hayo, vyanzo vya kipolisi vilisema.
Akiwa amechukizwa na uamuzi wa mama yake, askari wamesema msichana huyo akamfyatulia risasi mama yake huku rafiki wa binti huyo akimuua rafiki wa kiume wa mama huyo, Desemba 27, kabla ya binti huyo kutorokea nyumbani kwa binamu yake.
Kwa mujibu wa maofisa, msichana huyo  amekuwa akiishi na ndugu yake huyo bila kubainisha kwamba alifanya tukio hilo mpaka hivi leo alipoweka bayana.
Askari walisema binamu yake huyo alikuja kufahamu baada ya ukimya wa siku kadhaa kutoka kwa wazazi wa binti huyo, ndipo binti huyo akakiri kuhusika na kilichotokea.
Maofisa wa polisi ndipo walipokwenda nyumbani kwa familia ya binti huyo iliyoko ghorofa ya tano ya jingo moja lililoko kwenye majengo ya Sheepshead Bay Houses na kukuta mabaki ya miili ya mwanaume na mwanamke.
Ingawa awali wachunguzi walidhani waathirika hao walichomwa na vitu vyenye ncha kali, polisi walibaini baadaye kitu tofauti.

No comments: