Tanzania
inazidi kupiga hatua katika sekta ya afya, na sasa inatarajia kuachana na
usafirishaji wa sampuli za magonjwa ya uambukizi mkali yenye virusi
visababishavyo damu kutoka mwilini, ikiwemo ebola na dengue.
Hali
hiyo inatokana na kuanza ujenzi wa maabara ya magonjwa hayo, unaotarajiwa
kukamilika mwishoni mwa mwezi huu.
Maabara
ya kwanza ya magonjwa hayo, inajengwa katika Hospitali ya Rufaa Kanda ya Mbeya,
ambapo zaidi ya Sh milioni 109 zimeshatumika.
Maabara
hiyo itakayoanza kutumika hivi karibuni, itakuwa imeboreshwa kutoka iliyokuwepo
awali ya upimaji maambukizi ya kifua kikuu.
Naibu
Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk Steven Kebwe alisema ukarabati wa maabara
hiyo, ulianza Februari mwaka huu na utakamilika mwishoni mwa mwezi huu baada ya
mkandarasi kutia saini mkataba na Serikali Februari 6, mwaka huu akipewa wiki
nne. Alisema hayo baada ya kutembelea hospitali hiyo na kuzungumza na watumishi
hivi karibuni.
Dk
Kebwe alisema maabara hiyo inatarajiwa kuanza kutumika kabla ya mwezi Julai
mwaka huu, ambapo sekta ya afya itaingia katika mfumo wa Matokeo Makubwa Sasa
(BRN) na hivyo kusaidia urahisi wa upatikanaji wa huduma kwa kiwango cha juu.
Alisema
kukamilika kwa maabara hiyo, kutapunguza maambukizi ya magonjwa ya milipuko
kama vile dengue, ebola na homa ya bonde la ufa.
Pia,
maabara hiyo itatumika kufanyia utafiti, kufundishia na vipimo kwa watu
walioambukizwa na wasioambukizwa.
Naibu
Waziri alisema awali kabla ya kuwa na maabara ya kupima magonjwa hayo, mtu
yeyote akiugua ilikuwa inalazimu damu yake kuchukuliwa kisha kupelekwa Afrika
Kusini au Nairobi kwa ajili ya vipimo, kutokana na kuwepo kwa maabara yenye
uwezo huo na hivyo kuchelewa upatikanaji wa majibu.
Alisema
uwepo wa maabara katika Mkoa wa Mbeya, utasaidia kukabiliana na magonjwa ya
milipuko yanayotokea katika nchi za jirani, kama Malawi, Zambia na Jamhuri ya
Kidemokrasia ya Kongo (DRC).
Mkurugenzi
wa Hospitali ya Rufaa Kanda ya Nyanda za Juu Kusini, Dk Mpoki Ulisubisya
alisema upatikanaji wa maabara hiyo ni hatua kubwa na muhimu ambayo Serikali
imeifanya kukabiliana na magonjwa yanayotokana na kutokwa damu mwilini.
No comments:
Post a Comment