Upelelezi wa kesi ya kula njama ya kudhuru kwa sumu,
inayomkabili Mkurugenzi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Wilfred
Lwakatare na mwenzake bado haujakamilika.
Wakili wa Serikali Genes Tesha alidai hayo jana mbele ya
Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Janeth Kaluyenda wakati kesi
hiyo ilipotajwa jana.
Hakimu Kaluyenda aliahirisha kesi hiyo hadi Aprili Mosi
mwaka huu itakapotajwa tena kwa ajili ya kuangalia kama upelelezi umekamilika.
Lwakatare na Ludovick Joseph wanadaiwa Desemba 28, mwaka
juzi katika eneo la King’ong’o, Wilaya ya Kinondoni, kwa pamoja walikula njama
za kutoa sumu kwa nia ya kumdhuru Mhariri wa Gazeti la Mwananchi Dennis Msacky.
Katika hatua nyingine, upelelezi wa kesi ya mauaji
ya kutokusudia kutokana na kuporomoka kwa jengo la ghorofa 16, inayowakabili
watu 12 bado haujakamilika.
Washitakiwa katika kesi hiyo ni Gabriel Fuime,
mfanyabiashara Laza Radha, Diwani katika Manispaa ya Kinondoni, Ibrahim Mohamed
(59), vigogo wa Manispaa ya Ilala ambao ni Mhandisi Mkuu, Charles (48),
Mhandisi wa Majengo Godluck Sylivester (35) na Mkurugenzi Mkuu wa Mkaguzi wa
Majengo, Willibrod Mugyabuso (42).
Wengine ni Mhandisi Mohamed Abdurkarim (61), Mhandisi
Mshauri, Zonazea Oushoshaodaga Hema (59), Msajili Msaidizi AQRB, Albert Mnuo na
Ofisa Mkuu Mtekelezaji OQRB, Joseph Ringo (60), Mkadiriaji Ujenzi, Vedasto
Ruhale (59), Msanifu Majengo, Michael. Waliowasilisha ombi hilo ni washitakiwa
tisa uamuzi unawahusu washitakiwa wote.
Inadaiwa kuwa Machi 29 mwaka jana, katika mtaa wa India
Gandhi Ilala, Dar es Salaam bila kukusudia washitakiwa waliwaua watu 27.
No comments:
Post a Comment