SUMATRA YAZUIA VYOMBO VYA USAFIRI WA MAJINI
Mamlaka ya Usafirishaji wa Nchi Kavu na Majini
(Sumatra) imevizuia kutoa huduma kwa muda usiojulikana vyombo vyote vya
usafirishaji wa majini vya mkoani hapa hadi hapo vitakapokaguliwa.
Ofisa Mfawidhi wa
Sumatra Mkoa wa Tanga, Walukani Luhamba ametoa kauli hiyo wakati akifungua
kikao cha pamoja na maofisa uvuvi na askari wa majini kilichofanyika jijini
humo jana.
Alisema kuna umuhimu
wa kisheria kwa vyombo vyote vya usafiri kuhakikisha vinakaguliwa na maofisa wa
Sumatra ili kuhakikisha ubora na usalama safarini.
“Kutokana na ongezeko
la ajali za baharini, Sumatra kuanzia sasa hapa mkoani tumeamua kuvihakiki upya
ili tuweze kujiridhisha kwamba vyombo vyote vinavyotumika kusafirisha abiria au
mizigo vinakuwa kwenye hali ya ubora na usalama unaostahili
kabla ya safari,” alisema.
Luhamba alisema
pamoja na kwamba vyombo hivyo vilishasajiliwa kufanya shughuli za usafirishaji
abiria na uchukuzi wa mizigo mbalimbali lakini kigezo hicho hakitoshelezi
kuridhia kwamba viko katika usalama unaohitajika safarini.
No comments:
Post a Comment