Kampuni ya
Reli Tanzania (TRL) imesema mabehewa 15 kati ya 22 ya abiria yaliyonunuliwa na
serikali kutoka Korea Kusini yataanza kutoa huduma kwenda Kigoma kupitia
stesheni 17 kuanzia Aprili mosi mwaka huu.
Imesema mabehewa mengine yatabakia, ikiwa ni kwa
sababu za kiuendeshaji ndani ya kampuni hiyo.
Kaimu Mkuu wa Masoko wa TRL, Charles Ndenge alisema hayo jana Dar es Salaam na
kuongeza kuwa mabehewa hayo
yalishafanyiwa majaribio na kampuni hiyo
na kuridhika kuwa hayana kasoro. Aidha Mamlaka ya Usafiri wa Nchi Kavu na Majini (Sumatra) imetoa idhini ya kuanzishwa kwa
huduma hiyo kwa kuyatumia mabehewa hayo baada ya kutimizwa kwa masharti ya
uendeshaji.
Alisema safari za treni zitakuwa mara moja siku za
Jumapili ikianzia stesheni ya Dar es Salaam.
No comments:
Post a Comment