Tani 200,000 za silaha haramu zilizokuwa zimezagaa
nchi za Jumuiya ya Afrika ya Mashariki (EAC) zimeteketezwa.
Hayo yalisemwa jana na Katibu Mkuu wa EAC, Richard Sezibera (pichani) mbele ya
Rais wa Shirikisho la Ujerumani, Joachim Gauck
wakati alipozuru makao makuu ya jumuiya hiyo, jana.
Alisema silaha hizo zilizokamatwa kwa nyakati tofauti katika nchi
mbalimbali za EAC ni pamoja na mabomu
tani 200.
Akizungumzia ujio wa Rais wa Ujermani katika makao makuu ya Jumuiya
hiyo, Sezibera alikiri kufurahishwa na ujio huo na kusema kuwa utaongeza chachu
ya nchi hiyo kuisaidia jumuiya hiyo.
Sezibera alisema mahitaji makubwa yanahitajika katika kufanikisha
mahitaji ya wananchi wa EAC ikiwa ni pamoja na Afya, Mazingira, Miundombinu na
vikundi vya akina mama na vijana wanachama wa jumuiya hiyo.
Naye Rais Gauck alizitaka nchi hizo kudumisha jumuiya hiyo na kuiboresha
zaidi ikiwa ni njia mojawapo ya kuweka mshikamano kwa maslahi ya wananchi wake.
Alisema kuwa nchi ya Ujerumani na nchi nyingine za Ulaya zitakuwa mstari
wa mbele kuhakikisha zinatoa misaada kwa jumuiya hiyo bila ya kikwazo chochote.
Awali, Rais huyo alifanya ziara katika Mahakama ya Afrika ya Haki za
Binadamu iliyopo jijini Arusha kujionea utendaji kazi wa kila siku wa jumuiya
hiyo na kujua changamoto zake.
No comments:
Post a Comment