Katika
hali isiyokuwa ya kawaida, wakazi wa Mtaa za Nsalaga jijini Mbeya, asubuhi wameshuhudia
matukio ya mauaji ya watu wawili ndugu, moja likiwa ni mtu aliyemchinja na
kumtenganisha kichwa na kiwiliwili mtoto wa dada yake, kabla naye kuuawa kwa
kupigwa mawe na kisha mwili wake kuchomwa moto.
Yonah
Mwamwele (38), ndiye aliyekuwa wa kwanza kumuua mtoto Johnson Mwamwele (5)
mtoto wa dada yake kwa kutumia sululu.
Lakini
ghafla, naye alijikuta akivamiwa na kundi la watu wenye hasira na kuanza
kumshambulia kwa ngumi na silaha za jadi yakiwemo mawe hadi kumtoa uhai, na
kisha kuuteketeza kwa moto mwili wake.
Hayo
yamethibitishwa na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya, Ahmed Msangi aliyesema
tukio la kwanza lilitokea jana saa 5:30 asubuhi katika eneo hilo la Nsalaga.
Msangi
alisema kabla ya kumuua mpwa wake, Mwamwele alikuwa anamkimbiza mtoto huyo
aliyekuja kubainika kuwa ni wa dada yake ambaye aliamua kukimbilia kwenye
nyumba inayoendelea kujengwa iliyopo mtaani hapo, ambapo ndani yake walikuwepo
mafundi wakiendelea na ujenzi.
“Mafundi
walipomuona mtoto huyo akiingia na kufuatiwa na Mwamwele, walijaribu kumsihi
ili amuache mtoto huyo, lakini aliwatishia
sululu aliyokuwa ameishika mkononi ambapo mafundi hao waliogopa na
kurudi nyuma ambapo alipata nafasi ya kuingia ndani," alisema Msangi.
Kwa
mujibu wa Msangi, mara baada ya kuingia ndani ya nyumba hiyo, Mwamwele alimfuata moja kwa moja mtoto huyo na kumpiga
kwa sululu shingoni na kufanikiwa kutenganisha kichwa na kiwiliwili cha mtoto
huyo aliyeaga dunia papo hapo.
Aliongeza
mafundi baada ya kuona hali hiyo, walianza kupiga mayowe ya kuomba msaada,
ambapo ghafla kundi kubwa la watu lilijitokeza na kuanza kumfukuza Mwamwele
ambapo walifanikiwa kumkamata na kuanza kumpiga na baadaye waliamua kumchoma
moto hadi kuteketea na polisi walipofika eneo la tukio walimkuta tayari ameaga
dunia.
Kamanda
Msangi alisema baada ya kukamilisha kufanya mauaji hayo ya Mwamwele, wananchi
hao wenye hasira walirudi kwenye nyumba alimofia mtoto Johnson na kuanza
kuipiga mawe huku wakivunja vioo vya nyumba hiyo kwa mawe, sababu kuwa
ikielezwa wahusika walishindwa kutoa msaada kwa mtoto aliyeuawa.
Alisema
upelelezi unaendelea ili kuweza kutambua kiini cha Mwamwele kuamua kumfukuza
mtoto huyo wa dada yake na kisha kumuua kinyama kwa sululu.
*Picha ya Maktaba.
No comments:
Post a Comment