MAMA WA MTOTO ALBINO ASIMULIA JINSI ALIVYOJERUHIWA
Mama wa mtoto mwenye ulemavu wa ngozi, Yojana Bahati
(1), Ester Thomas aliyelazwa katika hospitali ya Bugando akipatiwa matibabu
baada ya kujeruhiwa, ameelezea jinsi alivyovamiwa na watu wasiojulikana.
Akizungumza na
mwandishi, Ester (30) alisema alijeruhiwa juzi nyakati za usiku
na watu wasiojulikana mkoani Geita baada ya kumvamia nyumbani kwao na kumpora
mtoto wake mwenye ulemavu wa ngozi.
Akizungumza kwa shida
hospitalini hapo, Ester alisema alivamiwa akiwa amelala na mtoto wake huyo
ambapo walimkatakata kwa mapanga sehemu mbalimbali za mwili na kisha kutokomea
kusikojulikana.
Naye Mkuu wa kitengo
cha dharura hospitalini hapo, Dk Derick David alisema mgonjwa huyo
alipokewa juzi saa nane mchana akitokea mkoani Geita.
Daktari alisema
mgonjwa huyo ambaye hali yake sio ya kuridhisha, alijeruhiwa sehemu mbalimbali
za mwili kutokana na kukatwa panga kwenye paji la uso pamoja na kukata sehemu
ya mfupa wa pua.
"Tunamshukuru
Mungu mgonjwa huyu anaendelea vizuri baada ya kufanyiwa upasuaji kwani kwa sasa
hali yake ni tofauti na alivyopokewa," alisema.
Alisema mama huyo
anaendelea na matibabu ya majeraha na pia atapatiwa na huduma ya kisaikolojia
kutokana na maumivu makali aliyonayo ya kuporwa kwa mtoto wake.
No comments:
Post a Comment