Mahakama
ya Hakimu Mkazi Kisutu, imeamuru raia kutoka nchini Marekani, Sammy Almahri
aliyekuwa anakabiliwa na mashitaka ya kumuua mke wake, ametakiwa kupelekwa
nchini Uingereza na kushitakiwa katika sehemu ambayo alifanya mauaji hayo.
Hakimu
Mkazi, Waliarwande Lema alitoa amri hiyo baada ya kukubali ombi la upande wa
Jamhuri lililowasilishwa baada ya kufuta mashitaka dhidi ya mshitakiwa huyo
wiki iliyopita.
Mshitakiwa
huyo alifikishwa mahakamani wiki iliyopita na kusomewa mashitaka hayo mbele ya
Hakimu Mkazi Janeth Kaluyenda, hata hivyo Mkurugenzi wa Mashitaka (DPP)
aliwasilisha hati mahakamani kuwa hana nia ya kuendelea kumshitaki.
Hata
hivyo, baada ya kuachiwa huru, Almahri aliendelea kuwa mahabusu chini ya ulinzi
hadi upande wa Jamhuri ulipowasilisha ombi la kumpeleka nchini Uingereza
akashitakiwe sehemu anayodaiwa kufanya mauaji.
Almahri
anadaiwa Desemba 31, mwaka 2014 nchini Uingereza ndani ya Hoteli ya Curdiff
South Wiles iliyopo nchini humo, kwa makusudi alimuua mpenzi wake, Nadine
Aburas.
Awali
mbele ya Hakimu Lema, mshitakiwa alisomewa maelezo ya ombi hilo na kupitia
Wakili wake, Mabere Marando alidai hana pingamizi kwa kuwa ndiyo matakwa ya
serikali kumpeleka huko.
Mahakama
iliamuru pia vitu vya mshitakiwa vilivyochukuliwa Polisi wakati
alipokamatwa, vipelekwe Uingereza na
atakwenda kukabidhiwa huko.
Awali
mshitakiwa huyo alipopandishwa kizimbani kwa mara ya kwanza, alidai alipokonywa
baadhi ya nyaraka zake muhimu, ana matatizo ya kiafya pia amefungiwa akaunti
zake za benki.
Aliomba
Mahakama itoe ruhusa ya kufunguliwa kwa akaunti hiyo pamoja na kurudishiwa
nyaraka ili isiathiri familia yake kwa kuwa ana watoto wawili ambao ni
wanafunzi nchini Marekani, pia ana matatizo ya kiafya, hivyo anatakiwa kuwa
chini ya uangalizi wa daktari maalumu.
No comments:
Post a Comment