Mchumi wa Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo
ya Makazi, Brown Kajange (42) amefikishwa katika Mahakama ya Mwanzo
Kariakoo kujibu mashitaka mawili, likiwamo la shambulio la aibu kwa kumshika
matiti mwanamke bila ridhaa yake.
Karani wa Mahakama hiyo, Blanka Shao alidai
mahakamani hapo mbele ya Hakimu Matrona Luanda kuwa mshtakiwa alitenda kosa
hilo Februari 16, mwaka huu katika eneo la kuuzia samaki la Feri Kivukoni
wilaya ya Ilala.
Shao alidai siku ya tukio saa 6 mchana katika
eneo hilo, mshtakiwa alimshika matiti Queensia Fusi bila ridhaa yake huku
akijua kufanya hivyo ni kinyume cha sheria.
Alidai kuwa shtaka la pili, mshtakiwa alimpiga
ngumi mlalamikaji katika jicho la kushoto na kusababisha maumivu
makali katika sehemu hiyo.
Mshtakiwa alikana mashtaka na Hakimu
Luanda aliahirisha kesi hiyo hadi Machi 3, mwaka huu itakapotajwa.
Mshtakiwa yupo nje kwa dhamana baada ya
kutimiza masharti ya dhamana ya kuwa na mdhamini mmoja mwenye barua
kutoka serikali ya mtaa, atakayesaini bondi ya Sh 300,000.
1 comment:
Baccarat | Play at UK's #1 Online Casino
Play at UK's #1 Online febcasino.com Casino. 바카라 사이트 Our website is updated regularly worrione with new casino games https://sol.edu.kg/ and online casino games. Read reviews, find bonuses and get latest 메리트카지노 news.
Post a Comment