Wakazi wa kijiji cha Uchindile wilayani Ifakara mkoani Morogoro
wamepata umeme unaozalishwa kwa kutumia kuni baada ya kuzinduliwa kwa mtambo wa
10kW uliotolewa na kampuni ya kimataifa ya Camco Clean Energy.
Mtambo huo wenye thamani ya zaidi ya Sh
milioni 75 ulizinduliwa na Mwakilishi wa Shirika la Misaada la Marekani
(USAID), Rogness Swai katika hafla iliyohudhuriwa na wadau mbalimbali wa sekta
hiyo, wakiwemo wananchi wa kijiji hicho.
Pamoja na Camco Clean Energy Tanzania
iliyofadhiliwa na USAID ili kufanikisha mradi huo utakaokabidhiwa kwa serikali
ya kijiji hicho, Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni hiyo nchini, Jeff Felten
aliwataja wengine waliochangia ujenzi wake kuwa ni kampuni ya Village
Industrial Power (VIP) na Kiwanda cha Karatasi cha Mufindi (MPM) cha Mgololo,
wilayani Mufindi.
Felten alisema mtambo huo utawezesha kaya 100
kati ya 265 za kijiji hicho kilichopo zaidi ya kilomita 100 toka Mafinga,
wilayani Mufindi mkoani Iringa kuwa za kwanza nchini kunufaika na nishati hiyo
inayotarajiwa pia kuzinduliwa mkoani Kigoma hivi karibuni.
No comments:
Post a Comment