WARIOBA ASHUTUMU UBINAFSI WA VYAMA VYA SIASA KURA YA MAONI


Waziri Mkuu mstaafu na aliyekuwa Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Joseph Warioba amevitaka  vyama vya siasa kuzingatia matakwa ya wananchi katika suala zima la Kura ya Maoni  ya Katiba Inayopendekezwa na badala ya kuwagawa.

Aidha, Warioba amesema anaamini baadhi ya vipengele vilivyokataliwa katika Rasimu ya Katiba, ipo siku  vitafanyiwa kazi kuondoa migongano huku akisisitiza, kisheria kura ya maoni  siyo mwisho wa mchakato.
Warioba alisema kwa  sasa,  badala ya kuwaweka wananchi  pamoja na kukubaliana wanachotaka , upo mvutano huku wengine wakitaka Katiba Iliyopendekezwa ikubaliwe na wengine wakitaka wananchi waikatae.
“Kwa suala hili la kundi la Ukawa kuwasihi wafuasi wake kutoshiriki katika upigaji kura ya maoni, inaonyesha dhahiri hakuna maridhiano na wananchi kwani badala ya kujua matakwa yao,  vyama vya siasa vinawagawa wananchi katika suala hilo jambo ambalo linaonyesha vyama hivyo vinajitazama vyenyewe,” alisema.
Alikuwa akizungumza katika kipindi cha Dakika 45 kinachorushwa na kituo cha runinga cha ITV.
Alisema suala la kupiga kura ya maoni ni kuangalia maridhiano na wananchi na si vyama vya siasa. Alisema hata katika mchakato wa awali,  waliangalia maridhiano ya  wananchi na walihakikisha maoni yao yanaingia kwenye Katiba pendekezwa.
Alisema vyama vya siasa vinataka maridhiano yao bila  kuangalia matakwa ya wananchi na kukubaliana jambo, alilosema ni tatizo.
Alisisitiza kwamba anaamini baadhi ya vipengele vilivyokataliwa, ipo siku vitafanyiwa kazi kuondoa migongano.
Alisema katika Katiba Inayopendekezwa, suala la mgawanyo wa madaraka halijaainishwa lakini anavyoona maendeleo katika dunia  na matatizo, ipo siku lazima madaraka yatenganishwe, kwani kutakuwa na migongano kati ya Serikali na Bunge.
Alisema ingawa masuala hayo hayajaingizwa katika Katiba Inayopendekezwa, kama ilivyokuwa kwenye rasimu iliyoandaliwa na Tume aliyokuwa akiiongoza,  anaamini kutakuwa na mabadiliko kabla ya kura ya maoni au baada kwa kuwa hayaepukiki.
 “Matatizo haya ya wazi ya masuala kama ya mgongano wa madaraka na Muungano yatafanywa kabla au baada ya kura ya maoni kwani kuna mambo katika Katiba pendekezwa hayawezi kutekelezwa na hayazungumziki,” alisema.
Akizungumzia suala la maadili,Warioba alisema sheria ya maadili ipo, lakini haina nguvu kama ilivyokuwa kwa nchi nyingine.  Alitoa mfano wa Ufilipino akisema walikuwa na sheria hiyo lakini wakaweka kwenye katiba iwe rahisi kutekelezwa. Alitaja pia  Namibia  na  Kenya.
Alisema suala la mgawanyo wa madaraka bado ni muhimu kwani kwa kutenganisha, kunaweza kusaidia katika uwajibikaji . Alitoa mfano wa sakata la  Tegeta Escrow bungeni na kusema Bunge na Serikali ziliingiliana madaraka badala ya  serikali kuwa na kauli moja.
“Hebu angalia suala la Bunge kumfukuza Katibu Mkuu, hii siyo kazi yake, lilichanganya madaraka, kama Bunge haliridhiki na mwenendo wa serikali haliwezi kwenda kufukuza watumishi wa serikali. Bunge linatakiwa kusema kutokuwa na imani na serikali na siyo kufurahia kusema fulani afukuzwe. Siyo utaratibu mzuri,” alisema.
Waziri Mkuu huyo mstaafu alisema kazi ya Bunge ni kusimamia serikali na siyo kufukuza watu, kwani wakati mwingine kunakuwa na suala la visasi na kufukuza watumishi ambao hawahusiki.
Kuhusu Muungano, alisema,  “Hili jambo ni ‘serious’(nyeti) lazima kufika wakati kuwa na nchi moja na hata kuangalia jinsi ya kuweka sawa suala la muundo wa serikali.”
Alisisitiza  msimamo wake kwamba yeye ni muumini wa Muundo wa serikali mbili kwenda moja na siyo muumini wa serikali tatu. Alipendekeza kwenda hatua kwa hatua hata baada ya miaka 100 kupata serikali moja.
Warioba alisema  siku ya  kupiga kura ya maoni, inaweza kubadilishwa kwani haiko kisheria na haitaathiri mchakato wa kupata Katiba mpya.
Alisema tarehe ya kupiga kura, imewekwa na wanaohusika na inaweza kuahirishwa kwa kadri wanavyoona maandalizi yamekamilika katika kuandikishwa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura.

8 comments:

Anonymous said...

Undeniably believe that which you said. Your favorite justification appearedd to be on the net the easiest thing to be aware of.
I say to you, I definitely get irked while people consideer worries tjat
they plainly don't know about. You managed to hit the nail upon the topp and defined out the whole
thing without having side effect , people can take a signal.
Will likely be back to get more. Thanks

Anonymous said...

Can you tell us more about this? I'd like to find out more details.

Anonymous said...

Simplу desire to saү yоur article is as astounding.
The clarity in your ost is just excellent and i can asѕume
you're an expert on this suƅject. Fine with уour permission let mme to grab y᧐ur fеed to
keep upp to dаte with forthcoming ρost. Thаnks a milliߋn and
pleаse carry оnn the rewarding work.

Anonymous said...

I loved ɑѕ mudh ɑs you'll receive carried
out right hегe. The skegch iss tasteful, your authored subject
matter stylish. nonetһeless, уou command gеt bought an impatience ovеr that ʏⲟu wish be delivering
the fⲟllowing. unwell unquestionably come fuгther formеrly agaіn as exаctly the same nearly vewry often іnside cas you shiwld tһis hike.

Anonymous said...

Remarkable issues һere. I'm νery happy to see your article.

Thɑnks a lot ɑnd I am taking a lokok forward tօ touch
you. Will you kindly drop me а mail?

Anonymous said...

Hmm it looks ⅼike youг website ate my first comment (it waѕ super long) so
Ӏ guess I'll ϳust sum іt uр what I submitted and say, I'm thorougһly enjoying yoᥙr blog.І too am an aspiring blog
writer but І'm stiⅼl neᴡ tоo everything.
Ꭰo уou haᴠe any helpful hints for inexperienced blog writers?
І'd certainly aрpreciate іt.

Anonymous said...

What's uup everүone, іt'ѕ my first pay а quick visit at
thyis website, and post iѕ in fact fruitful designed
f᧐r me, қeep up posting theѕе types оf posts.

Anonymous said...

Υоur style is reɑlly unique іn comparison to otheг
people I've read stuff from. Ӏ appreciate you for posting ᴡhen yoս've
got the opportunity, Guess I wіll ϳust book
mark tһis web site.