Kamati Kuu ya CCM (CC) iliyosubiriwa kwa muda
mrefu, hatimaye inakutana leo na suala kubwa linalotarajiwa na wanachama na
wananchi, ni tathmini ya hukumu ya vigogo sita wa chama, waliokuwa wakitumikia
adhabu baada ya kubainika kuanza kampeni za urais mapema.
Vigogo
ambao tathmini ya mwenendo wao inasubiriwa baada ya kikao hicho ni pamoja na
waliokuwa mawaziri wakuu, Edward Lowassa na Frederick Sumaye na Waziri wa Mambo
ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe.
Wengine
ni Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, January Makamba ambaye
ameshatangaza nia ya kugombea urais, Waziri wa Kilimo na Ushirika, Stephen
Wassira na Mbunge wa Sengerema, William Ngeleja.
Mwanzoni
mwa wiki hii, Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye, alitoa taarifa kwa
vyombo vya habari, ikielezea kuwepo kwa kikao cha Kamati Kuu leo
kitakachoongozwa na Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete.
Ingawa
ajenda za kikao hicho hazikuwekwa wazi, lakini tayari duru za siasa na
wachambuzi mbalimbali, walishaanza kuzungumzia umuhimu wa ajenda ya tathmini ya
hukumu ya makada hao, kwa kuwa muda wa kutumikia adhabu hiyo ya mwaka mzima
ulikamilika katikati ya mwezi huu.
Vigogo
hao wanaotajwa kutaka kuwania urais, walipewa adhabu hiyo ya onyo kali na
Kamati Kuu Februari 18, mwaka jana baada ya kuthibitika kuanza kampeni za
kutafuta kuteuliwa kugombea urais kabla ya wakati, kinyume na kanuni za uongozi
na maadili za CCM Toleo la Februari 2010, Ibara 6(7) (i).
Vilevile baada ya kuhojiwa, walithibitika kufanya vitendo vinavyokiuka maadili ndani ya chama na baadhi yao kufanya vitendo vinavyokiuka maadili ndani ya jamii.
Kutokana na adhabu ya onyo kali, vigogo hao kwa mwaka mzima walikuwa katika hali ya kuchunguzwa, ili kuwasaidia katika jitihada za kujirekebisha.
Pia kamati ndogo ya udhibiti iliagizwa kuchunguza na kuchukua hatua kwa wote waliohusika kwa namna moja au nyingine, katika vitendo hivyo vilivyovunja kanuni za chama.
Moja
ya vitu vinavyosababisha wachambuzi wa siasa kuamini umuhimu wa ajenda hiyo
katika kikao cha leo, ni tamko la chama hicho lililotolewa Januari mwaka huu,
baada ya kumalizika kwa kikao cha Kamati Kuu.
Katika
tamko hilo, CCM iliweka wazi kuwa baada ya kukamilika kwa adhabu hiyo, Kamati
Kuu ndio kikao ambacho kingefanya tathmini ya utekelezaji wa adhabu hiyo kwa
vigogo hao.
Tamko
hilo lilienda mbali zaidi na kubainisha kuwa, vigogo ambao watabainika katika
kikao hicho cha tathmini, kuwa walikiuka
masharti ya adhabu hiyo, adhabu zao zingeongezwa.
Kabla
ya kuhukumiwa kutojihusisha na masuala ya kampeni kwa mwaka mmoja, Kamati ya Maadili ya CCM, inayoongozwa na
Makamu Mwenyekiti wa CCM Tanzania Bara, Philip Mangula, iliwahoji watuhumiwa
hao.
Miongoni
mwa wajumbe walioshiriki kuhoji watuhumiwa hao mbali na Mangula, alikuwepo
Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahaman Kinana, William Lukuvi ambaye ni Waziri wa
Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi na Shamsi Vuai Nahodha, ambaye alikuwa
Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa.
Ajenda
nyingine inayotarajiwa kunguruma katika kikao hicho ni kuhusu vigogo wa chama
hicho, waliokumbwa na kashfa ya Akaunti ya Tegeta Escrow.
Kikao
cha Kamati Kuu ya CCM cha Januari kilichoketi Zanzibar, kilieleza kusikitishwa
kwake na baadhi ya viongozi wake walio katika dhamana ya kisiasa kukumbwa na
kashfa hiyo.
Aidha,
kiliagiza Kamati ya Maadili kuchukua hatua za kimaadili kwa wale wote
waliohusika na ukiukaji wa maadili kwenye sakata la Escrow, ambao wako kwenye
vikao vya uamuzi vya chama.
Wanaotuhumiwa
na kukiuka maadili katika fedha hizo ni pamoja na Mbunge wa Bariadi Magharibi,
Andrew Chenge, Ngeleja na Waziri wa zamani wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya
Makazi, Profesa Anna Tibaijuka.
Mwingine
katika tuhuma hizo, ni aliyekuwa Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter
Muhongo.
Vilevile baada ya kuhojiwa, walithibitika kufanya vitendo vinavyokiuka maadili ndani ya chama na baadhi yao kufanya vitendo vinavyokiuka maadili ndani ya jamii.
Kutokana na adhabu ya onyo kali, vigogo hao kwa mwaka mzima walikuwa katika hali ya kuchunguzwa, ili kuwasaidia katika jitihada za kujirekebisha.
Pia kamati ndogo ya udhibiti iliagizwa kuchunguza na kuchukua hatua kwa wote waliohusika kwa namna moja au nyingine, katika vitendo hivyo vilivyovunja kanuni za chama.
No comments:
Post a Comment