KARDINALI PENGO KUONGOZA MISA YA IJUMAA KUU


Askofu Mkuu wa Jimbo Katoliki la Dar es Salaam, Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo, anatarajiwa kuongoza misa ya Ijumaa Kuu, itakayofanyika katika Kanisa la Mtakatifu Joseph jimboni humo.

Wakristo wote duniani hufanya misa hiyo kila mwaka, kukumbuka mateso na kufa kwa Yesu Kristo.
Ratiba iliyotolewa Dar es Salaam jana na Katibu wa Jimbo, Dennis Wigirwa ilionesha kuwa Pengo ataadhimisha misa hiyo kanisani hapo itakayoanza saa 9:00 jioni.
Pia, alisema kuwa Misa ya  mkesha wa sikukuu ya Pasaka, itafanyika saa 2 usiku Jumamosi  na Askofu huyo ndio atakayeiongoza.
Aliongeza kuwa misa ya Pasaka ya kukumbuka kufufuka kwa Yesu Kristo. itafanyika saa 3:00 asubuhi na itaongozwa na Pengo.

No comments: