Mamlaka ya Udhibiti
Usafirishaji wa Nchi Kavu na Majini (SUMATRA), imewanoa wamiliki wa mabasi ya
masafa marefu kuhusu usimamizi na udhibiti wa sekta ya usafiri wa
barabara ili wazaidie kupunguza na kutokomeza kabisa ajali baada ya
kuwapatia semina maalumu.
Semina hiyo maalumu ya siku mbili iliyoanza juzi mjini
Morogoro imewashirikisha viongozi wa Chama cha Wamiliki wa Mabasi Tanzania (
TABOA) wakiongozwa na Mwenyekiti wao Taifa, Mohamed Hood, na kufunguliwa na
Katibu Mkuu wa Wizara ya Uchukuzi, Dk Shaaban Mwinjaka.
Dk Mwinjaka katika hotuba yake ya ufunguzi,
aliwataka wamiliki wa mabasi kuwatumia madereva wenye
weledi ili kupunguza ajali ikiwa na hatua ya kuwaendeleza kielimu
katika vyuo vya serikali na vya ufundi stadi Veta.
Mbali na hayo, aliwataka wamiliki wa mabasi
kushirikiana na vyombo vingine kwa ajili ya kubaini mienendo ya madereva
wao hasa suala la ulevi wanapokuwa kazini na mwendokasi, wakitambua
mabasi yao wameyanunua kwa gharama kubwa na pia yamebeba uhai wa maisha
ya binadamu.
Hata hivyo, alisema aliwahakikishia wamiliki wa mabasi ya masafa
marefu kuwa, Kamati iliyopewa jukumu ya kuangalia namna ya kurekebisha sheria
za makosa yanayowahusu wamiliki na kwa madereva wao imefikia hatua nzuri na
muda si mrefu utawekwa hadharani.
Pamoja na hayo, pia aliwataka wamiliki wa mabasi
kuhakikisha wanakuwa karibu kufuatilia kila jambo linalofanywa na dereva
wake, kwani mwisho wa yote basi litabaki kuwa ni mali ya mmiliki na dereva ni
mfanyakazi wake.
Naye Kamanda wa Kikosi cha Usalama Barabarani nchini,
Mohamed Mpinga alisema ajali za barabarani zinazohusisha
mabasi hazitaweza kupungua iwapo sheria na kanuni za
mwaka 2007 kanuni 317 hazitazingatiwa na wamiliki wa vyombo
hivyo sambamba na madreva wao.
Naye Mkurugenzi Mkuu wa SUMATRA, Gilliard
Ngewe, mada sita ziliandaliwa na kutolewa kwa wamiliki wa mabasi ya
masafa marefu, ikiwemo ya nafasi ya wamiliki wa vyombo vya usafiri katika
kuimarisha usalama barabarani sambamba na nyingine ya kanuni ya taratibu za
uwasilishaji makalamiko.
No comments:
Post a Comment