Wizara ya Kazi na Ajira iko katika
mchakato wa kuandaa Sheria mpya ya utoaji wa vibali vya ajira kwa wageni ili
kudhibiti kuajiriwa kwa wageni ili kufanya kazi ambazo Watanzania wenyewe
wanaweza kuzifanya.
Alisema mchakato huo uko karibu kukamilika na utapelekwa bungeni
kutokana na ratiba na kueleza kuwa itasaidia kudhibiti wafanyakazi wageni
wanaoingia nchini bila utaratibu maalum na kusababisha kuajiliwa kwenye kazi
ambazo wenyeji wanaweza kufanya.
Waziri katika wizara hiyo, Gaudentia Kabaka aliliambia Bunge kuwa sheria
hiyo itatoa mwongozo juu ya utoaji vibali, kwani sasa kumekuwa na sehemu nyingi
hivyo kuwa na sehemu moja pamoja na adhabu kwa wageni wanaofanya kazi
zinazoweza kufanywa na Watanzania.
Alisema hivi karibuni walibaini wageni 300 walioingia nchini kufanya
kazi katika kiwanda cha saruji cha Dangote, Mtwara kwa kazi zinazoweza kufanywa
na watanzania.
Wakati huo huo, wafanyakazi zaidi ya 350 wa Kampuni ya mgodi wa
Bulyanhulu waliodai kuachishwa kazi baada ya kupata madhara wakiwa kazini
wametakiwa kwenda kwenye Wakala wa Usalama na Afya Mahali pa Kazi
(OSHA) kupimwa ili kuthibitisha iwapo walipata madhara hayo kutokana na
kazi walizokuwa wakifanya ili kuweza kutibiwa.
Alisema kuwa OSHA ndiyo wenye mamlaka ya kuthibitisha kuwa wafanyakazi
hao wameathirika na kwa utaratibu walitakiwa kupeleka OSHA barua kutoka
kwa mwajiri ili kuweza kupimwa na kujua athari walizopata wakiwa kazini lakini
tangu wafukuzwe kazi mwaka 2007 hawakupeleka barua hiyo.
“Tumegundua kuwa wafanyakazi hao hawakuwa na uhusiano mzuri na chama cha
wafanyakazi hivyo kusababisha ufuatiliaji wa suala hilo kuwa mgumu hivyo
ninawaagiza kwenda OSHA Dar es Salaam wakapime kwani wako tayari wao pamoja na
wengine 50 waliofukuzwa “alisema Kabaka.
Pia alitaka chama cha wafanyakazi migodini (TAMICO) kuwaunganisha
wafanyakazi hao ili kufuatilia kwa pamoja na kuepusha kuwa mmoja mmoja.
Mbunge wa Kisarawe, Suleiman Jafo (CCM) alisema wafanyakazi hao wamekuwa
wakihangaika katika ofisi mbalimbali ikiwemo kwenye Wizara ya Kazi na Ajira
kufuatilia suala hilo.
No comments:
Post a Comment