Halmashauri
ya Manispaa ya Ilala, Dar es Salaam inakusudia kutunga sheria kadhaa ndogo,
ikiwemo ya kudhibiti ombaomba na uendeshaji wa soko la samaki Feri.
Sheria nyingine zinazotarajiwa kutungwa ni
pamoja na sheria za zao la ngozi na za mfuko wa elimu.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa kwa umma na
Halmashauri ya Ilala ambayo imesainiwa na Mkurugenzi wake, Isaya Mngurumi
imesema mabadiliko hayo ni kwa mujibu wa kifungu cha 89 cha sheria za Serikali
za Mitaa Mamlaka za Miji sura ya 288 ya mwaka 2002.
Aidha, sambamba na mabadiliko hayo, vilevile
halmashauri hiyo inakusudia pia kufanya marekebisho katika sheria nyingine
ndogo ambazo ni sheria ya usafi wa
mazingira, kodi za majengo na matumizi ya barabara.
Halmashauri hiyo imewataka wananchi pamoja na
wadau wote kujitokeza kutoa maoni yao na mapendekezo kuhusu utungaji wa
marekebisho ya sheria hizo zilizotajwa.
Aidha, maoni hayo yametakiwa kuwasilishwa kwa
njia ya maandishi katika ofisi za watendaji kata, ofisi ya mkurugenzi idara ya
sheria katika ofisi za Arnautouglo Mnazi Mmoja kabla ya Machi 31, mwaka huu.
No comments:
Post a Comment