Timu
ya Simba leo jioni ilitoa kipigo kikali kwa Prisons ya Mbeya kwa kuibugiza mabao 5-0
katika mchezo wa Ligi Kuu Tanzania bara uliopigwa Uwanja wa Taifa Dar es
Salaam.
Ushindi huo mnono
wa Simba umekuja wiki moja baada ya kupata kipigo cha bao 1-0 na Stand United
mjini Shinyanga.
Katika mchezo huo,
Simba walianza kuhesabu bao la kwanza kupitia kwa mshambuliaji wake, Ibrahim
Hajibu katika dakika ya 15 akiunganisha krosi nzuri ya Dan Sserunkuma.
Hajibu aliongeza
bao la pili katika dakika ya 21 baada ya kuuwahi mpira uliotemwa na golikipa
Mohammed Yussuf, aliyepangua shuti la Emmanuel Okwi kabla ya kufunga bao la
tatu dakika ya 41 kwa mkwaju wa penalti.
Penalti hiyo ilitolewa
baada ya beki wa Prisons, Lugano Mwangama kuunawa mpira kwenye eneo la hatari
akiwa katika heka heka za kuokoa hatari langoni mwake.
Mabao mengine ya
Simba yalifungwa na Emmanuel Okwi katika dakika ya 75 kwa shuti kali na
Ramadhani Singano maarufu kama Messi akifunga dakika ya 84 na kuhitimisha
karamu ya mabao kwa kikosi hicho.
Katika mchezo huo,
Nurdin Chona wa Prisons alitolewa nje katika dakika ya 68 kwa kadi ya pili ya
njano baada ya kumtolea maneno machafu mwamuzi.
Kwa ushindi huo,
Simba sasa imefikisha pointi 23, baada ya kushuka dimbani mara 16, ikiwa nafasi
ya nne nyuma ya Kagera Sugar yenye pointi 24, Azam FC pointi 27 na Yanga SC 31.
Simba: Ivo Mapunda, Hassan Kessy/Nassor
Masoud ‘Chollo', Mohammed
Hussein ‘Tshabalala’, Hassan Isihaka, Joseph Owino, Jonas
Mkude, Ramadhani Singano ‘Messi’, Said Ndemla, Dan Sserunkuma/Twaha
Ibrahim ‘Messi’, Ibrahim Hajib/Awadh Juma na Emmanuel
Okwi.
Prisons; Mohammed Yussuf, Lugano Mwangama,
Laurian Mpalile, James Mwasote, Nurdin Chona, Jumanne Elfadhil/John Mathei,
Adam Chimbongwe/Meshack Suleiman, Freddy Chudu, Ibrahim Isaka, Boniface
Hau/Julius Kwanga na Godfrey Magetha.
No comments:
Post a Comment