Chama
cha Wananchi (CUF) kimetangaza Mwenyekiti wa Taifa wa chama hicho, Profesa
Ibrahim Lipumba, kuwa ni mmoja kati ya wanachama wa chama hicho, atakayewania
nafasi ya Urais.
Pia
chama hicho, kimetoa rasmi ratiba ya uchukuaji fomu na utaratibu wa kura ya
maoni kwa wagombea wa nafasi mbalimbali za uwakilishi katika uchaguzi mkuu
unaotarajiwa kufanyika mwaka huu wa udiwani, ubunge, uwakilishi na urais, na
hadi ifikapo Aprili 25, chama hicho kitakuwa kimekamilisha uteuzi wa wagombea
ubunge na uwakilishi.
Akizungumza
na waandishi wa habari Dar es Salaam, Mkurugenzi wa Oganaizesheni na Uchaguzi
wa chama hicho, Shaweji Mketo alisema kati ya wagombea waliojitokeza mpaka sasa
kuwania nafasi hiyo ya urais ni Profesa Lipumba pekee.
“Kwa
upande wangu mie kama Mkurugenzi wa Uchaguzi nina imani na Profesa Lipumba,
kuwa atakuwa ndiye mgombea wetu wa urais tu kwa CUF bali hata kwa upande wa
Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa),” alisema Mketo.
Alisema
kwa mujibu wa makubaliano baina ya Ukawa, kila chama ni lazima kichague na
kuweka wagombea katika nafasi na majimbo yote ikiwemo Urais na baadaye ndipo
watakapochambua ni wagombea wangapi wabaki na akina nani waondoke na kwa nini.
Akizungumzia
ratiba ya kuchukua fomu na kura ya maoni kwa wagombea wa chama hicho, alisema
chama hicho kimeamua kujiandaa mapema kutafuta wagombea watakaokiwakilisha
katika uchaguzi huo mkuu ambao pia watachujwa kupitia utaratibu wa kura za
maoni.
Alisema
kwa upande wa wanaotaka kuwania nafasi ya udiwani, fomu zitaanza kutolewa Machi
Mosi hadi Machi 10, mwaka huu, na fomu hizo ambazo kila atakayezichukua
atazilipia Sh 10,000 zitafikishwa kwa Katibu wa Kata Machi 11 hadi 13 mwaka huu
kwa ajili ya utaratibu wa juu zaidi.
Kwa
upande wa nafasi ya ubunge, alisema fomu hizo zitakazolipiwa Sh 50,000 zitaanza
kutolewa nazo Machi Mosi hadi Machi 10, na Machi 15 hadi 30 mwaka huu, mikutano
ya kata ya kura za maoni kwa nafasi ya udiwani itaanza kufanyika.
Mketo
alisema kuanzia Machi 11 hadi 20, mwaka huu, Katibu wa kata wa chama hicho
atazifikisha fomu za wagombea nafasi ya ubunge kwa Katibu wa wilaya na baada ya
hapo maandalizi ya mikutano mikuu ya wilaya kwa ajili ya kura za maoni itaanza
kuanzia Machi 31 hadi Aprili 4, mwaka huu.
Alisema
kuanzia Aprili 5 hadi 15 mwaka huu, mikutano ya wilaya na majimbo ya kura ya
maoni itafanyika na baada ya hapo Kurugenzi itafanya uchambuzi wa fomu za
wagombea ubunge ili kuziwasilisha kwa Kamati ya Utendaji ya Taifa kuanzia
Aprili 17 hadi 19, mwaka huu.
Aidha
alisema kikao cha Kamati ya Taifa kwa ajili ya kuweka sifa za wagombea ubunge
kinatarajiwa kufanyika kuanzia Aprili 20 hadi 21, mwaka huu, na kikao cha
Baraza Kuu la Uongozi la Taifa kitafanyika kuanzia Aprili 22 hadi 23, mwaka
huu.
Na
kuanzia Aprili 24 hadi 25, mwaka huu, chama hicho kupitia Baraza Kuu la uongozi
kitafanya uteuzi wa mwisho kwa wagombea wa ubunge na uwakilishi.
Kuhusu
ratiba ya kuchukua fomu kwa wagombea wa urais, alisema bado wanasubiri kikao
cha pamoja cha Ukawa ambacho kitafanyika muda wowote kuanzia sasa,
kitakachoweka taratibu za kuwatafuta wagombea urais.
Pamoja
na hayo, Mketo alitupia lawama Jeshi la Polisi na kulituhumu kutumiwa vibaya na
chama cha CCM, ambapo wanachama wake takribani nane waliopo mikoa ya Kusini
wamekamatwa kwa tuhuma za ugaidi na hadi sasa hawajafikishwa mahakamani.
“Katika
uchaguzi wa Serikali za Mitaa chama chetu kilifanya vizuri katika maeneo yote
ya kusini na kutokana na matokeo haya, tuna uhakika wa kufanya vizuri katika
uchaguzi wa wabunge, sasa CCM wameona hivyo wanatumia polisi, kukamata viongozi
wetu wanaoona ni tishio kwa kisingizio cha ugaidi,” alisisitiza.
No comments:
Post a Comment