Waziri Mkuu,
Mizengo Pinda ameeleza sababu za Bunge kushindwa kujadili miswada kadhaa,
ikiwemo uliohusu Marekebisho ya Sheria ya Kiislamu, inayotambua Mahakama ya
Kadhi.
Akihitimisha
shughuli za mkutano wa 18 wa Bunge jana, Pinda alisema muswada huo umesogezwa
mbele, ili Kamati ya Bunge ipate nafasi na muda wa kupitia na kutoa ushauri kwa
Bunge.
Muswada wa
Sheria ya Marekebisho ya Sheria mbalimbali Namba 2 wa mwaka 2014, unaohusu
Muswada wa Marekebisho ya Sheria hiyo ya Kiislamu Sura 375 ni miongoni mwa
ambayo haikujadiliwa.
Mingine
iliyopangwa kujadiliwa katika mkutano huo wa Bunge, ni Muswada wa Sheria
ya Usimamizi wa Kodi wa mwaka 2014 na Muswada wa Sheria ya Takwimu wa mwaka
2013.
“Hatukuweza
kuijadili miswada hiyo katika mkutano huu, ili Kamati husika zipate nafasi na
muda wa kupitia na kutoa ushauri kwa Bunge lako Tukufu.
“Ni matumaini
yangu kwamba miswada hii itapata nafasi ya kuwasilishwa na kujadiliwa katika
mkutano ujao wa 19 wa Bunge lako Tukufu,” alisema Pinda.
Katika mkutano
huo, wabunge walipokea na kujadili taarifa mbalimbali zilizowasilishwa na
Kamati za Bunge za kisekta na zisizo za kisekta.
Wakati huo huo
katika hotuba yake, Pinda aliwaambia wabunge kwamba hali ya uzalishaji na
upatikanaji wa chakula nchini kwa ujumla, imeendelea kuwa ya kuridhisha katika
maeneo mengi, kutokana na mavuno mazuri katika msimu wa kilimo wa 2013/2014.
Kuhusu mwenendo
wa malipo ya madeni ya ununuzi wa mahindi kwa msimu wa 2014/2015, Pinda alisema
hadi kufikia Desemba 2014 Serikali ilikuwa inadaiwa Sh bilioni 89 na wakulima
waliouuzia Wakala wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula (NFRA) mahindi.
Hadi kufikia
Januari 29 mwaka huu, kwa mujibu wa Waziri Mkuu, Serikali ilikuwa imelipa
wakulima hao Sh bilioni 15 na kubakiza deni la Sh bilioni 74.
Alisema katika
juhudi za Serikali za kutatua changamoto ya deni hilo, mwezi huu
inatarajia kulipa Sh bilioni 40 na kubakia na deni la Sh bilioni 34 ambazo
zitalipwa kutokana na mkopo wa benki ya CRDB wa Sh bilioni 15 na Bajeti ya
Serikali.
No comments:
Post a Comment